MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
VYOMBO ( ASASI ) MBALI MBALI VYA KUKUZA NA KUENEZA KISWAHILI NCHINI

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
VYOMBO ( ASASI ) MBALI MBALI VYA KUKUZA NA KUENEZA KISWAHILI NCHINI
#1
Baada ya uhuru, serikali imechukua hatua mbali mbali ili kukuza na kueneza Kiswahili . hatua moja wapo ni ile ya kuunda asasi za ukuzaji Kiswahili.  Asasi hizo ni:
  1. UKUTA
 Hiki ni chama cha Usanifu wa Kiswahili na Mashairi . chama hiki kilianzishwa mwaka 1965 na mshairi Mathias Mnyapala kwa lengo la kukuza ushairi wa Kiswahili kwa ujumla.
  Ukuta ilikuwa na malengo yafuatayo:
     a). Kukuza lugha ya Kiswahili na ushairi kwa ujumla kwa njia ya kujishughulisha na kazi tafauti zinazohusiana na maendeleo ya Kiswahili na ushairi kama vile uhariri wa miswada ya Kiswahili, utunzi wa mashairi na uandishi wa vitabu na kutafsiri maandishi mbali mbali katika Kiswahili.
     b).  Kukuza utunzi wa ngonjera na kuhamasisha utunzi wa vitabu katika misingi yenye kuzingatia utamaduni wa Mtanzania.
Mafanikio ya UKUTA.
     c).   Imeweza kuundaa na kuendesha semina na makongamano ya Kiswahili na kutunga kazi za fasihi kwa kushirikiana na vyombo vingine.
     d).   UKUTA imeweza kuandika vitabu mbali mbali vya ushairi hususan vya ushairi, kama vile Ngonjera za  ukuta ( cha kwanza na cha pili – 1968 ), Mashairi ya Azimio la Arusha – 1974 na Mashairi ya miaka kumi ya Azimio la Arusha – 1977.
     e).   Imeweza kutafsiri kwa Kiswahili maandishi mbali mbali . mfano , iliwza kutafisiri majina ya baadhi ya mitaa ya jiji la Dar – es – Salaam kama vile mtaa wa uhuru badala Independence Avenue na mtaa wa Sokoine badala ya Sokoine Drive.
  1. TUKI ( Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili ).
     Taasisi hii kihistoria ilianzishwa mwaka 1930 ikiwa kamati ya lugha ya lugha ya Afrika Mashariki na uatwala wa Waingereza , na mnamo mwaka mwaka 1964, ilipandishwa hadhi na kuhamishiwa katika chuo kikuu cha Dar –es – Salaam baada ya kuimarishwa kwa sheria ya Bunge ya mwaka 1964. Na mwaka 1970 kilipoanzishwa chuo kikuu cha Dar –es Salaam taasisi ilikuwa moja wapo wa asasi za utafiti wa chuo, ambapo mpaka leo asasi hii imekuwa ikifanya kazi chini ya Chuo Kikuu,
    Mnamo mwaka 2009, taasisi hii ilibadili jina baada ya kuungana na Idara ya Kiswahili ya chuo na kujulikana kwa jina la Taasisi ya Taaluma za Kiswahili. ( TATAKI ).
    Malengo ya TUKI ( TATAKI ).
       i).  Kuichunguza na kuiendeleza lugha ya Kiswahili katika fani zake zote ikizingatia mipango ya muda mrefu katika Jamhuri ya Muungao wa Tanzania, Afrika na mashariki na Katika chuo kikuu cha Dar es Salaam.
3.BAKITA ( Baraza la Kiswahili Tanzania).
        Baraza hili liliundwa mwaka 1967 kaw sheria ya Bunge Na. 27. Ya mwaka huo.
        Malengo makuu ya uundwaji wa baraza hili ni kutaka kuwepo kwa chombo nchini cha kusimamia shughuli za ukuzaji Kiswahili.
