MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
NAFASI YA SANAA KATIKA ELIMU TANZANIA

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
NAFASI YA SANAA KATIKA ELIMU TANZANIA
#1
Nafasi ya Sanaa Katika Elimu Tanzania
L.A. Mbughuni
Sura ya kwanza ilijadili jinsi tunavyoweza kuunda falsafa ya Sanaa za Tanzania. Katika sura hiyo tuliona kwamba, uundaji wa sanaa hapa Tanzania, Afrika na mahali pengine pote duniani una malengo matatu muhimu ya kimsingi na ya jumuiya. Malengo hayo ni kuburudisha, kufunza maadili ya jamii au kutoa funzo maalum na kuitia jamii motisha wa kufuata na kutimiza mafunzoyenyemaadili katika maishayakilasiku.
Kwa hiyo lengo la kwanza muhimu la sura hii ni kujadili kwamba: sanaa isiyo na tumizi lolote au isiyotoa elimu au funzo lenye maadili ya jamii ya msanii, sanaa hiyo haijatimiza malengo yake mawili muhimu ya kimsingi katika uundaji wake kwani sanaa isiyonafunzo lenyemaadili ya jamii, haijakamilika, na kukomaa kisanii na msanii wa sanaa hii hajatimiza sehemu moja muhimu yawajibu wakekwajamii.
Mjadala wa kwanza wa sura hii utatumia mifano ya Sanaa za aina ya zana na zile za aina ya hisi yaani sanamu za picha za kuchora, picha za aina ya posta na vielelezo. Nia ya mjadala huu ni kufafanua jinsi sanaa itoavyo funzo au elimu wakati inapotumika katika maisha ya kila siku, mashuleni, katika vitabu, majarida, magazeti na katika matangazo ya biashara.
Lengo la pili muhimu la sura hii ni kutoa mifano maalum inayodhihirisha uhusiano mkubwa uliopo kati ya sanaa na elimu kwa kuhaklkisha kwamba, sanaa kamilifu halplngani na misingi ya asili yake au chimbuko lake. Kwa hlyo mjadala wa lengo la pili na la sura hii, nia yake ni kudhihirisha kwamba: Sanaa inayopoteza lengo na matumizi ya asili yake, sanaa hiyo hupoteza hadhl yake na hatlmaye Itafifia kisanii katika jamii yake, mpaka uundaji wa sanaa hiyo ulimbuke katika misingi na matumlzi mengine katika Jamii nylnglneau ya msanil.1
Quote:1Tangu awali sanaa ya aina va lipiku, lengo lake ni elimu na sherehe za jando baadhi ya jamu ya Makonde Jamn nyingi za Ulaya huheshimu lipiku kama sanaa bila ya kuiali matumizi yake kwa Wamakonde Na jamii mpya, huhifadhi sanaa hiyo makumbusho na kufundisha historia ya Wamakonde.
Lengo muhimu la tatu la sura hii ni kujadili na kutoa mifano michache itakayoonyesha na kudhihirisha kwamba sanaa Inaweza kutumika kikamilifu katika kufunza jamii na katika kudumisha misingi ya Taifa la Tanzania ya Elimu ya Kujitegemea, kama ilivyo elezwa na Mwalimu J.K. Nyerere, katika Elimu ya Kujitegemea (1967). Elimu ya Kujikomboa (1974), Azimlo la Arusha (1967) na sera nyingine za ChamanaSerikali.
Mjadala wa lengo la tatu na la mwisho la sura hii una nia ya kuonyesha na kuthibitisha kwamba, Sanaa muhimu ya wakati wowote, katika historia ya mapambano, baina ya jamli na mazingira yake, ni ile itumiayo usanifu wa hali ya juu katika uundaji, matumizi fulani, pamoja na kuipa jamii hamasa ya kufuata maadili ya maisha ya jamii hiyo, ili jamii iweze kufikia malengo yake katika hali zote muhimu za malsha: hamasa hiyo hutolewa kama elimu na kishawishi cha Sanaa inayohusika:
SANAA NI EUMU
Hapa Tanzania na duniani pote, elimu ni utaratibu uliokusudiwa kuongoza maarifa ili jamii ifikle malengo yake. Kwa Tanzania, malengo ya uongozl wa maarifa ni kutayarisha – jamii yenye maadili ya kljamaa na kujitegemea.
Kuna alna mbili za utaratibu wa kuongoza maarifa hapa Tanzania na duniani pote. Aina ya kwanza ni utaratibu utumikao katika shule zetu na vyuo. Alna ya pili hutumika nje ya shule na vyuo vy.etu. Lakini alna zote mbili zilikuwepo hapa Tanzania tangu zamani na aina zote mbili hivi sasa zinatambulika na kuheshimika katika taifa letu kwamba ni muhimu kwa jamii ya Tanzania katika kufikia malengo yetu ya Ujamaa na Kujitegemea.
Kwa sababu Mwalimu J.K. Nyerere (1967) alitoa maelezo kamili kuhusu madhumuni na malengo ya elimu ya kujitegemea hapa Tanzania, hatutarudia mraelezo hayo katikasura hii.
Sasa hatuna budi kuonyesha nafasi ya sanaakatika elimu kwa misingi ya maana hii na maelezo yaliyotolewa na Mwalimu J.K. Nyerere katika Elimu ya Kujitegemea, kuhusu madhumuni namalengoyaelimu hapa Tanzania, katika kujenga na kuadilisha Jamii ya Tanzania kufuatia maadili ya ujamaa na Kujitegemea.
