MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MISEMO YA VYOMBO VYA USAFIRI (2)

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
MISEMO YA VYOMBO VYA USAFIRI (2)
#1
Misemo yenye Ujumbe kuhusu Maisha kwa Ujumla
 
      1. “Ajali sio kugongwa na gari tu, hata kukosea kuoa au kuolewa pia ni ajali”
 Maana:
·    Kuoa au
kuolewa ni jambo linalopaswa kufanywa kwa umakini sana.
·    Ndoa njema
ni kiini cha furaha na mafanikio; ndoa mbaya ni kiini cha faraka na maangamio
ya kimaisha.
·   Waoaji au
waolewa wanapaswa kuzingatia vigezo vya msingi katika kutafuta wenza wa kuishi
nao.
·   Mwenza akiwa
mkorofi ndani ya ndoa, maisha kwa ujumla huwa magumu na machungu.
       2.  “Asili haipotei”
 Maana:
·    Mambo ambayo mtu aliwahi kuyafanya katika maisha
yake ya awali hayawezi kubadilika yote hata kama atabadilisha mfumo au mtindo
wa maisha au utamaduni.
·   Mtu hawezi kusahau kwao.
·   Hata mtu awe katika maeneo ya mbali na kwao bado
vitu vya asili yake vitaendelea kubakia katika kumbukumbu zake; hivyo
atavitamani avipate.
        3.  “Bora uzima”
  Maana:
·   Vitu vyote ukose (kiuchumi, kielimu au kijamii)
lakini uzima (na uhai) uwepo.
·   Mtu hata akiwa na ulemavu wa namna yoyote, bado
sio tatizo ili mradi yuko hai.
·    Mengine yote ni ziada, kilicho muhimu ni uhai.
        4.  “Born to suffer”
  Maana:
·  Duniani ni sehemu ya kuchakarika, siyo kulegea.
·  Maisha ni kazi
·  Kiumbe yeyote anayeishi hapaswi kutetereka hata
kidogo.
·   (Mwandishi) Amezoea matatizo, shughuli ngumu,
shida na madhila mengine ya hali ngumu ya maisha.
·   (Mwandishi) hatishwi na lolote linaloambatana na
harakati za maisha.
       5.  “Chanda chema….?
  Maana:
·   Mtu anayetenda mema hutuzwa.
·   Ni vema tutende mema ili tuhifadhiwe au majina
yetu yatajwe vema hata baada ya kuondoka duniani.
·   Mambo mema huhifadhiwa vizuri na kwa fahari.
        6.  “Bora uzee kuliko uzembe”
  Maana:
·    Ni afadhali Mzee (ambaye mara nyingi nguvu huwa
zimemwishia) hufanya mambo yake taratibu na kwa umakini mkubwa, lakini
hufanikiwa au hufika mwisho; kuliko mtu mzembe ambaye huacha au husita kufanya
jambo kwa makusudi na mwisho haambulii chochote au hupata madhara.
·    Uvivu hauna faida katika maisha.
·    Vema kujitahidi katika jambo fulani lenye
mafanikio kuliko kuliacha kabisa.
       7.  “Hakuna tuzo ya ngono zaidi ya UKIMWI”
  Maana:
·    Uzinzi na Uasherati una hasara kubwa kwa mtu na
jamii; hasara kubwa ni kwa mhusika kupata maradhi kama vile UKIMWI.
       8. “Butua uwakomboe wenzako”
  Maana:
·   Tujenge tabia ya kuwasaidia wenzetu.
·   Fanya lolote uwezalo ili kuwasaidia walio chini yako.
·   Kumbuka kutumia kile ulichoruzukiwa na Mola kwa
kuwasaidia masikini.
       9. “Hata bibi alikuwa binti”
   Maana:
·   Maisha ni mapito yanayomtokea binadamu hatua kwa
hatua, hivyo, kuwa makini na kila hatua ya maisha.
·    Uhai, umri au utajiri huwa havidumu milele, bali
huisha au hubadilika baada ya muda.
·    Fanya ufanyalo lakini jua kuna kesho.
·    Kila jambo lina wakati wake.
      10.  “Bosi hanuniwi”
Maana:
·   Bosi (kiongozi) hata akikosea kwa waajiriwa wake
hawezi kuchukiwa, kwani yeye ndiye aliyeshinda maisha yao kiuchumi.
·     Mwenye mali au pesa anaweza kufanya chochote kwa
asiye nazo.
·    Katika kutafuta maisha tunaaswa kupambana na
changamoto mbalimbali zinazojitokeza.
      11.  “Bora lawama kuliko hasara”
Maana:
·    Ni bora mtu kumweleza ukweli wa jambo hata kama
hapendi, kuliko kukaa kimya na baadaye kitu kibaya kikatokea kutokana na huo
ukimya.
·    Hasara ni adui wa maendeleo.
·    Ni bora ulaumiwe kuliko kuingia matatizoni.
·    Kabla ya kukubali kufanya jambo au kitu
chochote, ni vema kuangalia na kupima matokeo yake.
.   Mtu anapaswa kuchukua uamuzi unaoleta madhara
madogo kuliko ule unaoleta madhara makubwa.
Chanzo:
Ponera, A. S na Kikula, I.S,  (2017) Misemo
ya Vyombo vya Usafiri. UDOM. Afroplus Industries, Ltd.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)