KAZI ZA BAKITA.
   i). Kuhimiza matumizi ya Kiswahili fasaha, kuandika vitabu vya Kiswahili na taaluma zake hususan fasihi na sarufi.
   ii).  Kutoa huduma za ukalimani kwa serikali na mashirika
   iii). Kuratibu kazi za ukuzaji Kiswahili nchini na zile zinazofanyika nchi za nje.
    iv). Kuchapisha majarida ya Kiswahili yatakayoongoza matumizi sahihi ya maneno na maendeleo yake.
    v). Kuchunguza usahihi wa lugha ya Kiswahili inayotumika katika uandishi wa vitabu mbali mbali vinavyokusudiwa kutumika kufundishia shuleni na vyuoni kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu.
   vi). Hujishughulisha na uthibitishaji wa tafsiri sanifuza isitilahi na kusimamia utafiti wa lugha ya Kiswahili.
   vii). Kutoa ushauri kwa waandishi na wachapishaji kuhusu utumiaji wa Kiswahili fasaha na kuratibu maendeleo ya Kiswahili nchini.
        Katika utekelezaji wa shughuli zake, baraza hilo limeanzisha idara tano za taaluma. Nazo ni:
  Idara ya Uhariri na Uchapishaji.
   Idara hii hujishughulisha na  masuala mbali mbali ya uchapaji wa taarifa za BAKITA na majarida mengine.
Idara ya Lugha na Fasihi.
    Idara hii husimamia matumizi sahihi ya Kiswahili sanifu katika vyombo vya habari  na matumizi rasmi na kutoa ithibati ya vitabu vya Kiswahili vinavyokusudiwa kutumika katika elimu.
Idara ya Tafsiri na Ukalimani.
Idara hii hujishughulisha na kutoa huduma za tafsiri na ukalimani kwa lugha ya Kiswahili kwa mashirika,idara,wizara,balozi na watu binafsi.
 Idara ya Istilahi na kamusi.
Hii inafanya kazi ya kufanya tafiti za isitilahi, kuandaa orodha ya isitilahi na kuandaa kamusi kwa matumizi ya asasi, shule na watu wa aina mbali mbali.
Idara ya Uhusiano
Idara hii inafanya kazi ya kutangaza kazi za shughuli za baraza kwa kutumia radio,magazete na majarida na kusimamia vipindi vya Kiswahili katika radio na televisheni, pamoja kuimarisha uhusiano baina ya vyombo vya ukuzaji Kiswahili kwa kuandaa warsha na semina.
MAFANIKIO YA BAKITA
.  Bakita imeandaa isitalahi za taaluma mbali mbali kama vile za Fizkia, Kemia, Uchumi, Ufundi, Bunge , maktaba n.k
.  Bakita inatoa majarida mbali mbali yanayohusu lugha ya Kiswahili kama vile lugha yetu tusome tuijue, jifunze Kiswahili uwafunze wengine , lugha ya kiswahili – fasihi na sarufi yaken.k
.  Bakita huendesha vipindi mbali mbali vya Kiswahili katika radio Tanzania dar es sallam  kama vile lugha yetu, ulimwengu wa Kiswahili, Kiswahili lugha ya taifa n. k
MATATIZO YA BAKITA.
  1. Uhaba wa fedha wa kuendeshea shughuli za bakita, kama vile warsha ,semina,makongamano uchapishaji wa majirida.
  2. Uhaba wataalamu
4). TAASISI YA KISWHILI NA LUGHA ZA KIGENI. ( TAKILUKI ).
    Taasisi hii iliundwa mwaka 1979 ikiwa chini ya Wizara ya Elimu  na Mafuzo ya Amali Zanzibar.
 Lengo kubwa ya kuanzishwa taasisi hii ni :Kusimamia na kuendeaha shughuli za ukuzaji wa kiswahli na lugha za kigeni kisiwani humo.
KAZI ZA TAKILUKI:
  1. Kutoa mafunzo na elimu ya Kiswahili kwa kiwango cha juu kwa watumishi wa serikali na viongozi wa chama ua vyama ili kukuza ujuzi wa Kiswahili  na kuzumgumza Kiswahili fasaha
  2. Kufanya utafiti wa Kiswahili , kuandika vitabu vya taaluma mbali mbali za Kiswahili na kutafsiri katika kisahili maandishi mbali mbali yaliyo katika lugha za kigeni.
  3. Kuhimiza matumizi ya Kiswahili fasaha , kuchapisha vitabu vya Kiswahili  na kuwapa waandishi chipukizi miongozo ya uandishi sahihi wa vitabu.