Ikiwa maana ya elimu iliyotolewatunaikubali, basi sanaa ni elimu ikiwa sanaa zitatumika kama’utaratibu uliokusudiwakuongozamaarifa, tokakizazi hadi kizazi, ili kuwezesha jamii yoyote kufahamu’ na kufikia lengo maalum.
Kwa hapa Tanzania sanaa za mapangoni za Kondoa Irangi au sanamu ya Askari iliyoko mtaa wa Independence, Dares Salaam ni elimu kamasanaa hiyo ni utaratibu uliowekwa kwa makusudio ya kuongoza maarifa kwa watu wa Tanzania toka kizazi hadi kizazi.
Elimu ni lengo muhimu lasanaa kwasababu, moja ya asili za sanaa ni Elimu. Sanaa zote za hisi zina mawasiliano ya lengo na ujumbe maalum, lakini ni baadhi tu ya sanaa aina ambazo zina lengo na ujumbe maalum. Kwa hiyo katika uwanda wa nadharia na mantlki, tunaweza kujadili kwamba; Sanaa isiyo toa elimu au funzo fulani kwa jamii haitimizl moja ya lengo lake muhimu. Vile vile sanaa hiyo hupingana na asili yake ikiwa haitoi elimu yenye maadili. Kwa hiyo sanaa hiyo ni sanaa lakini sio sanaa kamilifu au sanifu; wala sio sanaa muhimu na ya hali ya juu kwa jamii ya msanii.
Nia yetu ni kudhihirisha kwamba iklwa kwa mfano, chakula ni sehemu muhimu ya afya na uhai wa viumbe, binadamu hula chakula ili aishi wala haishi ili ale chakula: kwa hiyo chakula kisicho muhimu kwa afya na uhai wa kiumbe slo chakula muhimu na cha hali yajuu kwa afya na maisha ya binadamu. Chakula hicho ni chakula, lakini ni cha hali ya chini. Hicho slo chakula bora.
Kwa hiyo, kwa kufuatia mfano huu huu wa chakula, afya na maisha; tunaweza kujadili kimantiki kwamba, sanaa isiyo na tumizi lolote au isiyo toa elimu au funzo lenye maadili fulani ya jamii inayohusika, sanaa hiyo siyo ya hali ya juu na wala siyo sanaa muhimu ya wakati ilipoundwa kwa jamii yake. Kwa sababu haifuati asili na lengo lake ambalo ni elimu wala haina tumizi lolote.
Kimantiki tunaweza kujadili na kuamua kwamba, kitu ambacho hupingana na misingi ya asili, iliyokifanya kitu hicho kiwe kitu, kitu hicho huonekana na hatimaye kutoweka au kugeuka kuwa kitu kingine, kama vile chakula kinavyoweza kugeuka sumu na kuhatarisha afya na maisha ya kiumbe, badala ya kuwa msingi wa afya na maisha bora ya binadamu.
Maswali muhimu, hapa yanayohitaji majibu ni haya: Asili ya Sanaa ni nini? Malengo yake ni yapi? Asili na malengd hayo yana uhusiano gani na elimu ya jamii? Kuna falsafa na nadharia tatu muhimu za asili yasanaa hapa Tanzania, Afrika na duniani pote, na zote zinasehemu inayohusishasanaa katikaelimu.
Nadharla ya falsafa ya sanaa kwanza hutambulisha sanaa kama kitu cha kuiga, klnachoundwa na binadamu wala sio wanyama, ingawaje kuna wanyama waliojipatia sifa mbalimbali kwa ajili ya utundu na ujanja wao kama vile sungura, nyani na sokwe. Nadharia ya falsafa hii Ina hoja tatu muhlmu za asili ya, Sanaa:-
Quote:(1) Kwambabinadamu ni kiumbe muigaji kwaasili na ana uwezo mkubwa wa kuiga kubunia na kutafsiri kushinda wanyama wengine wote.
Quote:(2) Kwamba binadamu tangu mwanzo wa maisha yake hujifunza kutokana na mazingira yake kwa kuiga.
Quote:(3) Kwamba binadamu hupendezewa sana na kazi za kuiga tuitazo Sanaa za hisi.
Hoja ya kwanza hujibu swali: Kwa nini binadamu anaunda Sanaa? Jibu lake ni kwamba ana uwezo mkubwa wa kuiga kwa asili na hutumia uwezo huo kwa kuunda sanaa: Sungura, Nyani na Sokwe hawana uwezo huo na ndio maana hawaundi sanaa.
Hojaya pili nayatatu hujibu swali: Sanaa inafaida gani kwa binadamu tangu akiwa mchanga hadi mwisho wa maisha yake? Jibu kwamba Sanaa ni elimu na kitambulisho cha ukuzi wa akili ya binadamu. Hojaya pili naya tatu hutoa maelezo ya kutosha kuhusu swali. Sanaa ni elimu kwa jinsi gani? Na hoja ya kwanza ambayo ndio msingi wa falsafa wa nadharia, yake huegemea sana uundaji wa Sanaa utokanao na asili ya binadamu mwenyewe. Baadhi ya sanaa hutumika hasa kwa madhumuni ya kuyatawala mazingira ya msanii kamavilesilaha.
Mjadala wa nadharia ya falsafa ya kwanza kwamba asili ya sanaa ni uwezo wa binadamu wa kuigiza mazingira yake. Na sanaa ni elimu kwa vile binadamu hujifunza njia za kutawala mazingira yake wakati anapoigiza mazingira kwa kuunda sanaa.
