MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
TOFAUTI KATI YA TENZI NA MASHAIRI

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
TOFAUTI KATI YA TENZI NA MASHAIRI
#1
Tenzi na mashairi hutofautiana hasa katika vipengele muhimu vifuatavyo: –

1. MUUNDO
Tenzi hutumia muundo wa tarbia katika beti zake ambapo mashairi yanauhuru wa kutumia miundo mingine tofauti kama vile tathilitha, takhmisa.


2. UREFU
Tenzi kwa kawaida ni ndefu kwa vile hutoka zikiwa katika mtindo wa usimulizi na hivyo kuwa na beti nyingi sana ili kukamilisha usimulizi wa kisa ambapo mashairi kwa kawaida hutumia beti chache.


3. VINA
Tenzi zina vina vya mwisho tu, hazina vina vya kati ambapo mashairi yana vina vya kati na vya mwisho.


4. UREFU WA MSTARI
Tenzi mistari yake ni mifupi, haigawanyiki katika nusu ya kwanza na ya pili. Mashairi mistari yake ni mirefu na hugawanyika mara mbili, nusu ya kwanza na nusu ya pili huitwa vipande.


5. IDADI YA MIZANI
Tenzi katika mistari yake huwa na mizani isiyozidi kumi na mbili, mashairi huwa na mizani 16 katika mistari yake.


6. KITUO
Kituo cha utenzi hubadilikabadilika kutoka ubeti mmoja hadi mwingine, kituo cha shairi kinaweza kubadilika au kutobadilika.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)