MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
Majina ya ukoo/ familia katika lugha ya kiswahili

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
Majina ya ukoo/ familia katika lugha ya kiswahili
#1
Haya ni majina ya heshima yanayotumiwa na watu mbalimbali katika familia 
kulingana na uhusiano wao. Pia huitwa msamiati wa nasaba/jamaa/jamii
Familia Ndogo
Lengo letu ni kufundisha na kuendeleza lugha ya kiswahili kama kitambulisho cha jamii.
Hii ni familia ya karibu ambayo huhusisha tu wazazi na watoto wao. 
1. baba : ( father ) 
ni mzazi wa kiume. 
2. mama : ( mother ) 
mama ni mzazi wa kike. 
3. mwana : ( child ) 
mtoto wako 
4. mzazi : ( parent ) 
mtu aliyekuzaa 
5. ndugu : ( sibling ) 
mtoto wa mzazi/wazazi wako. Mara nyingi ’ndugu’ hutumika kurejelea watoto waliozaliwa baada yako, au watoto wa kiume waliozaliwa na wazazi wako. 
6. kaka : ( brother ) 
mvulana aliyezaliwa na mzazi/wazazi wako. Aghalabu kaka hurejelea mvulana aliyekutangulia kuzaliwa. 
7. dada : ( sister ) 
msichana aliyezaliwa na mzazi/wazazi wako. Aghalabu dada hutumika kurejelea wasichana waliokutangulia kuzaliwa. 
8. bin : ( son, mwana ) 
mtoto wa kiume
9. binti : ( daughter ) 
mtoto wa kike. 
10. kifungua mimba : ( first born ) 
mtoto wa kwanza kuzaliwa 
11. kitinda mimba : ( last born ) 
mtoto wa mwisho kuzaliwa 
12. mapacha : ( twins ) 
watoto wawili waliozaliwa siku moja na mama mmoja 
13. mke : ( bibi, wife ) 
mwanamke mliyefunga ndoa pamoja kuanzisha familia. 
14. mume : ( husband ) 
mwanamume mliyefunga ndoa pamoja ili kuanzisha familia. 
15. baba wa kambo  : ( stepfather ) 
mwanaume aliyeoa mamako, na ambaye si baba yako wa damu 
16. mama wa kambo : ( stepmother ) 
mwanamke aliyeolewa na babako, na ambaye si mama yako wa damu
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)