Mantiki ya falsafa na nadharla hii Imeegemea katika taaluma ya uundajl sanaa na jinsi binadamu alivyopata uwezo wa kuunda sanaa, akilinganishwa na wanyama wengine wenye akili kama vile Sungura, (katika methali za Afrika), Nyani na Sokwe.
Falsafa na nadharla ya pili ina mjadala mmoja muhlmu ambao pla unawelekeo wa kutoa funzo na elimu, Ingawaje mwelekeo huu hautamkwl hivyo wazi wazi. Falsafa na nadharia yake hujadili kwamba: asili ya sanaa ni mawazo na hisia za msanii kuhusu jamii na mazingira yake. Hoja na mantikl ya nadharla hil hudhlhlrlsha kwamba, msanii huhuslsha hlsla zake na mawazo yake, kuhusu jamli na mazinglrayake kwa nla ya kutoa elimu au funzo fulani kwa jamil hlyo, na kulpa hamasa jamii hiyo kutenda mambo fulani au kulshi maisha ya aina fulani, kama mambo hayo yanavyowakilishwa katika dhamira na ujumbe wa sanaa.
Mantiki na hoja za falsafa hii huegemea katika umuhimu wa dhana katika asili ya Sanaa, dhana ambayo lengo lake kubwa ni kutoa mafunzo kwajamii wakati sanaa inatoa kiburudisho kwa jamii.
Kwa kutumia sanaa kama nyenzo au zana ya kujipatia chakula na kumshambulia adui zake, kame hadi karne, binadamu alipata elimu kubwa ya kuyatawala mazingira yake aliweza kuishi maisha marefu na bora yeye na jamaa yake.
Katika mapambano haya binadamu wa asili hapa Tanzania, Afrika na mahala pengine duniani alianza kuunda zana za kujipatia chakula katika uwindaji, uvuvi, na hatimaye ukulima wakati alipojifunza kujenga mahali pa kuishi, na kufuga wanyama. Zana hizo hizo za kujipatia chakula, alizitumia kwa kuwashambulia maadui zake. Zana hizo ni kama shoka za mawe, silaha za miti, na baadaye alipendelea zaidi, mkuki na ngao, upinde na mishale.
[Image: p084.jpg]
Vielelezo vya zana na silaha za miti toka enzi ya kale Tanzania
Sanaa hizi tunaziita elimu ingawaje wakati binadamu wa mwanzo alipoziunda, bila shaka alizipamba kwa nakshi ili zipendeze, au alizipa umbo fulani ambalo ni la kupendeza ingawaje umbo hilo na nakshi hizo havikuwa na uhusiano kamili na kazi ya kumpatia chakula au kushambulia adui zake; bali jambo lililo muhimu kwa mjadala wa sehemu ni kwa kutumia sanaa kama nyenzo au zana, karne hadi karne, binadamu alipata mafunzo naelimu kubwayakutawala mazingira yake ili aweze kuishi maisha marefu nabora. Elimu hii iliporithishwa toka kizazi hadi kizazi na kukuzwa na vizazi mbali katika historia ya binadamu, imekuwa chanzo na kisa kinachoendelea cha maendeleo ya binadamu tangu kale hadi leo, kama inavyoonekana katika historia ya sanaa na ya zana za binadamu.
Sehemu hii imejadili kwamba, Sanaa ni elimu kwa vileasili mojawapo muhimu yasanaani elimu nalengo
kubwa mojawapo la sanaa ni kutoa funzo au elimu fulani kwa jamii ya msanii, na binadamu hujifunza mbinu za kutawala mazingira yake wakati akiunda sanaa za kumsaidia kuyafahamu na kuyatawala mazingirayake.
SANAA NI ZANA YA ELIMU
Tangu enzi ya ukoloni wa Kiingereza hadi leo sanaa za aina mbalimbali zimefundishwa katika mashule ya Tanzania na sanaa za aina nyingi zinatumika kama zana ya kuwakilisha ujumbe, katika mawasilianobainaya mwalimu na mwanafunzi.
Wakati wa ukoloni (1895 – 1961) na hata 1980, ni shule chache tu ambazo zimefundisha sanaa kama somo lenye uzito sawa sawa na masomo mengine kama vile hesabu na sayansi. Kati ya miaka 1895 na 1960, shule chache ambazo Waafrika walikuwa wanasoma zilifundisha somo la sanaa tangu shule za ukuzi hadi shule za sekondari na vyuo vyaelimu. Shule hizo chache ni kama vile Tabora Shule ya Sekondari, Tanga na Chuo cha Waalimu cha Butimba na Mpwapwa. Lakini wakati huohuo, mashule yote ya wanafunzi wa Kizungu na wa Kihindi, katika ngazi zote za elimu sanaa ilifundishwa kama masomo mengine, wala sio kama kiburudisho baada ya masomo kama ilivyofanyika katjka mashule mengi yaWaafrika.
Hata hivyo, umuhimu wa somo la sanaa katika ngazi mbalimbali za elimu tangu shule za ukuzi hadi Chuo Kikuu ulifahamika hapa Tanzania tangu enzi ya ukoloni hadi leo. Chuo Kikuu cha Makerere cha Uganda ambacho kilipokea wanafunzi wa Diploma ya sanaa toka Tanganyika kilifunguliwa 1940 na tdara ya Sanaa za Maonyesho ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ilifunguliwa mwaka 1967, lakini Idara ya Sanaa ilifunguliwa 1974.
