MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SHAIRI : RAIS ANAYEFAA KWA MUNGU ATATOKEA

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SHAIRI : RAIS ANAYEFAA KWA MUNGU ATATOKEA
#1

  1. Kampeni zimeanza, uchaguzi wasogea
    Ilani wanatangaza, kuwanadi wagombea
    Swali la kujiuliza, nani anayetufaa?
    Rais anayefaa, kwa Mungu atatokea.

  2. Wengi wamejitokeza, ikulu kugombania
    Mazuri wayatangaza, tupate kuwachagua
    Kama ukiwachunguza, ni vigumu kuamua
    Raisanayefaa, kwaMunguatatokea

  3. Chama gani kinaweza, kuivusha Tanzania?
    Kero zetu kumaliza, watu waache kulia?
    Rushwa kuitokomeza, ufisadi kufukia
    Rais anayefaa, kwa Mungu atatokea

  4. Sifa za anayeweza, kuwa Rais sawia
    Ni amchaye Muweza, Muumbaji wa dunia
    Mwenye kujinyenyekeza, watu kuwatumikia
    Rais anayefaa, kwa Munguatatokea

  5. Asiyekwenda kuuza, mali za Watanzania
    Wala kujipendekeza, kwa wanaotuibiaMwenye sifa ya kuweza, maovu kuyakemeaRais anayefaa, kwa Mungu atatokea
  6. Asiyejitanguliza, kwake kujipakulia
    Awezae kufukuza, wanaotuharibia
    Mwenye kuitekeleza, katiba ya Tanzania
    Raisanayefaa, kwa Mungu atatokea

  7. Yule asiyewabeza, fukara kuwabagua
    Aweza kuwatangaza, mali wanotuibia
    Vijana nao ajuza, aweze kuwatetea
    Rais anayefaa, kwa Mungu atatokea

  8. Awezae kuzitunza, mali zote zaraia
    Wageni wanowekeza, wazingatie sheria
    Aweze kuwahimiza, kodi zetu kulipia
    Rais anayefaa, kwa Mungu atatokea

  9. Kilimo kiwe cha kwanza, njuga akikivalia
    Viwanda wamedumaza, yeye ajekufufua
    Ajira kuzitokeza, uchumi kuufufua
    Rais anayefaa, kwa Mungu atatokea

  10. Utalii kuukuza, kipato kuongezea
    Ufanisi kuukaza, huduma za jumuia
    Ukali kuongeza, uzembe ujepotea
    Rais anayefaa, kwa Mungu atatokea

  11. Kila ninakoangaza, simjui anofaa
    Mola peke anaweza, kutupatia Kifaa
    Maombi tukiongeza, Yeye atatusikia
    Rais anayefaa, kwa Mungu atatokea

  12. Yeye atakayeweza, usukani kuchukua
    Pasi kutudidimiza, ni vigumu kumjua
    Mungu kumtanguliza, ndio njia nawambia
    Rais anayefaa, kwa Mungu atatokea

  13. Wengi wamejitokeza, wakidai wanania
    Ya machungu kumaliza, ikulu wakiingia
    Kumbe myoyoni wawaza, faida kujipatia
    Rais anayefaa, kwa Mungu atatokea

  14. Wagombea nakataza, mziepuke ghasia
    Yaache yenye kukwaza, kote mtakotembea
    Sera zenu kueleza, pasi kuleta udhia
    Rais anayefaa, kwa Mungu atatokea

  15. Ninarudia kukaza, jibu la Watanzania
    Maombi jambo la kwanza, Mola asikie dua
    Mmoja kumchomoza, hata kama wajemia
    Rais anayefaa, kwa Mungu atatokea

  16. Shairi nalikatiza, hapa sitaendelea
    Maneno niloeleza, nibudi kuzingatia
    Mungu uliye Muweza, ibariki Tanzania
    Rais anayefaa, kwa Mungu atatokea

  1. Rodgers Namwenje0764 222244
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)