  4. Kuratibu na kusimamia maendeleo ya Kiswahili visiwani Zanzibar pamoja na kuendesha mafunzo ya lugha ya Kiswahili kwa wazawa na wageni
  5. Kuandaa isitalahi za taaluma mbali mbali pamoja na kutoa huduma za tafsiri na ukalimani kwamashirika ,idara wizara kampuni,na watu binafsi , pia hufundisha lugha za kigeni kama vele GR, PR FR ARB CHINA na kuandika vitabu vya Kiswahili.
  6. Hujishughulisha na ufuatiliaji pamoja na usimamizi wa matumizi sahihi ya Kiswahili katika vyombo vya habari katika shughuli mbali mbali za serkali na za kawaida.
  7. Kufanya utafiti wa lahaja na fasihi simulizi ya Kiswahili.
MAFANIKIO YA TAKILUKI.
Takiluki imepata mafanikio kadhaa yakiwemo haya yafutayo:
  1. Kuchapisha vitabu mbali mbali vya Kiswahili kama vile malenga wapya, na tungo zakale.
  2. Kuandaa na kuendesha semina na makongamano mbali mbali ya Kiswahili.
  3. Kuhimiza ufundishaji wa Kiswahili visiwani Zanzibar.kushirikiana na vyombo mbali mbali vyaukuzaji lugha ya Kiswahili katika kutekeleza mipango mbali mbali ya ukuzaji Kiswahili.
BAKIZA. ( BARAZA LA KISWAHILI ZANZIBAR ).
     Ni chombo chengine ambacho kimesidia kukuza na kustawisha kugha ya Kiswahili visiwani Zanzibar. Baraza hili lilianzishwa mwaka 1983.
KAZI ZA BAKIZA.
  • Kuratibu na kusimamia maendeleo ya Kiswahili visiwani Zanzibar.
  • Kuhimiza matumizi ya Kiswahili fasaha na kufanya utafiti wa Kiswahili kwa kushirikiana na vyombo vingine.
  • Kuendesha semina za Kiswahili na kuwafundisha waandishi misingi ya uandishi.
  • Huratibu maendeleo ya Kiswahili na kutoa ushauri kwa serikali kuhusu namna ya kufanikisha ukuzaji wa Kiswahili ndani nan je ya Zanzibar.
CHAMA CHA KISWAHILI CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM
           Chama hiki kilianzishwa mwaka 1970 kwa juhudi za mwanzo za wanafunzi walioingia chuo kikuu kusoma Kiswahili katika ngazi ya shahada ya kwanza.
      Chombo hiki kilikuwa na madhumuni yafuatayo:
  • Kuwapa wanachama nafasi ya kuvumbua na kukuza vipawa vyao katika isimu na fasihi ya Kiswahili.
  • Kuamsha ari ya kimapinduzi katika kuendeleza lugha ya Kiswahili kwa njia ya uchunguzi namaandishi.
MAFANIKIO YA CHAMA HIKI.
  1. Kutoa jarida ya kioo cha lugha.
  2. Kutoa nafasi kwa walimu na wanafunzi kujadili na kuhakiki fani mbali mbali za isimu na fasihi.
  3. Kuongoza makongamano ambayo mijadala yake huhaririwa na kutolewa katika kijarida kiitwacho ZINDUKO.
TAASISI YA ELIMU.
    Taassisi hii ilianzishwa mwaka 1966  na ilikuwa na kazi zifuatazo:
  1. Kutayarisha mihutasari ya masomo ya shule za msingi na sekondari  pamoja vyuo vya elimu.
  2. Kutayarisha na kuongoza semina mbali mbali  kwa walimu ili waweze kufundisha vyema lugha ya Kiswahili.
  3. Kutoa muongozo mpya kuhusu utahini wa somo la Kiswahili katika kidato cha tatu na nne wakishirikiana na baraza la mitihani la taifa.
MAFANIKIO YA TAASISI HII.
  • Kuandaa mihutasari ya masomo mbali mbali hapa nchini.
  • Kuandaa vitabu vya kufundishi Kiswahili sekondari kama vile Kiswahili kidato cha 1 – 4 (1996).
TAASISI YA ELIMU YA WATU WAZIMA.
       Taasisi hii ilianzishwa mwaka 1963. Kama chombo cha kuwasaidia wazelendo  katika stadi za kusoma na kuandika ambao hawakupata fursa ya kupata elimu katika ngazi ya msingi na sekondari.