Suala la sanaa na elimu ya sanaa katika Chuo Kikuu halinabudl ilchunguzwe ndani ya misingi ya Chuo Klkuu chenyewe, kwa kuchunguza suala zima la lengo, madhumuni na wajlbu wa Chuo Klkuu katika nchl Inayoendelea. Katika mljadala mingi Inayoendelea Juu ya suala hili, Mkuu wa Chuo cha Dar es Salaam, Mwalimu J.K. Nyerere, alitoa matamshi katika hotuba yake wakatl wa sherehe ya kufungua Chuo Klkuu cha Dares Salaam mwaka 1970, kuhusu wajlbu na lengo la elimu ya Chuo Klkuu kwa Jumla, ambayo yanatoa mwongozo wa kimsingi.
Mwalimu J.K. Nyerere alieleza kwamba tegemeo la jamil kwa kila taaluma ya Chuo Klkuu ni kutafltl ukweli wa kitaalamu katika kila taaluma kufuatla mslmamo unaojitambulisha na mategemeo ya jamii.
Vilevile, Mwallmu alieleza kwambawajlbu wakila taaluma ya Ohuo Klkuu ni kufunza watu wenye uwezo wa kuflkirl kulingana na mabadiliko ya jamii inayoendelea.
Lakinl, Mwalimu alionya na kusisitiza kwamba ingawaje, kila taaluma Ina uhuru wa kutafiti ukweli bila woga au upendeleo, taaluma hazitaweza kukuza elimu na kusaidla Jamli, kama matokeo ya Juhudl hiyo, hayatajali hatari yakekwajamli.
Kwa hlyo kila taaluma ya Chuo Klkuu: nla, wajibu wakutafutamaananaukweli bila yawogalaklnlwakatl huohuo, inawajibuwakutumlkiajamli.
Ingawaje Mwalimu aliyasema haya yote kuhusu kila taaluma na Idara ya Chuo Klkuu, mambo haya ndiyo msingl wa wajibu na malengo ya elimu ya sanaa na nafasi ya sanaa katika Chuo Kikuu kama inavyohusu taaluma zote nyingine.
Malengo na wajlbu huo pia umetamkwa katika katibaya Chuo Kikuu, yaani kuhifadhi elimu ya sanaa tangu kizazi kihgine hadi vingine, kufanya utaflti katika sanaa na kutafuta ukweli wa viwango vya juu katika sanaa bila woga, na kufunza wataalamu wa sanaa, katika viwango vya juu ili watimize mahitaji ya taifa ya wataalamu wa Sanaa.
Kwa maelezo zaidl, kuhusu wajibu na malengo ya sanaa na elimu ya sanaa katika Chuo Kikuu, soma hotubaya Mwallmu J.K. Nyerere, Agosti 1970, Uk. Wa 8 – 13.
Kwa hiyo nafasi ya sanaa na elimu yasanaa katika shule za sekondari, vyuo vya Waalimu na Chuo Kikuu ni kutimiza mahitaji ya taifa hili, ambayoni uundajiwa sanaa na kutoa wataalamu wa viwango mbalimbali katika taaluma ya sanaa kwa madhumuni ya kutumikia raifa la Tanzania kama mwalimu alivyoeleza katika hotuba zake mbalimbali kuhusu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na wajibu wake kwa taifa la Tanzania.
Katika viwango vya mwanzo sana vya elimu hapa Tanzania tangu wakati wa zamani hadi leo, sanaa na elimu ya sanaa ina nafasi muhimu nne:
Quote:1. Sanaa ni zana ya mawasiliano baina ya mwalimu na mwanafunzi.
2. Sanaa ni zana ya uthamini wa ukuzi wa mawazo na akili ya mtoto tangu umri wa miezi 6 hadi miaka 10.
3. Sanaa ni chombo au zana ya kuhimiza ukuzi wa mawazo na akili ya mtoto wa umri uliotajwa.
4. Sanaa ni zana ya kutambulisha ufahamu wa binadamu na matokeo ya ufahamu huo.
Nafasi ya Sanaa Katika Elimu Tanzania
Sanaa kama zana ya elimu hutumika kwa maana hiyo hiyo katika kuelimisha watu wazima ambao hawajui kusoma na kuandika, kama inavyoonekana katika vitabu vingine sana hapa Tanzania vilivyoandikwa kwa ajili ya elimu ya watu wazima tangu mwaka 1969 hadi 1981. Vitabu hivyo ni kama vile Jifunze kusoma (1968), Jiendeleze kusoma (1970), Jifunze kusoma: Kilimo Bora cha Pamba (1970) na vinginevyo.
Zaidi ya sanaa kutumlka kama kielelezo cha mwalimu, chakuwakilishia ujumbe wa elimu toka kwake au ‘kltabuni hadi kwa mwanafunzi wake, kumfunzia mtoto na mtu mzima kusoma na kuandika; elimu ya saikoiojia ya watoto sasa imethibitlsha kwamba, sanaa ni zana muhimu sana katika uthamini wa ukuzl wa fikra na akili ya mtoto. Vile vile saikolojia ya elimu ya watoto imethlbitishwa kwamba sanaa iliyochorwa na mtoto yaweza kutumika katika uchunguzl wa kuelewa maendeleo na matatizo ya mtoto anayehusika. Kwa mfano, mtoto huweza kuchora magarl au ndege kwa sababu anapenda sana ndege na magari, au mtoto anaweza kutishika sana hata akaota ndoto za jinamizi akiona picha za vitu anavyoviogopa sana. Vile vile maumbo fulani na mistari ya sanaa ya kuchora, vinatafsiri mbalimbali kwa wataalamu wa saikolojia kuhusu akili ya msanii akiwani mtoto au mtu mzima.
