MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
ETIMOLOJIA YA NENO 'ANUANI/ANWANI' - Printable Version
JIFUNZE KISWAHILI
ETIMOLOJIA YA NENO 'ANUANI/ANWANI' - Printable Version

+- JIFUNZE KISWAHILI (https://jifunzekiswahili.co.tz)
+-- Forum: My Category (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=1)
+--- Forum: Majadiliano ya Wadau wa Kiswahili (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=16)
+--- Thread: ETIMOLOJIA YA NENO 'ANUANI/ANWANI' (/showthread.php?tid=2526)



ETIMOLOJIA YA NENO 'ANUANI/ANWANI' - MwlMaeda - 04-23-2022

HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'ANUANI/ANWANI'

Neno *anuani/anwani*  katika lugha ya Kiswahili ni *Nomino [Ngeli: i-/zi-]* yenye maana zifuatazo:

1. Maelezo ya mahali ambapo mtu huishi au hufanya kazi, ambayo husaidia kumfikishia kufurushi au barua iliyotumwa hasa kwa njia ya posta; mahali panapotumiwa kufikishia barua.

2. Akaunti ya mtandao wa kutuma na kupokea barua kupitia mfumo wa intaneti.

3. Mada au jina la kitabu.

Katika lugha ya Kiarabu neno *anuani/anwani* linatokana na neno la Kiarabu  *unwaaanu (soma: unwaanun/unwaanan/unwaanin عنوان)* lenye maana  zifuatazo:

1. Kinachotoa utambulisho wa kipekee kwa kitu usiofanana na mwengine. Kwa mfano: *Unwaanul Kitaabi  عنوان الكتاب* anuani ya kitabu.

2. Maandishi yaliyodhihirishwa yanayoelezea kilichofichwa.

3. Maandishi yanayoandikwa juu ya bahasha kubainisha anayepelekewa na makazi yake.

Kinachodhihiri ni kuwa neno *unwaanun  عنوان*  lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa  kuwa neno *anuani/anwani* maana yake katika lugha ya asili - Kiarabu inayohusu utambulisho haikubadilika.

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*