MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
KWA VIPI FASIHI NI SANAA?

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
KWA VIPI FASIHI NI SANAA?
#1
Sanaa ni uzuri unaojitokeza katika umbo lililosanifiwa ambapo mtu hulitumia umbo hilo kueleza yale anayotaka wengine wayafahamu.
i. Matumizi ya mtindo katika kufikisha ujumbe. Mtindo humtofautisha mwanafasihi mmoja na mwingine. Kila mwanafasihi ana mtindo wake. Ufundi unakuja pale ambapo ufundi hutumika katika mtindo ambapo mambo kama, matumizi ya barua, dayolojia, monolojia na matumizi ya nafsi hujumuishwa.
ii. Matumizi ya muundo. Jinsi ambavyo visa hupangiliwa kwa ufundi mkubwa ili kuwezesha kuifikisha kazi ya fasihi kwa walengwa, ndiyo sanaa yenyewe. Maana yake ni kwamba, mwandishi hutumia ubunifu katika kupangilia visa na matukio.
iii. Matumizi ya lugha. Lugha itumikayo katika fasihi ni tofauti na lugha nyingine. Katika lugha ya fasihi kuna matumizi ya tamathali za semi, misemo, nahau na ujenzi wa picha na taswira. Haya yote yanaifanya fasihi iwe sanaa.
iv. Matumizi ya wahusika. Si kutumia wahusika pekee, bali ule uchaguzi mzuri wa wahusika huifanya fasihi iwe sanaa. Mwanafasihi anauwezo wa kuamua anataka wahusika wa aina gani katika kazi yake. Ana uwezo wa kumwacha hai mhusika mpaka mwisho wa kazi yake. Pia, ana uwezo wa kuyakatisha maisha ya mhusika yeyote.
v.  Matumizi ya mandhari. Jinsi mwandishi anavyojenga mandhari yake kwa ubunifu ndiyo huifanya fasihi ikawa sanaa. Kadiri mandhari inavyojengwa na mwandishi ndivyo inavyosaidia kuijenga kazi ya fasihi na kuifanya ieleweke zaidi kwa wasomaji.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)