   Baadhi ya mafanikio ya elimu ya watu wazima ni:
  • Kufanikiwa kutoa elimu ya watu wazima katika stadi za kusoma na kuandika wakati wa jioni kwa lengo la kufuta ujinga .
  • Kutoa masomo kwa njia ya posta kwa kidato cha kwanza hadi cha sita katika somo la Kiswahili.
  • Kuanzisha maktaba makao makuu ambayo huwasidia wanafunzi kupata vitabu na majarida mbali mbali ya Kiswahili.
  • Kunzisha idara ya mafunzo ya elimu ya watu wazima ambapo wanafunzi kutoka ndani na n je ya nchi husomea diploma ya elimu ya watu wazima.
IDARA YA KISWAHILI – CHUO KIKUU DAR ES SALAAM
 Idara hii ilianzishwa mwaka 1970 baada ya kuanzishwa chuo kikuu.
    Kazi kubwa ya idara hii ilikuwa ni:
  • Kutayarisha walimu na wataalamu wenye shahada katika somo la Kiswahili ili waweze kufundisha mashuleni na vyuoni.
  Mafanikio makubwa ya idara hii ni kuweza kutoa walimu wengi wenye shahada  ya Kiswahili wanaofundisha mashuleni mashuleni na vyuoni,
   Pia imeweza walimu wenye shahada ya pili , tatu  na hata uprofesa wa lugha ya kiswahili.
CHAMA CHA KISWAHILI CHA AFRIKA.
     Chama hiki kiliundwa katika semina ya kimataifa kuhusu usanifishaji wa isitilahi za Kiswahili iliyofanyika chuo kikuu dar es salaam mwaka 1978. Ikiwa na wajumbe tafauti waliotoka nchi za Kenya, Tanzania, msumbuji, na Zambia ikiwa na madhumuni yafuatayo:
  • Kukuza kueneza Kiswahili kote afrika.
  • Kuleta umoja katika mataifa ya kiafrika kwa kutumia lugha ya asili.
Pia semina nyengine iliandaliwa tena mwaka 1983 na kuhudhuriwa na wajumbe kutoka Kenya, Rwanda, Comoro, Uganda, DRC, Zanzibar  na kutoka radio mbali mbali kama vile India, BBC, RTD, Radio Rwanda n.k na waliazimia mambo yafuatayo:
  • Kuandaa mikutano ,semina na warsha  zitakazotumika kuchambua isitilahi za Kiswahili badala ya kawaachia Tanzania peke yake.
  • Kusambaza isitilahi za Kiswahili zitumike na watu wa kawaida na hasa wale wanaojishughuisha na ukuzaji Kiswahili ndani na nje ya mipaka yake.
  • Kupendekeza mpango wa usanifishaji wa isitilahi uwe wa kiwango cha kimataifa.
  • Kuanzisha jarida makhsusi ambalo litajidili masuala ya usanifishaji ili kuimarisha taasisi mbali mbali zinazo jishughulisha na Kiswahili kama vile unesco.
MATATIZO YA CHAKA.
  • Kuachiwa Tanzania peke yake katika usanifishaji wa isitilahi.
  • Kutafsiriwa kwa maneno ya kigeni bila ya utafiti mkubwa ambayo hupelekea kutokuwa na mvuto kwa wasomaji wa kawaida.
  • Kutokuwa na msukumo wa viongozi wa nchi wanachama kwani viongozi wengine walipiga vita shughuli hii badala ya kutoa ushauri na kuhimiza.
UWAVITA. ( Umoja wa waandishi wa vitabu Tanzania ).
   Umoja huu ulianzishwa mwaka 1974 na ulikuwa na madhumuni yafuatayo:
  • Kuwahimiza watu kuandika vitabu mbali mbali vya Kiswahili.
  • Kuwasidia waandishi chipukizi ikiwa ni pamoja kuwafahamisha uandishi wa masuala mali mbali ya fasihi.kujishughulisha na kukikuza na kukitangaza Kiswahili katika vyombo vya habari kama vile radio na magazeti.
  • Kutetea maslahi ya waandishi wa kitanzania ili kuwaunganisha pamoja.
