MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
OSW 123/133: FASIHI YA KISWAHILI NADHARIA NA UHAKIKI

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
OSW 123/133: FASIHI YA KISWAHILI NADHARIA NA UHAKIKI
#1
SWALI:  “Sauti ya kilio cha kichanga ni ishara hisia, siyo zake tu bali za mama, yaya na jamii nzima.” Je, dhana ya chanzo au isimu ya fasihi kutokana na kazi imekuja kujaje?
JIBU
Sauti ya kilio cha kichanga ni mfano halisi wasauti anayoitoa msanii na mtunzi wa kazi ya fasihi. Sauti hiyo ya msanii wa kazi ya fasihi huwa imebeba hisia zilizosheheni moyo wa mtunzi iwe zinamgusa yeye moja kwa moja au zinaigusa jamii yake. Kwa hiyo mtunzi yeyote wa fasihi huwa kama kipaza sauti cha jamii na kupitia yeye matatizo mbalimbali ya jamii yake huweza kusikika na kuvuma mbali na hatimaye kupatiwa ufumbuzi. Miongoni mwa masuala yanayopigiwa kelele na wasanii ni pamoja na:
Uzalendo, suala hili limekuwa likijadiliwa kwa muda mrefu na wasanii mbalimbali kwa lengo la kuhamasisha wanajamii kupenda nchi zao na hata kuwa tayari kutoa uhai mfano: Zawadi ya Ushindi, Kusadikika na Mtu ni Utu ni miongoni mwa kazi za fasihi ambazo watunzi wake wamekuwa wakipiga kelele kuhusu suala la uzalendo.
Maradhi, ujingana umaskini- haya nayo ni masuala yanayochochea watunzi wa kazi za fasihi kupaza sauti zenye hisia kali kama ishara ya mapambano dhidi ya maadui hao kwa mfano: Ngoswe – Penzi Kitovu cha Uzembe, Hawala ya Fedha na Kilio Chetu ni miongoni mwa fasihi zinazopaza sauti ili jamii isikie na kuchukua hatua stahiki katika mapambano hayo.
Dhuluma na uonevu, nayo ni masuala yanayopigiwa kelele kwa lengo la kuleta jamii yenye usawa katika Nyanja zote na isiyo na migogoro mfano: Vuta N’kuvute, Pesa zako Zinanuka, Tende Hogo na Kwenye Ukingo wa Thim pamoja na diwani ya Wasakatonge. Watunzi wa kazi hizo pamoja na mambo mengine wanakemea kwa nguvu zote dhuluma na uonevu unaofanywa kwa jamii hasa ya watu wanyonge kwa sababu matokeo yake mara nyingi huwa ni migogro ya kijamii na mivutano isiyokwisha.
Masuala ya mapenzi na athari zake katika jamii yameshughulikiwa na watunzi wa kazi za fasihi kwa kiasi kikubwa kwa sababu yanabeba hisia zisizojali umri wala uwezo wa mtu kielimu na kiuchumi. Kwa mfano; katika riwaya ya Mfadhili pamoja na riwaya ya Hiba ya Wivu tunaona nguvu ya mapenzi na matokeo yake katika jamii ili kuipa hadhari jamii kwenda kwa makini au kujiepusha kabisa na masuala ya mapenzi ili kukwepa madhara yake.
 
Kwa maelezo hayo ni dhahiri isiyopingika kuwa chanzo cha fasihi ni msukumo wa hisia alizonazo mtunzi wa kazi ya fasihi iwe ni hisia zake binafsi au hisia za jamii yake na wala sio kama wanavyodai baadhi ya watu.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)