MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
OSW 123/133: FASIHI YA KISWAHILI NADHARIA NA UHAKIKI

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
OSW 123/133: FASIHI YA KISWAHILI NADHARIA NA UHAKIKI
#1
SWALI:  Jadili tofauti ya fasihi ya Kiswahili (ya Wapwani) na fasihi kwa lugha ya Kiswahili (ya jamii zote nje ya mwambao wa Afrika Mashariki)
JIBU
Fasihi ya Kiswahili ya wapwanini ile iliyoandaliwa na mswahili kwa kutumia lugha ya Kiswahili kuwahusu waswahili, na fasihi kwa lugha ya Kiswahili ni ile iliyoandaliwa na mtu yeyote asiye mswahili bali ametumia lugha ya Kiswahili au iliyoandaliwa kwa lugha nyingine kasha ikatafsiriwa kwa lugha ya Kiswahili.
Fasihi ya Kiswahili ya waswahili inatofautiana sana na fasihi kwa lugha ya Kiswahili kwa kuzingatia vipengele vifuatavyo:
Moja, maandalizi: fasihi ya Kiswahili ya waswahili huandaliwa na mswahili kwa lugha ya Kiswahili. Fasihi hii hujikita zaidi katika kuelezea mambo yanayowahusu waswahili lakini fasihi kwa lugha ya Kiswahili huandaliwa na mtu asiye mswahili na aghalabu huihusu jamii yake au jamii ingine tu kwa kutumia lugha ya Kiswahili.
Pili, matumizi ya lugha: fasihi ya Kiswahili ya waswahili hutumia lugha sanifu na fasaha yenye kuficha mambo kwa sababu mtunzi huwa anakijua Kiswahili na jinsi ya kukitumia lakini fasihi kwa lugha ya Kiswahili huwa na lugha ya kawaida na mambo huelezwa wazi hata yale yasiyopaswa kuanikwa hadharani kutokana na uwezo mdogo wa mtunzi katika kuimudu lugha.
Tatu, mandhari: fasihi ya Kiswahili hutumia mandhari ya pwani kwa kiasi kikubwa kwa sababu ndiko anakotokea mtunzi lakini fasihi kwa lugha ya Kiswahili hutumia mandhari mchanganyiko kulingana na upeo wa mtunzi kimazingira.
Nne, wahusika: wahusika wa fasihi ya Kiswahili ya waswahili hutambulika wazi kwa majina, mavazi na matendo yao ambayo hufungamana na imani yao. Kwa mfano kanzu, baibui lakini fasihi kwa lugha ya Kiswahili huweza kuchanganya majina ya wahusika na hasa yasiyojipambanua wazi kiimani kwa mfano Dongo, Jalia, Mzee Toboa au Lomolomo.
Tano, shughuliza kiuchumi: fasihi ya Kiswahili ya waswahili itazungumzia shughuli za kiuchumi za pwani kama vile uvuvi wa baharini, kilimo cha mazao yanayostawi pwani kama nazi, mwani, karafuu lakini fasihi kwa lugha ya Kiswahili ambayo mtunzi wake ni mwenyeji wa maeneo ya bara atazungumzia shughuli za uzalishaji mali hasa kilimo cha kahawa, ndizi, pamba au mahindi.
Pamoja na tofauti hizo fasihi ya Kiswahili na fasihi kwa lugha ya Kiswahili zina mchango mkubwa kwa jamii katika kukuza na kuendeleza mila na desturi za jamii kwa ujumla.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)