MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI - SIMULIZI : “JENEZA LA AJABU” **SEHEMU YA 13**

JIFUNZE KISWAHILI

Full Version: SIMULIZI : “JENEZA LA AJABU” **SEHEMU YA 13**
You're currently viewing a stripped down version of our content. View the full version with proper formatting.
SIMULIZI : “JENEZA LA AJABU”
**SEHEMU YA 13**
Msitu wa majini;
Njoshi anapata fahamu usiku wa manane, huku ngome ya malikia ikiwa kimya sana kwani majini wote walikuwa wamelala. Akiwa na maumivu makali, huku damu ikichuruzika kutoka mwilini mwake, kutoka katika majeraha ambayo aliweza kung’atwa na nge pamoja na siafu. Aliyazungusha macho yake kuangaza kila sehemu katika ngome ya malikia, lakini hakuweza kumwona jini yoyote aliyekuwa akimtazama.
Haraka haraka bila kupoteza muda kwani aliona huo ndio ulikuwa wakati sahihi wa yeye kutoroka, alijaribu kufungua kamba ngumu ya katani iliyotumika kufunga mikono yake katika mti wa mateso, na hatimae aliweza kufanikiwa.
Baada ya kujifungua kamba kutoka katika mti ule, alichukua begi lake ambalo alikuwa bado amelivaa, kwani hawakumnyanganya baada ya kulikagua na wala hawakukuta kitu chochote. Lakini alipotaka kujifuta damu mwilini mwake, aliamua kukagua begi lake ili aone kama chochote niite kupata kitambaa chochote aweze kufuta damu na kusafisha majeraha yake.
“Eeeeh mizimu ya mababu nini hiki?, “,Njoshi aliongea baada ya kukuta kipande kidogo cha jiwe ndani ya begi, lakini kipande hiki kiling’aa kama dhahabu. Kipande hiki kilifichwa ndani ya begi, sehemu ambayo ilikuwa ni ngumu kuliona kama ukikagua begi kwa papala, kama alivyofanya jini aliyekagua begi mwanzoni kwani siku zote haraka haraka haina baraka. Njoshi alitaka kulitupa jiwe hili, lakini roho yake ilisita kwani aliyakumbuka maneno ya mama yake kuwa asiweze kuliacha begi lile. Hivyo aliamini lazima jiwe lile litakuwa na msaada kwake, na bila kupoteza muda kuendelea kulishangaa jiwe lile ,aliliweka mfukoni ili atokomee kutoka katika ngome hatari ya malikia.
“Heeeeeh ……mbona kama mazingaombwe,! “Njoshi alishangaa baada ya kuliweka jiwe lile mfukoni, na kuona majeraha yote yakipona huku sumu ya nge ikimtoka mwilini.
“Ahaaaah, tayali nilishafahamu hili jiwe ni muhimu kwangu “,Njoshi alitamka maneno yale kwani tayali alitambua jiwe lile ndio lililomponya, hivyo basi alilifunga vizuri katika mfuko wa kaptura yake lisiweze kudondoka na kupotea.
 Baada ya jambo hilo kutokea, Njoshi alielekea ndani kwa malikia huku majini wote wakishindwa kugundua chochote, jambo ambalo lilikuwa la ajabu sana. Aliendelea kupenya ndani kwa malikia, na kukagua kila kona lakini hakuweza kuliona panga wala kitambaa chake. Njoshi aliendelea kupekua huku na kule lakini hakufanikiwa, hivyo basi aliamua kuahirisha kila kitu ili atoke ndani ya msitu kuyaokoa maisha yake kabla hapajakucha, kwani tayali alikuwa hajaona fimbo ya kifalme wala panga pamoja na kitambaa.
Njoshi akiwa anatoka katika lango la malikia, alishangaa kuona kabati moja iliyokuwa karibu na mlango wa nyumba ya malikia ikijifungua huku miale kama ya jua ikitoka mfukoni mwake. Akiwa anashangaa miale ile, aliamua kulitoa jiwe lile mfukoni kwake, na baada ya kulishika mkononi, miale mikali ilitoka katika jiwe lile na kusababisha kufuli kubwa la ajabu katika kabati ile kujifungua.
“Aiseeeh asante sana mama, jiwe hili linamsaada mkubwa kwangu, sikujua kama linanguvu kiasi hiki “,Njoshi aliongea maneno ya furaha huku akiitazama fimbo ya kifalme, fimbo iliyokuwa inang’aa sanaa kwani ilitegenezwa kwa dhahabu, madini ambayo yalionekana kutumika pia kutengenezea jiwe la ajabu ambalo lilionekana kuwa msaada mkubwa kwa Njoshi. Haraka sana ikiwa tayali giza limeanza kutoweka, huku sauti za ndege walioamka mapema zikianza kusikika, Njoshi aliichukua fimbo ile na kisha kuchukua kalamu ya ajabu iliyokuwa pembeni ya fimbo ile ndani ya kabati.
“MFALME NJOSHI “,yalikuwa ni maneno ambayo Njoshi aliweza kuyaandika katika fimbo ya kifalme, kwa kutumia kalamu ya ajabu na kisha kucheka kwa sauti kubwa sana, kicheko cha furaha kwani tayali angeweza kuwa mfalme kama akifanikiwa kutoka nje ya msitu na fimbo ile ya kifalme. Japo Njoshi alicheka kwa sauti kubwa, majini ambao walionekana kulala sana siku hiyo, hawakuweza kusikia chochote kile bila kufahamu kuwa jiwe lile ndio liliweza kufanya maajabu yale yote.
