MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
ETIMOLOJIA YA NENO "BULIBULI'' - Printable Version
JIFUNZE KISWAHILI
ETIMOLOJIA YA NENO "BULIBULI'' - Printable Version

+- JIFUNZE KISWAHILI (https://jifunzekiswahili.co.tz)
+-- Forum: My Category (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=1)
+--- Forum: Majadiliano ya Wadau wa Kiswahili (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=16)
+--- Thread: ETIMOLOJIA YA NENO "BULIBULI'' (/showthread.php?tid=2815)



ETIMOLOJIA YA NENO "BULIBULI'' - MwlMaeda - 08-28-2022

HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO "BULIBULI''

Neno *bulibuli* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino: [Ngeli: i-/zi-*] yenye maana ya mtindo mmojawapo wa kofia nyeupe yenye nakshi (viua) inayovaliwa hasa mwambao wa pwani ya Afrika Mashariki, kofia ya kazi.

Pia ni kivumishi kwa maana ya: -zuri, -a kupendeza, bambam, -ema.

Mwanafunzi mwenye tabia bulibuli hufaulu vizuri katika mitihani yake.

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *bulibuli* linatokana na nomino ya Kiarabu *bulbulu بلبل* yenye maana zifuatazo:

1. Ndege mdogo aina ya kunega maarufu kwa kuimba vizuri.

2. Sehemu ya kumiminia maji katika birika.

Kinachodhihiri ni kuwa neno *bulbulu  بلبل* lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *bulibuli* lilichukua maana mpya ya (nomino) kofia yenye viua inayovaliwa pwani ya Afrika Mashariki na maana ya (kivumishi): -zuri, -a kupendeza, bambam, -ema.

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*