MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MWONGOZO WA MBINU ZA KUFUNDISHIA SHULE ZA AWALI

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
MWONGOZO WA MBINU ZA KUFUNDISHIA SHULE ZA AWALI
#1
Makala hii ni maalumu kwa walimu wa shule za awali. Kutambua na kuchagua Mbinu sahihi za kufundishia kwa mwalimu ni jambo muafaka katika kulea watoto.
Ikumbukwe kuwa ufundishaji wa watoto wa shule ya awali ni tofauti na ule wa shule za msingi. Mwalimu anatakiwa kuzingatia kuwa mtoto wa umri huu katika shule ya awali hafundishwi masomo kama wale wa shule za msingi, badala yake watoto hawa hujifunza kwa vitendo, vinavyowapa msingi na kanuni mbalimbali za kuwakuza na kuwawezesha kukabiliana na maisha ya kawaida pamoja na kuwatayarisha kuanza elimu ya msingi.
Msisitizo mkubwa kwa mwalimu umewekwa katika matumizi ya mbinu shirikishi ambazo zitawawezesha watoto kushiriki katika kujadili, kuigiza kuwasiliana wao kwa wao, kufanya ziara na uchunguzi.
Mwalimu anatakiwa kubuni na kufaragua zana mbalimbali za kufundishia elimu ya awali. Aidha mwalimu bora wa elimu ya awali anatakiwa kuwa na sifa zifuatazo;
  1. Awe na mvuto wa kutosha wa kupenda kufundisha shule ya awali.
  2. Ajiamini katika kushughulika na masuala ya elimu ya awali.
  3. Aweze kujiongoza na kuwaongoza wengine kama mtaalamu wa elimu ya awali.
  4. Ajifunze zaidi na kuthamini mawazo ya watu wengine ili kuboresha na kuendeleza shule ya awali.
  5. Apende na kuhimiza ushirikiano na mawasiliano na wadau wengine wa elimu ya awali.
Maswali:
  1. Eleza maana ya Elimu ya Awali
  2. Taja malengo matano (5) ya kufundisha na kujifunza malezi ya Elimu ya Aawali kwa Mwalimu daraja A.
  3. Eleza umuhimu wa Elimu ya Awali.
  4. Nini mtazamo wa Elimu ya Awali kwa jamii ya Tanzania?
  5. Kwa nini ongezeko la shule za awali ni kubwa mno maeneo ya mjini kuliko vijijini ambako kuna ongezeko la watu wengi?
  6. Taja aina kuu mbili (2) za uchunguzi wa mtoto wa Elimu ya Awali.
  7. Kuna aina anuai za kufanya uchunguzi wa mtot. Taja njia tatu (3).
  8. Taja njia nne (4) zinazoweza kueneza magonjwa ya watoto wadogo.
  9. Nchini Tanzania, Elimu ya Awali ilianza Mwaka gani?
  10. Ainisha aina kuu mbili (2) za uchunguzi wa mtoto na kila moja eleza kwa kutumia mifano miwili miwili kwa ufafanuzi.
  11. Watoto wadogo huwa na matatizo wakati wa kula. Je, matatizo hayo husababishwa na nini?
  12. Ni ajali zipi hutokea mara kwa mara katika Shule za Awali na husababishwa na nini?
  13. Taja na kueleza vifaa vinavyopaswa kuwemo katika Kisanduku cha Huduma ya Kwanza.
  14. Nini maana ya adhabu? Eleza faida na hasara za adhabu katika tendo la kujifunza.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)