04-13-2022, 05:54 AM
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'MSHAHARA'
Neno *mshahara* katika lugha ya Kiswahili ni *Nomino [Ngeli: u-/i-, wingi: mishahara]* yenye maana zifuatazo:
1. Malipo ya mwezi anayopewa mwajiriwa kwa kazi aliyofanya.
2. Ujira anaolipwa mtu na mwajiri wake kila baada ya kipindi fulani kwa kazi aliyotumikia.
Katika lugha ya Kiarabu neno *mshahara* linatokana na neno la Kiarabu *shahru (soma: shahrun/shahran/shahrin شهر)* lenye maana zifuatazo:
1. Mwezi, sehemu moja ya sehemu kumi na mbili za Kalenda ya mwaka unaozingatia mzunguko wa Mwezi *As-Sanatul Qamariyyatu السنة القمرية* au mwaka unaozingatia mzunguko wa Jua *As-Sanatush Shamsiyyatu السنة الشمسية*.
2. Mwezi Mwandamo.
3. Ulimwengu.
Kinachodhihiri ni kuwa neno *shahrun شهر* lilipoingia katika Kiswahili lilitamkwa *shahara* kisha likaingia katika ngeli ya *m-/mi* - na kupatikana neno *mshahara* lililochukua maana mpya ya *ujira anaolipwa mtu na mwajiriwa wake kwa kazi aliyoifanya katika kipindi maalumu.*
*TANBIHI* :
Maneno ya Kiarabu yenye maana ya ujira anaolipwa mtu na mwajiri wake mwishoni mwa mwezi ni *raatibun shahriyyun راتب شهري* mshahara wa mwezi au *badalun shahriyyun بدل شهري* posho ya mwezi.
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*
Neno *mshahara* katika lugha ya Kiswahili ni *Nomino [Ngeli: u-/i-, wingi: mishahara]* yenye maana zifuatazo:
1. Malipo ya mwezi anayopewa mwajiriwa kwa kazi aliyofanya.
2. Ujira anaolipwa mtu na mwajiri wake kila baada ya kipindi fulani kwa kazi aliyotumikia.
Katika lugha ya Kiarabu neno *mshahara* linatokana na neno la Kiarabu *shahru (soma: shahrun/shahran/shahrin شهر)* lenye maana zifuatazo:
1. Mwezi, sehemu moja ya sehemu kumi na mbili za Kalenda ya mwaka unaozingatia mzunguko wa Mwezi *As-Sanatul Qamariyyatu السنة القمرية* au mwaka unaozingatia mzunguko wa Jua *As-Sanatush Shamsiyyatu السنة الشمسية*.
2. Mwezi Mwandamo.
3. Ulimwengu.
Kinachodhihiri ni kuwa neno *shahrun شهر* lilipoingia katika Kiswahili lilitamkwa *shahara* kisha likaingia katika ngeli ya *m-/mi* - na kupatikana neno *mshahara* lililochukua maana mpya ya *ujira anaolipwa mtu na mwajiriwa wake kwa kazi aliyoifanya katika kipindi maalumu.*
*TANBIHI* :
Maneno ya Kiarabu yenye maana ya ujira anaolipwa mtu na mwajiri wake mwishoni mwa mwezi ni *raatibun shahriyyun راتب شهري* mshahara wa mwezi au *badalun shahriyyun بدل شهري* posho ya mwezi.
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*
Mwl Maeda