MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI - SIMULLIZI : MIMI NI MUAFRIKA ……SEHEMU YA 11…

JIFUNZE KISWAHILI

Full Version: SIMULLIZI : MIMI NI MUAFRIKA ……SEHEMU YA 11…
You're currently viewing a stripped down version of our content. View the full version with proper formatting.
…SEHEMU YA 11…
Msitu wa mikoko;
Mpuzu Yahimana aliongoza mashambulizi,waliwashambulia kwa mishale askari wa kikoloni, walipojaribu kuwasaidia wenzao waliojeruhiwa na mitego iliyotegwa na Waafrika, askari wa kikoloni hawakutambua mahali adui zao walipojificha, ilibidi wakimbilie vichakani, kila mtu njia yake, kuziokoa nafsi zao …
“,Tushukeni chini, tuwafuate porini, wengine wakusanye bunduki za maadui tuliowaua,tuzihifadhi mahali salama,maana vita haiishi leo wala kesho……”,Mpuzu aliongea, wote wakakubaliana naye,wakateremka juu ya miti, askari takribani therathini, akiwemo Angel Richald pamoja na Mwamvua.
“,Tufanye haraka, maadui bila Shaka na wao wanatutafuta, “Mwamvua aliongea.
“,Kweli kabisa, kweli kabisa, tufanye haraka! “,mzee Nyamigo aliongea kwa mkazo, akitikisa kichwa,akashika tawi la mti, akaning’inia kama nyani, akaruka chini…
dakika tatu zilitumika,kundi moja la askari lilikuwa chini, wakaanza kuokota silaha,kutoka kwa Wazungu waliouawa baada ya kutumbukia shimoni, huku wengine wakishambuliwa na mishale,waliendelea kukusanya bunduki, wakawasachi mifukoni, wakawanyanganya mabomu waliyokuwa wameweka katika mifuko yao, Mpuzu alikuwa bize akiangalia kila kona ya msitu, akichunguza usalama, wenzake wakiwa wanakusanya silaha kutoka kwa wazungu waliopoteza maisha.
…………………………………
Kundi la pili la Waafrika, kundi ambalo liliongozwa na Ishimwe, walimaliza kushambulia, waliua askari wa kizungu wengi sana, zaidi ya hamsini, huku kiongozi wao wa kizungu, jenerali Agustino Darwin akiuawa vibaya na gogo ambalo lilitegwa na kumpiga tumboni.
“,Leo kapatikana, roho yake mbaya, imesababisha afe kifo kibaya, ona sasa …!”,Ishimwe aliongea,akiwa pamoja na kundi lake la askari therathini, wakiutazama mwili wa kamanda wa kikoloni, jenerali mkatili ambaye aliwachukia sana Waafrika.
“,Puuuu, puuuu … “,..
“,Muache,ameshakufa! “,
“,Wacha nimtie adabu! “,
“,Achana naye,tayali ameshakua mzoga ……”,.
“,Pumbafu sanaa, ngozi nyekundu kama nyanya, harafu unajifanya mjanja, leo umepatikana! “,
Mpuzu alimshika kijana mwenzake, aliyekuwa na hasira kupita kiasi, licha ya Agustino Darwin kupigwa na gogo tumboni,akakata roho, lakini kijana huyu alikuwa bado ana hasira naye, alimpiga ngumi tumboni, akimtukana matusi ya kila aina, alichoshwa na ukatili wa jenerali huyu aliokuwa akiwafanyia.
“,Wengine okoteni silaha tuondoke, watatushambulia,wameingia vichakani,…”,
“,tushamaliza, ”
“,kama mmemaliza, turudini nyuma tukaonane na wenzetu! “,
“,Sawa, sawa …”,
Walimaliza kuokota bunduki za wazungu, wakarudi nyuma,kuonana na wenzao, kundi la Mpuzu.Macho yao yaliangaza mita hamsini mbele, hamsini nyuma, kulia na kushoto, walikuwa makini wasije wakashambuliwa na askari wa kikoloni waliokimbilia vichakani, walipo washambulia awali na kuwazidi nguvu.