SANAA NA ELIMU YA JAMII
Hapa Tanzania na mahali pengi duniani, sanaa ilitumika kama zana kuelimishia jamii kuhusu mambo muhimu katika maisha yao ya kila siku kati ya mwaka 1969 na 1980, sanaa za aina ya Posta na Vielelezo zimetumika kwa faida kubwa sana kwa jamii mbali mbali za Tanzania katika kampeni mbalimbali za kitaifa, kama vile kampeni za Afya Bora, Chakula bora, uchaguzi naukulimabora.
Katika maisha ya kila siku ya jamii ya Tanzania sanaazaaina ya zana hutumika sana kuelimishajamii, mambo mbalimbali kwa njia ya sanaa za ishara. Elimu hiyo hutokana na ujumbe unaowasilishwa na sanaaya ishara kwa Jamii. Ilani ya hatari kwenye nguzo za umeme hukutahadharisha na kifo, au kukulazimu ugundue njia ya kuepuka kifo kutokana na hatari ya umeme. Ishara za barabara hutoa ujumbewenyeelimu kwa njia hiyo hiyo ingawaje ishara hizo hizo pia hutumika katika elimu au kampeni za usalama wa barabarani.
Kuna aina nyingi za zana ambazo walimu hutumia kwa madhumuni ya kufundishia katika viwango mbalimbali vya elimu; Baadhi ya zana hizo ni sinema, radio na sanaa ya aina ya vielelezo.
Matumizi ya sanaa katika kutoa funzo na elimu fulani fulani, ni tofauti na yale ya msanii ambaye huingiza funzo lake katika dhana ya sanaa wakati akiunda sanaa hiyo. Kwa hiyo jamii nupata funzo la sanaa kutokana na tafsiri ya lengo la dhana ya sanaa hiyo, yaani ujumbe wa sanaa hiyo.
Sanaa hutumika kama zana ya elimu ya kufundishia wakati Inapotumika kama zana ya kuwakilishia ujumbe, ambao ni funzo, kutoka kwa mwalimu hadi kwamwanafunzi.
Kwa njia hiyo hiyo, sanaa hutumika kama zana ya kutoleaujumbewenyefunzotokakwamtu mmojahadi kwa mtu mwingine, taifa moja kwa taifa jingine au jamii moja kwa jamii nyingine.
Katika viwango vya mwanzo sana vya elimu kwa mfano, sanaa za kuchora hutumika kama msingi na zana ya kufundishia kusoma na kuandika. Sanaa za kuchora hutumika kama vielelezo vya mambo na mawazo ambayo ingekuwa vigumu kumwelimisha mtoto mchanga kwa maneno, bila ya kumchosha, kumtatanisha akili au kuvunja nia yake ya kujifunza kusoma na kuandika. Kwa hiyo vitabu vya elimu vya kiwango hiki cha mwanzo sana cha elimu huwa na maneno machache, maelezo mafupi au majinayavitu na picha za kuchora kama vielelezo.
Kwa kutumla kielelezo cha picha ya kuchora, mwalimu wa shule ya ukuzi hufanikiwa zaidi na kwa urahisi kumweleza mtoto mdogo wa shule ya ukuzi mama na baba ni nani kwa kutumia kielelezo cha picha ya baba na ya mama. Zana hii hil huweza kutumika kumweleza mtoto mambo mengi kama wanyama ambao hajawaona au vitu ambavyo havifahamu, au anavifahamu lakini hajui majina yake.
[Image: p090.jpg]
Kinyamkera cha Wazaramo
MAADILI YA JAMII MPYA KAMA DHANA YA SANAA
Sehemu hii inayohusu maadiliyajamli mpyakama dhana za sanaa katika harakati za ujenzi wajamii mpya itajadili na kujaribu kujibu maswali matatu muhlmu:
Maadili hayo yanajitokeza vipi katika sanaa za wakati huo, (1954-1980 -)? Maadili hayo yanafahamika vipi na kueleweka vipi kwa jamii? Maadili hayo ni yapi na yanapatikanawapi?
Adili ni nini? Adili ni funzo linalohusu maisha ya jamii naimanizake; misingiya imani hiyokatikaelimu, uchumi, siasa na utamaduni; tabia, mila na desturi, malengo, madhumuni na mategemeo ya jamii kuhusu hayayote.
Lengo kubwala adili au maadili yajamii ni kujenga misingi ya imani za maisha zinazo kubaliwa na kufuatwa na jamii katika mawazo na akili za watu wa Jamii hiyo, hasa watoto navijana, ili Jamii iwezekufikia na kudumisha malengo na mategemeo yake, toka kizazi hadi kizazi.
Kwa hiyo katika sehemu hii, neno adili litakuwa na maana hii; na maadili ya jamii mpya ya Tanzania ni matokeo ya mchujo au mchekecho wa hali ya juu wa maandishi na matamshi muhimu au sera muhimu za Chama na Serikali.
Mchujo au mchekecho huo hufanywa na watu wenyewe katika ngazi zao mbalimbali za maisha ya kila siku tangu nyumbani chini ya uongozi wa baba na mama, mashuleni chini ya uongozi wa mwalimu, serikalini chini yaviongozi wake; hadi katikachamana ngazi zake mbalimbali. Matokeo ya mchekecho huo ndio mafunzo ambayo hutumika kuiadilishajamii.
