09-01-2021, 01:42 PM
NAACHAJE?
Moyoni ameingia, naachaje kumpenda?
Mahaba anayajua, naahidi kumlinda,
Machoni anavutia, kwa mwingine sitoenda,
Naachaje kumpenda, mrembo aloumbika?
Mfano wake siuoni, uzuri alojaliwa,
Ngozi yake ya laini, kipenzi ameumbiwa,
Mwingine sitotamani, ya nini kujisumbua?
Naachaje kumpenda, mrembo aloumbika?
Anipatia furaha, daima nachekelea,
Vi maneno vya mzaha, hachoki kuniambia,
Si mjuzi wa karaha, mrembo ametulia,
Naachaje kumpenda, mrembo alojmbika?
Naahidi kumlinda, wezi wasimkwapue,
Wakafanya nikakonda, rahaye niijutie,
Nikikosa langu tunda, nitaghafirika mie,
Naachaje kumpenda, mrembo aloumbika?
Moyoni ameingia, naachaje kumpenda?
Mahaba anayajua, naahidi kumlinda,
Machoni anavutia, kwa mwingine sitoenda,
Naachaje kumpenda, mrembo aloumbika?
Mfano wake siuoni, uzuri alojaliwa,
Ngozi yake ya laini, kipenzi ameumbiwa,
Mwingine sitotamani, ya nini kujisumbua?
Naachaje kumpenda, mrembo aloumbika?
Anipatia furaha, daima nachekelea,
Vi maneno vya mzaha, hachoki kuniambia,
Si mjuzi wa karaha, mrembo ametulia,
Naachaje kumpenda, mrembo alojmbika?
Naahidi kumlinda, wezi wasimkwapue,
Wakafanya nikakonda, rahaye niijutie,
Nikikosa langu tunda, nitaghafirika mie,
Naachaje kumpenda, mrembo aloumbika?