“Hapa ngoja nikatengeneze JENEZA LA AJABU, harafu nirudi nyumbani “,Njoshi alizungumza kwa ujasiri huku akitabasamu, na kisha kutimua mbio kuelekea katikati ya msitu kutengeneza jeneza la ajabu, jeneza ambalo mfalme Mutapa atafufuka baada ya wiki moja kama akizikwa ndani yake.
Bila kutegemea Njoshi aliweza kupita katika geti la malikia, geti ambalo lilinyunyiziwa maji ya ajabu na kumgandisha binadamu yoyote ambaye angeyakanyaga maji hayo.Lakini kwa wakati huu, alipita bila tatizo lolote jambo ambalo lilimfanya Njoshi alibusu jiwe lile, jiwe ambalo alilishika kwa nguvu katika mkono wake wa kulia kwani ndio siraha pekee aliyonayo kwa muda huu.
“Hapa tayali nimefanikiwa ,mimi ni mshindi “,Njoshi aliongea maneno haya huku akitokomea vichakani, lakini baada ya Njoshi kutoa mguu wake katika ngome ya malikia. Malikia alishtuka na kufuatiwa na majini wote, huku kila mmoja akiwa hajitambui. Hali hii ilimfanya Malikia kutoka nje, na kushangazwa kutomkuta Njoshi katika mti wa mateso, aliporudi ndani alishangaa kukuta kabati likiwa wazi huku fimbo ikiwa imeibiwa. Akiwa na mshangao na kushangaa namna Njoshi aliweza kufungua kabati, na ngome yote wasiweze kusikia hakupata jibu sahii. Harakaharaka aliwaita majini wote na kutoa amli Njoshi aweze kutafutwa haraka sana.
Ikulu kwa mfalme Mutapa;
Hofu juu ya mfalme kutofufuka tena inaikumba familia ya mfalme Mutapa, kwani mganga kutoka Muyeshi alifika na kueleza kila kitu ambacho alikigundua kutokana na uwezo aliokuwa nao.
“Haraka sana mama yake Njoshi auawe mala moja, baada ya hapo Ngesha na mama yake muwaue pia “,mtoto mkubwa wa mfalme, mtoto aliyeonekana kuwa katili sana, alitoa amli kwa askari wake na bila kupoteza muda askari waliondoka kutekeleza amli. Hayo yote kipindi yanatokea, Grace alikuwa chumbani kwake akimuwaza mpenzi wake Njoshi, bila kufahamu kuwa tayali askari waliweza kutumwa na kaka yake wakamuue mama mkwe wake. Jambo ambalo angelipinga, kama angeshuhudia kipindi amli hiyo ikitolewa.
Mwamutapa;
Siku zote misemo ya wahenga huwa inamaanisha kitu fulani,kama vile msemo maarufu unaosema ‘siku ya kufa nyani miti yote hutereza ‘
Msemo huu ulidhihirishwa kwa mama yake Njoshi, kwani siku hiyo aliahirisha kwenda shamba aweze kumsubili mwanae ,kwani ilikua ni siku ambayo Njoshi alitakiwa arudi kutoka msituni.Lakini pia siku hiyo mama yake Njoshi alisahau kutazama kioo cha ajabu ,kioo ambacho kilikua katika chumba maalumu katika nyumba kubwa waliyonayo.Siku zote kioo hicho alikitazama kila asubuhi anapoamka,na kufahamu jambo ambalo lingetokea siku hiyo.Hivyo basi  kama asingesahau kutazama kioo hicho cha ajabu,inawezekana angeepuka kifo.
********
Asubuhi na mapema siku ya jtano ,mama Ngesha aliamka na kuandaa chai ili waweze kuelekea shambani yeye na mwanae.Siku hii aliamka mapema tofauti na siku zingine,kwani alikosa usingizi mzima akiyatafakali maneno ambayo aliambiwa na mwanae usiku uliopita kuhusu kifo cha mfalme.Kifo ambacho kilikuwa siri,huku mfalme akiugua kwa takribani mwezi mzima,wananchi wakiwa hawafahamu.
“Amka unywe chai twende shamba”,mama Ngesha alimwamusha mwanae aliyeonekana kulala sana siku hiyo ,tofauti na siku zote.
“Mama naumwa sana,leo tusiende shamba,baki nyumbani,ukiniacha utakuta nimekufa”,Ngesha aliongea maneno yaliyomfanya mama yake asitishe kwenda shambani siku hiyo amuuguze mwanae,kwani alionekana kuchemka sana ,pale mama yake alimpomshika katika shingo lake na kulihisi joto kali la mwane likiwa limepanda sana,na kusababisha Ngesha atokwe na jasho mwilini.
“Sawa tutabaki wote,vua shati lako joto lipungue mwilini, ukihitaji chochote niite, mimi niko nje napukuchua mahindi “,mama yake Ngesha alimtoa hofu mwanae, na kisha kutoka ndani ya chumba cha mwanae. Bila kutambua kuwa kifo kilikua mbele yao.
Ilikujua hatma ya Njoshi, na mama yake, pia hatma ya Ngesha na mama yake, usikose sehemu ya 14.