“Maisha bora ni Vijijini”, kwa mfano ni adili litokanalo na mawazo ya Mwalimu J.K.Nyerere, katika Maendeleo Vijijini. “Ukulima Utu Bora” vile vile ni adili ambalo lilichekechwa kutokana na kitabu hicho hicho. Kuna mifano mingine mingi ya maadili ya ujenzi wa jamii mpya yaliyopatikana kufuatia utaratibu huu, na kutumika kama dhana au dhamira ya fani mbalimbali za sanaa hapa Tanzania tangu 1954, kama yanavyoonekana katika mifano hii michache.
Quote:Jitegemee usiwe kupe
Ubepari ni Unyama, ujam aa ni utu
Uhuru wa Bara zima la Afrika ni fukumu letu
Unyonyali kwetu ni haramu
Njia kuu za uchumi zlwe chini ya wakulima na wafanyakazi Elimu kwa wote.
Hii ni mifano michache ya maadili ambayo yalichujwa na kutumika kama dhana au dhamira ya sanaa kutokana na “Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea, “Azimio la Arusha, “Madhumuni ya TANU” Azimio la Arusha na Elimu ya Kujitegemea.
Katika jamii zetu za asili hapa Tanzania na Bara la Afrika, maadili ya maisha ya jamii hizo yalitolewa kwa njia mbalimbali, hasa kwa kutumia mithali au vigano na maadili fulani yakiwa ni dhamira kuu ya mithali au vigano, kwamfano:-
Quote:Usipoziba ufa, utajenga ukuta
Pole pole ndio mwendo
Haraka haraka, haina mbaraka
Usiposikia la mkuu yatakupata makuu.
Hapa tumeona maana ya maadili na jinsj maadili hayo yanavyopatikana na baadhi ya njia za kuya wakilisha kwa jamii.
Je, maadili ya jamii mpya ya Tanzania tangu 1954 hadi leo ni yapi na maadili hayo yanapatikana wapi?
Sehemu moja ya swali hili imekwisha jibiwa kwa ufupi sana na sehemu ya pili tutajaribu kuijibu kwa ufupi vile vile, kwa vile sera za Chama na Serikali, matamshi muhimu, maandishi ya Chama naSerikali ni mengi mno nafasi ya kuyataja na kuyajadili hayo yote haipokatikasura hii. Na hata kama nafasi yaainahiyo ingepatikana ni vigumu kuorodhesha katika kitabu kimoja maadili yote ya jamii yo yote. Kwa hiyo hapa tutatoa mifano michache tu.
Maadili ya ujenzi wajamii ya Tanzaniayanatokana na mchujo wa falsafa na mawazo yaliyomo katika maandishi ya Mwalimu J.K. Nyerere maandishi ya Chama na Serikali, mikutano semina, vikao vyaChama namatamshi yotemuhimu yaChamanaSerikali.
Machache baadhi ya maandlshi muhimu kwasura hii ni kama vile. Azimio la Arusha (1967). Ujamaa (1968). Elimu ya Kujitegemea(1967). Maendeleo Vijijini (1967), “Elimu ya Kujikomboa” (1974), Mwongozo (1971) na baadhi ya matamko muhimu ni kama lile ‘Tamko la Musoma kuhusu Elimu ya Kujitegemea”, Semina ya Kibaha, kuhusu Mwongozo, utekelezaji wa “Operesheni Vijiji vya Ujamaa” na “Operesheni Maauka”.
Moja ya sehemu yenye maadili muhimu yahusuyo’ tabia, desturi na mwenendowaviongozi wajamii mpya imo katika Azimio la Arusha.
Sehemu hiyo inaelekeza kwamba:
Quote:1. Kiongozi wa TANU (sasa CCM) au wa Serikali sharti awe mkulima au mfanyakazi, na asishiriki katikajambololotela kibepari au ukabaila.
2. Asiwe na hisa katika Makampuni yoyote.
3. Asiwe mkurugenzi katika kampuni ya kikabaila au kibepari.
4. Asiwe na mishahara miwili.
5. Asiwe na nyumba ya kupangisha.
Mfano mmoja wa adili litokanalo na sehemu hii ni kama vile, “Kiongozi wa CCM hanyonyi wala hanyonywi”. Huu ni mfano mmoja tu wa maadili mengi yanayoweza kuchujwa kutokana na sehemu hiyo na yakatumiwa kama dhana au dhamira ya fani mbali mbali zasanaa.
Je, maadili hayo yanafahamika na kueleweka vipi kwawatu waTanzania?
Baada ya miaka 10 tangu Elimu ya Kujitegemea na vitabu vingine vilivyotajwa vichapishwe hadi leo bado jamii na wasanii wa Tanzania wanajadili na kujitahidi kuyaelewa vyema ili kuyatekeleza mawazo nafalsafaza maandishi hayo, lakini utekelezaji huo haujafikia kiwango cha ufanisi kilicho tegemewa na Chama na Serikali. Sababu tatu muhimu zinazokaribiana zimetolewa kueleza hali hii mpaka sasa sehemu ya kwanza ni kwamba, hatukuielewa vyema sisi watu wa Tanzania falsafa ya siasa ya Elimu ya Kujitegemea, hasa Viongozi na Vyombo vya umma vya utekelezaji. Kama ilivyoelezwa katika Azlmlo la Baada ya Miaka Kumi.
