MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI - KISA CHA KUSISIMUA

JIFUNZE KISWAHILI

Full Version: KISA CHA KUSISIMUA
You're currently viewing a stripped down version of our content. View the full version with proper formatting.
INASIKITISHA JAMANI SOMA HII!
Baba na mama baada ya kurudi kazini pamoja wakakuta BARUA iko mezani SEBULENI ikisema…. “Baba na mama, ni matumaini yangu kuwa mtasoma ujumbe wangu huu kwenye karatasi niliyoiweka
juu ya meza, naomba msishtuke mana ni mambo ya kawaida kwenye maisha tunayoishi, najua mtaumia kwa vile bado nasoma na ndo nipo kidato cha kwanza…” Napenda kuwajulisha kwamba sasa hivi mnaposoma hii barua sipo nyumbani, nimetoroka mana nimegundua nina uwezo wa kujitegemea kwa sababu mi ni kijana mwenyewe umri wa miaka 14 na ninajua kipi chema na kipi kibaya. Tangu mwezi mmoja uliopita nilikuwa na uhusiano na binti mmoja aliyeitwa Rachel, mwenye umri wa miaka 27 na kwa sasa ndo naishi naye kwenye chumba alichopanga. Nilipokuwa nyumbani sikuwa napata hela za kutosha ila sasa nimeanza kushika noti za shilingi 10,000… Msichana niliyenaye ni mzuri sana wa umbo na ninampenda sana, amenifundisha njia za kutafuta hela. Amenipangia kazi ya kuuza madawa ya kulevya na yeye ikifika usiku
anaenda kuuza mwili wake, basi kila siku tunapata hela ya kutosha, huyu mchumba wangu ni msichana mwenye bidii, kwa siku analala masaa 6 tu maana mwanaume yeyote akija lazima awe naye chumbani kwa muda wa masaa 3. Msiwe na hofu, nipo salama kabisa na nimeamua kumwoa Rachel mana ni kila kitu kwangu. Pia amenunua gari la kubebea mbao kwahiyo biashara inaenda vizuri, Rachel ameenda kupima afya na amekutwa na upungufu wa kinga mwilini,mara nyingi namridhisha anapotaka kitu flani, iwe kufanya
naye mazoezi ya viungo au kufanya naye mapenzi, si mnajua unapokuwa na mgonjwa unakuwa naye karibu, ila mi pia sijihisi vizuri mana kila saa nakohoa tu na sina uhakika kama nimeathirika. Tumepanga baada ya miaka miwili tutawatembelea, nadhani mpaka miaka miwili iishe atakuwa ameshajifungua, na ni furaha yangu mtamwona mjukuu wenu. Wazazi wangu sina la kuongeza kwaherini Mungu akipenda tutaonana.

 NB: “Baba na mama, mi nipo chumbani kwangu najisomea, mnachokisoma ni home work ya mwalimu wa kiswahili alituambia tutunge hadithi fupi ya kusisimua, naomba muiangaliekama kuna
makosa