MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
UTENZI : 'TIKADI YA UJAMAA'

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
UTENZI : 'TIKADI YA UJAMAA'
#1
‘TIKADI YA UJAMAA.
************************
‘Tikadi ya Ujamaa,
wengi hawakuelewa,
si ya Wachina jamaa,
si ya Warusi jamaa,
siasa ya Ujamaa,
ya Wafirika jamaa.

*******
N’jaribu kuelewesha,
Ujamaa kumaanisha,
ni mfumo wa maisha,
vema uliowezesha,
ya babu zetu maisha,
haswa kuyaneemesha.

*******
Wa binadamu usawa,
msingi wa ujamaa,
kazi kwa kila mjamaa,
na mapato ya wajamaa,
kugawana kwa usawa,
ni misingi ya ujamaa.

*******
Misingi ye nainena,
haswa kuthaminiana,
maana’ke kupendana,
pia kuheshimiana,
na walikaribiana,
tena kushirikiana.

*******
Mjamaa alikuwa,
ni haki kuthaminiwa,
ana haki ya kupendwa,
na tena kuheshimiwa,
alipaswa kuelewa,
ya jamii kushirikishwa.

*******
Ilikuwa mila yetu,
ni desituri ya kwetu,
kumjali jamaa yetu,
mtu ‘kiugua kwetu,
huyo ni mgonjwa wetu,
anauguzwa kiutu.

*******
Kama mzazi ‘lizaa,
alituzwa na jamaa,
arusi ikitokeaa,
inafanywa kijamaa,
mjamaa ‘kilemaa,
alitunzwa na jamaa.

*******
Huko kuthaminiana,
jamaa wakipendana,
pia kuheshimiana,
mema walifanyiana,
huku wakishirikiana,
Wajamaa kufaana.

*******
Na pale mifarakano,
i’pokuwa jamii ino,
ulifanywa mkutano,
na hata makongamano,
ya kuleta mapatano,
sawa kwa ushirikiano.

*******
Hini ya Ujamaa mi’ko
uongo na rushwa mwiko,
umimi ‘likuwa mwiko,
sisi kwa sisi ni mwiko,
uvivu wizi ni mwiko,
utengano uli mwiko.

*******
Jama ninakumbukia,
jamaa wa’vyochangia,
mambo yote ya jamia,
kwa pamwe ninawambia,
ya shari walichangia,
na shwari kufurahia.

*******
Jamii ya Wanyarwanda,
Ujamaa tuliutenda,
Wasukuma na Waganda,
Wakikuyu na Wamanda,
jamii zote zilipenda,
Ujamaa kuulinda.

*******
Na siwezi kuyamala,
ya Ujamaa yetu mila,
marefu si masihala,
ja ‘lufu lela ulela,
Wazungu kututawala,
yetu waliyakatala.

*******
Waliyakatala yetu,
wakaosha bongo zetu,
eti ya kishenzi yetu,
tukawacha mila zetu,
na Ujamaa wa kwetu,
Mkoloni hana utu.

******
(Tungo litaendelea…)
Rwaka rwa Kagarama,
Mshairi Mnyarwanda.

Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)