Katika fani mbalimbali za sanaa harakati za utekelezaji wa siasa ya Elimu ya Kujitegemea zilifanyika na ushahidi huo ni mifano mingi ya sanaa zilizoundwa na zenye maadili ya siasa hii kama dhana au dhamira ya sanaa hizo.
Tatizo linalohusu kuelewa vyema, tafsiri sahihi na utekelezaji bora wa falsafa na siasa iliyotolewa katika maandishi na matamshi ya Mwalimu J.K.Nyerere Chama na Serikali, ulijitokeza katika maandishi mengine muhimu ya wakati wa ujenzi wajamii mpya, chini ya misingi ya ujamaa na kujitegemea. Kuna wasanii kwa mfano waliokuza wazo ambalo si sahihi katika sanaa zao na akili za wananchi, kwamba kila mtu mwenye tumbo kubwa ni mnyonyaji au kila mtu aliyekonda konda au aliye na umbile la kadiri sio mnyonyaji. Huu ni mfano mmoja tu wa mingi inayothibitisha kwamba hata baadhi ya wasanii walipata matatizo haya.
Kutokana na ushahidi huu wa shughuli za utekelezaji wasiasa, madhumuni, na harakati zaujenzi wa jamii mpya ya Ujamaa na Kujitegemea, ni wazi kwamba, ujuzi wa maadili ya ujenzi wa jamii mpya bado unaendelea na tahadhari kubwa inatakiwa ili tufikietafsiri ambazoni sahihi nasiasayetu.
Pili, tafsiri sawa na sahihi za siasa na falsafa za ujenzi wa Jamii mpya utategemea kuelewa vyema na kutoa tafsiri sawa na sahihi za utekelezaji wa maandishi, matamshi, na sera zote muhimu za Chama na Serikali.
Tatu, tuna hitaji kufunua akili zetu, muda na juhudi kubwa ya kuyachunguza na kuyaelewa madhumuni, imani malengo na mategemeo ya ujenzi wa jamii mpya, ili maadili tutakayo chuja au chekecha kwa madhumuni ya kuadilisha jamii mpya yawesawa na misingi ya ujamaa na kujitegemea.
Nne, ujuzi wa imani, malengo, madhumuni na mategemeo ya ujenzi wa jamii mpya unaojengwa juu ya ujuzi wa sera moja, tamshi moja, kitabu kimoja, au ibara chache zilizonakiliwa kutokana na moja ya hayo yote, huo ni ujuzi wa bandia na ujuzi wa aina hiyo ni hatari, kwa vile una uwezo mkubwa sana wa kutupotoshakatikamaadili yetu.
Ujuzi wa aina hii hautamwezesha mtu wa Tanzania au mtu ye yote kutoka nje ya Tanzania kuelewa sanaa zenye maadili yaujenzi wajamii mpya na hasa maadili yenyewe.
Maana ya sehemu hii ni kwamba, ikiwa mtu hajui historia ya vita vya Maji Maji, mtu huyo anaweza ashindwe kuelewa kwa urahisi tafsiri ya dhana na ujumbe wasanamu au pichaya vitavyaMaji Maji.
Au ikiwa mtu hajui kisa cha kusulubishwa kwa Bwana Yesu, sanaa za kusulubishwa kwa Bwana Yesu zitamuwia vigumu kwa jinsi hiyo hiyo. Na ikiwa mtu haelewi au hajui chanzo cha vitavya ukombozi dhidi ya uvamizi wa Fashisti idi Amini kwa Tanzania, sanaa zenye dhana au dhamira ya vita hivi pia zitamtatanisha kama ilivyoelezwa.
Kwa ufupi sana, sehemu hii imeeleza jinsi matatizo yanavyoweza kuzuka na aina ya matatizo yaliyokwisha zuka katika kuelewa maadili ya ujenzi wa jamii mpya na yanaweza kutokea wakati wa kuyatumia katika fani mbalimbali za sanaa, ili kuadilisha jamii ya msanii.
Je, maadili haya hujitokeza vipi katika sanaa za ujenziwajamii mpya?
Maadii hayo hujitokeza kama tafsiri ya mawazo na hisia za msanii kuhusu jamii mpya na mazingira yake.
Vile vile maadili hayo hujltokeza kama dhamlra kuu au dhana ya sanaa, baada ya msanil kupata mahamasa kutokana na kuelewa kwake imani, madhumuni, malengo na mategemeo ya ujenzi wa jamil mpya, au siasa, falsafa mawazo, na shughuli za utekelezajl wa siasa ya ujamaa na kujitegemea.
Kwa mfano, picha ya P.P. Ndembo dhana yake ni elimu ya watu wazima na lengo la picha hii ni kuwashawishi watu wazima kuelewa umuhimu wa kujua kusoma na kuandika. Picha hii vile vile imetokana na kampeni nyingi za elimu ya “watu wazima zilizoendeshwa hapa Tanzania na Wizara ya Elimu ya Taifa kati ya 1969 na 1980.
Tangu mwaka 1969 hadi 1980, Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima ikishirikiana na wizara mbalimbali za serikali. Chama, na vyombo vya utangazaji wa habarl, iliendesha kampeni nylngi sana za elimu ya watu wazima. Baadhi ya kampeni hizo ni kama vile;
“Uchaguzi ni wako (1970)”, “Wakati wa Furaha (1971)”, “Kupanga ni Kuchagua (1972)”, “Mtu ni Afya (1973),” “Chakula ni Uhai (1974),” na nyinginezo ambazo zilikuwa na marengo mbalimbali
Picha hii imefanikiwa kufikisha ujumbe wake; kwa hiyo ilikuwa picha nzuri na muhimu ya wakati huo wa kampeni zilizotajwa. Vile vile yaelekea msanii alitumia usanii wa hali yajuu katikauundaji wapichahii.
