MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
ETIMOLOJIA YA NENO 'AMI' - Printable Version
JIFUNZE KISWAHILI
ETIMOLOJIA YA NENO 'AMI' - Printable Version

+- JIFUNZE KISWAHILI (https://jifunzekiswahili.co.tz)
+-- Forum: My Category (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=1)
+--- Forum: Majadiliano ya Wadau wa Kiswahili (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=16)
+--- Thread: ETIMOLOJIA YA NENO 'AMI' (/showthread.php?tid=2513)



ETIMOLOJIA YA NENO 'AMI' - MwlMaeda - 04-16-2022

HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'AMI' 

Neno *ami*  katika lugha ya Kiswahili ni *Nomino [Ngeli: a-/wa-]* yenye maana zifuatazo:

1. *Nomino [Ngeli: a-/wa-]* mwanamume aliyezaliwa tumbo moja na baba.

2. *Nomino [Ngeli: a-/wa-]* mwanamume anayependa umaridadi na kujinadi.

3. *Kihisishi*, neno linalotumika kumwita mtu aghalabu wa rika lolote badala ya jina lake.

Katika lugha ya Kiarabu neno *ami* linatokana na neno la Kiarabu  *ammu (soma: ammun/amman/ammin عم)* lenye maana zifuatazo:

1. Ndugu mwanamume aliyezaliwa tumbo moja na baba.

2. Kundi kubwa la watu.

3. Mtende mrefu.

Kinachodhihiri ni kuwa neno *ammun  عم*  lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa  kuwa neno *ami* maana yake ya msingi katika lugha asili - Kiarabu haikubadilika bali Waswahili walilipa neno hili maana mpya ya *mwanamume anayependa umaridadi na kujinadi.* na *kihisishi cha kumwita mtu badala ya jina lake.* na kuacha maana zingine katika lugha asili - Kiarabu.

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*