MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
UHUSIANO WA KIJAMII – JINSI TUNAVYOITANA

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
UHUSIANO WA KIJAMII – JINSI TUNAVYOITANA
#1
Nasaba

Nasaba ni uhusiano wa kizazi baina ya watu. Uhusiano huu unaweza kuwa katika familia au ukoo mmoja.

Mchoro: Uhusiano wa Kijamii
[Image: jamii.PNG]


Majina ya nasaba
1. Mama/nina: Mzazi wa kike.
2. Baba: Mzazi wa kiume.
3. Kaka: Ndugu wa kiume.
4. Dada: Ndugu wa kike.
5. Nyanya/Bibi: Mama wa baba au mama.
6. Babu: Baba wa mama au baba.
7. Mjukuu: Mtoto wa mwana.
8. Kitukuu: Mwana wa mjukuu.
9. Kilembwe: Mwana wa kitukuu.
10. Kilembwekeza/kining’ina: Mwana wa kilembwe.



Majina ya nasaba
11. Ami/amu: Kaka wa baba.
12. Shangazi/miomba amati: Dada wa baba.
13. Mjomba/hau: Kaka wa mama.
14. Halati/hale: Dada wa mama.
15. Mkazahau: Mke wa mjomba.
16. Mkazamwana: Mke wa mwana.
17. Mavyaa: Mama wa mume.
18. Bavyaa: Baba wa mume.
19. Mamamkwe: Mama wa mke.
20. Babamkwe: Baba wa mke.

Majina ya nasaba
21. Mcheja: Mzazi wa mke au mume (mkwe).
22. Kivyere : Jina wazazi wa mume na wazazi wa mke hutumia kuitana.
23. Mpwa: Mtoto wa ndugu. Yaani unayemwita ami, shangazi, mjomba na halati naye atakuita mpwa.
24. Mkoi: Mtoto wa shangazi, mjomba, halati.
25. Binamu: Mwana wa kiume wa ami.
26. Bintiamu: Mwana wa kike wa ami.
27. Shemeji: Ndugu wa mke au ndugu wa mume.
28. Mama wa kambo: Mama asiyekuzaa lakini anakulea.
29. Baba wa kambo: Baba asiyekuzaa
30. Umbu: Jina waitanalo kaka na dada.
31. Ndugu mlungizi: Ndugu anayekufuata


Majina ya nasaba
32. Ndugu mlungizi: Ndugu anayekufuata nyuma.
33. Wifi: (a) Mke wa kaka. Iwapo wewe ni msichana, mke wa kaka yako utamwita wifi. (b) Dada wa mume: Iwapo msichana ameolewa dada wa mumewe atamwita wifi.
34. Mwamu/mlamu: a) Kaka wa mke. Mwanamume akioa, kaka wa mkewe atamwita mlamu. b) Mume wa dada: mvulana au mwanamume atamwita mume wa dadaye – mlamu.
35. Mwanyumba: Wanaume waliooa katika familia moja.
36. Mkemwenza/mitara: Jina wanalotumia wanawake walioolewa na mwanamume mmoja.
37. Kifungamimba/ kitindamimba/ mzuwanda: Mtoto wa mwisho kuzali- wa katika familia.
38. Mwanambee/kifunguamimba/kichinjamimba: Mtoto wa kwanza kuzaliwa katika familia.
39. Nyanyamkuu: Mama wa nyanya.
40. Babamkuu: Baba wa babu.
41. Maharimu: Mtu usiyeweza kumwoa au kuolewa naye kwa sababu ya uhusiano wa nasaba.
42. Mnuna: Ndugu anayenifuata ndugu mdogo.



Zoezi A: Soma aya ifuatayo kisha ujibu maswali yatakayofuatia.
Pendo ni bintiye Fatuma na Hamisi. Pendo anao dada wawili: Subira na Baraka. Aidha, anaye kaka mmoja aitwaye Majaliwa. Pendo ameolewa na mwanamume aitwaye Rono. Wavyele wake Rono ni Kiprono na Nekesa. Rono anaye dada aitwaye Silvia na kaka aitwaye Musa. Rono na Pendo wamefanikiwa na mtoto aitwaye Eliza.


Jibu maswali yafuatayo:
1. Pendo na Silvia wataitanaje?
2. Eliza atamwitaje Fatuma?
3. Nekesa atamwitaje Fatuma?
4. Kiprono atamwitaje Eliza?
5. Subira atamwitaje Eliza?
6. Musa atamwitaje Pendo?
7. Pendo atamwitaje Kiprono na Nekesa?
8. Rono atamwitaje Fatuma na Hamisi?
9. Eliza atawaitaje kila mmoja wa hawa? a) Silvia b) Musa c) Majaliwa d) Baraka
10. Fatuma na Hamisi wataitanaje na Kiprono na Nekesa?
11. Rono na Majaliwa wataitanaje?
12. Iwapo Subira ana mtoto, Eliza atamwitaje mtoto huyo wa Subira?


B. Jaza mapengo yaliyoachwa
1. Dadaye mjomba ni mama au
2. Mzazi wa kitukuu ni _________
3. Mzazi wa mkoi ni ________________
4. Babu au nyanya wa kilembwekeza ni ___________
5. Mke wa mwana ni ____________



Zoezi C. Jibu maswali yafuatayo
1. Musa na Fatuma ni ndugu. Fatuma ana mtoto aitiwaye Rosa. Je, Rosa atamwitaje Musa?
2. Karembo na Kazuri ni dada wa toka nitoke. Karembo ameolewa na Vumilia naye Kazuri ameolewa na Stahamala. Je, Vumilia na Stahamala wataitanaje?
3. Tumaini na Neema ni ndugu wa toka nitoke. Nyanya yao anaitwa Baraka. Je, Tumaini na Neema wataitwaje na Baraka?
4. Meho amemwoa Susi. Mamaye Meho anaitwa Pendo. Pendo atamwitaje Susi?
5. Kali anaye dada aitwaye Mpole. Mpole ameolewa na Tarajio. Tarajio na Kali wataitanaje?
6. Kakaye mama huitwaje?
7. Ndugu wa kike wa mama huitwaje?
8. Kaka yake mama anaitwa Bora. Ana mke aitwaye Tuishi. Je, nitamwitaje Tuishi?
9. Pale na Hapo ni ndugu. Hapo ana mtoto aitwaye Leo. Pale atamwitaje Leo?
10. Mjukuu wa kitukuu ni nani?
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 2 Guest(s)