Jambo jingine ambalo ni muhimu kuhusu.plcha hii ni kwamba, msanii wa picha hii hakujishughulisha na kunakili andishi lolote muhimu, bali alitoa tafsiri yake kuhusu utekelezaji wa kampeni yaelimu kwawatu wazima. Na wasanii wengine wengi walifanya hivyo hivyo kuhusu Elimu ya Kujitegemea, Azimio la Arusha, “Ukombozi wa Afrika , Tabla za uongozi”. “Imani na madhumuni ya Chama”na mengineyo.
Tangu mwaka 1954, wasanii wengine wengi wa Tanzania wamejishughulisha na uundaji wa sanaa katika fani mbalimbali, wakitoa tafsiri ya hisia na mawazo yao juu ya shughuli za ujenzi wajamii mpya kwa madhumuni ya kustarehesha watu, kuwapa watu ‘ari na kuwaadilisha chini ya misingi ya malengo na mategemeoyajamii mpya.
[Image: p097.jpg]
Elimu ya Watu Wazima, Picha ya Kuchora: P.P. Ndembo, 1978. (Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.)
Ujumbe wake, kama vile: “Ujamaa Vijijini”, “Ujamaa”, “Umoja ni Nguvu”, “Watu wanalima Shambani”, “Elimu ya Watu Wazima”, “Vita vya Ukombozi wa Afrika”, “Wake wa Wagombea Uhuru”, “Kijiji cha Ujamaa”, Sanamu na picha nyingi za Mwalimu J.K. Nyerere, viongozi wengine wa Chama na Serikali, badala ya picha za Malkia au Magavana wa Kiingereza kama ilivyokuwa kabla ya 1954. Mifano micheche ya sanaa za wakati huu ni kama vile:
Quote:1. Seif Salimu: Mwalimu J.K. Nyerere na Rals S. Machel, (1977) Mozambikiy/Tanzania Instituteof Foreign Relations, Dares Salaam.
2. Pejume Alale: “Umoja ni Nguvu”, sanamu ya mpingo, (1976), Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
3. E. Jengo: “Wanamuziki” (1969), Kalenda ya Baraza la Taifa la Sanaa.
4. E. Tunginie: “Maji Safi kwa Wote” (1969), Kalenda ya Baraza la Sanaa la Taifa.
5. S. J. Ntiro: “Mnara wa Azimio la Arusha” (1974), Acusha.
6. E Jengo: “Mnara wa Tabora” (1974), Tabora.
7. J. G. Somola “Mnara wa Iringa” (1977), Iringa, Toka Maisha ya ubinafsi kuelekea kwenye Maisha ya kijamaa.
Kwa wakati huu wote inaelekea sanaa ziliundwa kwa madhumuni muhimu matatu, sanaa zilitumika kama utaratibu wa kufundishia au kama zana ya elimu. Pili sanaa ziliundwa kama tafsiri ya hisia na mawazo msaniiyanayostareheshawakati jamii inaadilishwa. Na tatu, sanaa ilitumika kama adilisho lenye kutia hamasa na ari ya kufikia malengo na mategemeo ya ujamaa na kujitegemea. Katika Chuo cha Elimu cha Butimba, Mwanza na Kigurunyembe, Morogoro, sanaa zilitumika kufundishia historia fupi ya mapambano muhimu na marefu yanayoendelea ya ujenzi wa jamii mpya; hasa katikakuelezea historia yaukombozi wa Tanganyikana mchango wa Mwalimu J.K. Nyerere, kama shujaa mkubwa, baadhi ya mashujaa wengi waliojihusisha na mapambano haya.
Katika elimu ya watu wazima, mashuleni na vyuoni, sanaa za aina ya hisi na zana zilitumika kama zana ya kufundishia elimu ya siasa na maadili ya jamii mpyayaujamaanakujitegemea.
Katika gazeti la kila siku la Kiswahili la Uhuru na Mzalendo kuna sehemu ya picha za makaragosi zilizotoa maadili kwa kutumia wahusika waitwao, “Bwanyenye”, “Polo” na “Chakubanga.”
Nyingi ya baadhi ya picha za mhusika “Chakubanga” na “Bwanyenye” zimetoa maadili mbalimbali ya kuijenga na kusifu siasa ya ujamaa na kujitegemea kwa kukanusha au kupinga destuh na tabiaza “unyonyaji” “uzururaji”, “ombaomba”, wizi na mengineyo.
Mpaka sasa picha nyingi za “Chakubanga” zinatoa mafunzo au maadili ya kujenga ari ya kupinga tabiaza unypnyaji katika maisha ya kilasiku yajamii na kujenga ari ya kujitegemea. Kwa kutumia wahusika hawa maadili mengi yamekwisha tolewa kwa jamii chini ya dhamira kama vile: “Jitegemee Usiwe Kupe”, “Usafiri wa Mazingira”, “Kilimo cha Kufa na Kupona”, “Tuhamie Vijijini”, uigaji mbaya wa mila na desturi za Kigeni nakugusia matatizoya kila siku yajamii.
Chanzo>>>>>>
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)