MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
OSW 123/133: FASIHI YA KISWAHILI NADHARIA NA UHAKIKI

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
OSW 123/133: FASIHI YA KISWAHILI NADHARIA NA UHAKIKI
#1
SWALI: 3 Andika kumhusu mwalimu maarufu wa uhakiki wa kazi za fasihi nchini Tanzania.
JIBU
Uhakiki wa kazi za
fasihi ni taaluma ambayo nchini Tanzania muasisi wake ni mwalimu wa walimu,
gwiji wa uhakiki almaarufu T.S.Y Sengo. Umaarufu wa mwalimu huyu upo katika
kufundisha wahakiki wengi lakini pia katika kuweka misingi ya nadhariya za
kuhakikia kazi za fasihi.
Uhakiki uliofanywa
katika HISI ZETU unatoa mwanga katika kazi ya uhakiki licha ya baadhi ya
wanafunzi wake kutaka kuleta hadithi za sikio kupita kichwa kwa kumkosoa
mwalimu mkongwe kuwa amekosea kuzungumzia hisi badala ya hisiya ingawa
hawakufua dafu.
Umaarufu wa mwalimu wa
uhakiki unajidhihirisha pia katika kitabu chake cha SENGO NA FASIHI ZA KINCHI
ambamo anatoa nadhariya za kumuongoza mhakiki yeyote wa kazi ya fasihi ili
kuifanya kazi ya uhakiki kuwa taaluma yenye misingi thabiti halikadhalika
anaonesha maana halisi ya uhakiki kwa kuchambua diwani ya Wasakatonge
iliyoandikwa na M.S. Khatib kwa kukosoa pale alipokosea katika utunzi na
kukiuka nadharia za utunzi kama vile hadhira ya uhalisia pamoja na ile ya
Kiislamu.
Mwalimu Sengo pia ni
maarufu katika utunzi na umaarufu huo unajidhihirisha katika diwani yake ya
TUNGIZI ZA MNYAGATWA ambapo amesheheni mashairi yenye kufikirisha, lugha nzito
yenye kuthibitisha hasa uwezo mkubwa alionao katika kuimudu lugha.
 
Kwa ujumla mwalimu
Sengo ni mtaalamu mbobezi wa taaluma ya uhakiki wa kazi ya fasihi ambaye
mchango wake haupaswi kupuuzwa wala kuchukuliwa kirahisi na mtu yeyote.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)