MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
UTENZI: UMUGANURA

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
UTENZI: UMUGANURA
#1
   

UMUGANURA
----------------
UMUGANURA ni siku,
maarufu Rwanda ino.
Maeneo yote huku,
ni sherehe ya mavuno.
-------
Ni Ijumaa ya kwanza,
ya kulla wa nane mwezi.
Sikukuu tunafanza,,
kimila tukiuenzi.
-------
UMUGANURA 'likuwa,
desturi asilia.
Wanajamii wakiwa,
pamwe wanafurahia.
---------
Nafaka pia maziwa,
wahenga walichangia.
Nazo nyama zililiwa,
togwa na kangara pia.
--------
Sikukuu ya mavuno,
kwetu ndo UMUGANURA.
Siku ya makongamano,
kukumbuka ya kikwetu.
--------
Twala mapishi ya jadi,
na vinywaji kutumia.
Tukipeana zawadi,
umoja kuzingatia.
-------
Mila za Waafurika,
sana zakaribiana.
Mshairi mshirika,
n'kusaili muungwana.
--------
Hini siku ya mavuno,
tunayoienzi sana,
jamii ya pande zino,
kwenu inapatikana?
-------
Utenzi natamatisha,
wasanii n'kiwaomba,
milazo kunijulisha,
awabariki MUUMBA.
=============
Rwaka rwa Kagarama
(Mshairi Mnyarwanda),
Jimbo la Mashariki,
Wilaya ya Nyagatare,
R W A N D A.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)