04-20-2022, 02:01 PM
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'AMANI'
Neno amani katika lugha ya Kiswahili ni Nomino [Ngeli: i-/zi-] yenye maana zifuatazo:
1. Hali ya kuwapo utulivu dhidi ya usumbufu
2. Hali ya kuwa na usalama na utulivu; kutokuwa na vita au vurugu (machafuko) yoyote.
3. Makubaliano ya usalama baina ya nchi zenye vita.
Katika lugha ya Kiarabu neno amani linatokana na neno la Kiarabu amaanun (soma: amaanun/amaanan/amaanin أمان) lenye maana zifuatazo:
1. Kusalimika; usalama; jina linalotokana na Kitenzi cha Kiarabu amina امن amesalimika.
2. Hali ya kuwapo utulivu.
3. Ahadi; makubaliano baina ya watu wawili au watu wengi.
4. Ulinzi.
5. Ukweli; kutokuwapo udanganyifu au dhulma.
Kinachodhihiri ni kuwa neno amaanun امان lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno amani maana yake katika lugha ya asili - Kiarabu inayohusu usalama na utulivu haikubadilika na maana ya makubaliano baina ya nchi zenye vita iliongezwa.
Shukran sana.
Khamis S.M. Mataka.
Neno amani katika lugha ya Kiswahili ni Nomino [Ngeli: i-/zi-] yenye maana zifuatazo:
1. Hali ya kuwapo utulivu dhidi ya usumbufu
2. Hali ya kuwa na usalama na utulivu; kutokuwa na vita au vurugu (machafuko) yoyote.
3. Makubaliano ya usalama baina ya nchi zenye vita.
Katika lugha ya Kiarabu neno amani linatokana na neno la Kiarabu amaanun (soma: amaanun/amaanan/amaanin أمان) lenye maana zifuatazo:
1. Kusalimika; usalama; jina linalotokana na Kitenzi cha Kiarabu amina امن amesalimika.
2. Hali ya kuwapo utulivu.
3. Ahadi; makubaliano baina ya watu wawili au watu wengi.
4. Ulinzi.
5. Ukweli; kutokuwapo udanganyifu au dhulma.
Kinachodhihiri ni kuwa neno amaanun امان lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno amani maana yake katika lugha ya asili - Kiarabu inayohusu usalama na utulivu haikubadilika na maana ya makubaliano baina ya nchi zenye vita iliongezwa.
Shukran sana.
Khamis S.M. Mataka.
Mwl Maeda