  • Kubuni na kuendesha miradi ya uandisshi, uchapaji na uchapishaji.
  • Kuwaelimisha wananchi juu ya umuhimu wa kusoma, uandishi wa vitabu na Sanaa zinazoambatana nazo kwa njia ya radio na magazeti.
TATHMINI YA MAENDELEO YA KISWAHILI BAADA YA UHURU.
       Lugha ya Kiswahili baada ya uhuru imepata mafanikio kadhaa. Miongoni mwa mafanikio hayo ni:
  1. Uendelezwaji wa Kiswahili.
    Kiswahili kimeweza kuendelezwa kwa njia mbali mbali kama vile kufundisha kama somo moja wapo katika ngazi zote za elimu nchini, kufanyiwa utafiti, kusanifiwa na kutumika kama lugha kuu ya mawasiliano.
  1. Kuongezeka kasi ya ueneaji wa lugha ya Kiswahili.
         Kiswahii kimeweza kuenea hadi nje ya Tanzania katika mataifa mbali mbali na hata kufikia moja wapo lugha ya kimataifa na pia kuongezeka msamiati.
  1. Kuongezeka kwa uundwaji wa vyombo vya ukuzaji Kiswahili.
    Kuendelea kujitokeza vyombo mbali mbali vya ukuzaji wa Kiswahili ndani na nje ya Tanzania  ni mafanikio makubwa kwa upande wa lugha ya Kiswahili kwa sababu vyombo hivyo vimewea kuikuza lugha ya Kiswahili kwa njia mbali mbali.
  1. Kutumika Kiswahili katika vyombo vya habari vya nje.
    Kuendelea kutumika lugha ya Kiswahili katika vyombo mbali mbali vya habari vya nje kama viel BBC. Deutchwelle,radio japani, sauti ya amerika na nyinginezo kumeifanya lugha ya Kiswahili kuwa miongoni mwa lugha mashuhuri duniani
CHANGAMOTO ZINAZOATHIRI MAENDELEO YA KISWAHILI.
   Pamoja na mafanikio hayo ,zimekuwapo changamoto kadhaa zinazoathiri maendeleo ya Kiswahili. Baadhi ya changamoto hizo ni:
  • Upotoshwaji wa lugha ya Kiswahili.
       Upotwashwaji wa Kiswahili hutokea kwa namna kadhaa mfano ni wa uchanganyaji wa Kiswahili na kingereza na pia kutumia Kiswahili kwa maneno yasio yanifu na pia utumizi wa Kiswahili ulioathiriwa na sarufi ya lugha za kikabila hususan kimatamshi na kimuundo.
  • Athari za lugha za kigeni.
Tatizo la kutokithamini Kiswahili miongoni mwa wanajamii ni changamoto ya kuathiriwa na kasumba za ukoloni ambapo wanajamii huthamini Zaidi lugha za kigeni hususan kingereza.
  • Kutokuwepo uwiano wa kimatumizi.
Hii ni changamoto nyengine ambapo Kiswahili hakina uwiano wa kimatumizi katika nchi nzima, tofauti hizi zipo kutokana na jamii moja na nyingine kuathiriwa na lugha mama.
  • Utafauti wa sera .malengo na mipango ya vyombo vya ukuzaji Kiswahili.
  Juhudi za ukuzaji Kiswahili zinaonekana hazina mashiko kutokana na kuwepo idadi kubwa ya vyombo vya ukuzaji Kiswahili ambayo havina mshikamano wa pamoja kwani kila chombo kina malengo,sera, na mipango ya yake ya uendeshaji wa Kiswahili.
  • Uhaba wa wataalamu.
  Uhaba wa wataalamu katika vyombo vya ukuzaji wa Kiswahili husababisha vyombo kutofanya  na kutekeleza malengo kwa ufanisi.
  • Kutokwepo mpango wa kukitumia Kiswahili kama lugha ya kufundishia.
   Ni tatizo jengine linalokwanishwa maendeleo ya Kiswahili kwa kutotekelezwa kwa mpango wa kukitumia Kiswahili kama lugha ya kufundishia katika ngazi zote za elimu nchini, na hivyo kutoa mwanya hasa kwa lugha za kigeni kama vile kingereza kustawi zaidi na hivyo kuathiri nafasi ya Kiswahili katika jamii.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)