…………………………………
Makundi yote mawili, makundi ya askari wa Kiafrika, yalikutana pamoja, wakiwa na machale, walijadiriana namna ya kuendeleza mapambano dhidi ya wazungu,ili kupigania uhuru wao …
“,Wameingia vichakani, tuwafuate! “,
“,Hapana, huko sio salama, tutakufa! “,
“,Kweli, mahali salama kwa mashambulizi, ni juu ya miti, turudini huko, wakija maeneo haya tuwashambulie !”,
“,Wazo zuri, tufanye hivyo! “!
“,Jamani, sikieni, hamsikii sauti za miguu, kuna watu wanakuja …”,
“,Harry up, let’s go back, tupande juu ya miti …”,
“,Hata mimi nasikia,wanakuja! “,
Kundi lote la takribani askari sabini, walipanda tena juu ya miti,baada ya kijana mmoja wa Kiafrika kusogeza sikio lake juu ya ardhi, karibu na udongo, akasikia ardhi ikitetemeka kwa mbali, bila shaka kuna watu walikuwa njiani wanakuja, tena wakikimbia, Angel Richald, mpenzi wake Mpuzu, mtoto wa gavana Richald Robeni, hata yeye alikuwa akichezwa na machale, akawahimiza wenzake, wakapanda juu ya miti haraka sana, ndani ya sekunde kumi, wote walikuwa juu ya miti, mikononi walishika upinde na mishale, huku bunduki walizowanyanganya wazungu wakiwa wamezikusanya pamoja, na kuziweka mahali salama juu ya mti, Angel alichukua bunduki moja aina ya smg, pamoja na baadhi ya mabomu madogo takribani matano, silaha zote za kizungu alijua namna ya kuzitumia, mafunzo aliyoyapata katika jeshi la Uingereza, aje kurithi mikoba ya baba yake, miaka kumi ijayo.
“,Shiii, silence please, they are coming, wanakuja! “,
“,Yeah wanakuja,kaeni tayali kwa ajili ya kushambulia,”
“,Sawa, sawa. …”,
Angel Richald, aliwasisitiza wenzake kuwa makini, kujiandaa kwa ajili ya mashambulizi, bunduki yake aliishikilia ipasavyo, jicho lake la kushoto alikuwa amelifumba, jicho lake la kulia lilitazama darubini, na kumuweka adui kwenye targeti, huku kidole kimoja cha mkono wake, kikijiandaa kwa ajili ya kuvuta taiga ili kuruhusu risasi kumiminika na kuteketeza maadui.
…………………………………
Malikia Magreth alikuwa mbele, mume wake, gavana Richald Robeni alifuatia, kisha kundi la askari wa kikoloni wakafuata, nyuma ya gavana Richald Robeni.Msururu ulikuwa mrefu, kutokana na wingi wao, wote walikimbia kwa kufuata njia ndogo, nyembamba, iliyokuwa ikiingia katikati mwa msitu, upande wa kulia.
“,What!, they have killed him, wamemuua Darwin! “,
“,Wamemuua kwa mtego,shit! Africans are bastard, we will kill you too, tutawaua ……”,
Wakiwa wanakimbia, ghafla mama yake Angel, malikia Magreth alifunga breki, alikutana na mwili wa kiongozi wao wa jeshi, walipoangaza upande wa pili, askari wengi wa kikoloni walikuwa wamepoteza maisha, wakavua kofia zao, jasho jembamba likawatoka, walichoka,
“,Who are you, wewe ni nani? “,
“,Colonial soldiers, askari wa kikoloni, don’t shoot us, msitushambulie …”,
Ghafla, malikia Magreth machale yalimcheza, alihisi majani ya vichaka yakicheza cheza, akanyosha bastola yake vichakani, kundi lote la askari wa kikoloni wakanyosha silaha zao kuelekea sehemu hiyo ya vichaka, askari takribani ishirini, askari wenzao wakajitokeza, huku wakionekana kuchoka sana.
“,Tulishambuliwa, wengine wakauawa, hatujui maadui walitokea upande gani, tumetoka vichakani kuwatafuta hatujawaona, ”
“,Tuondokeni, tusonge mbele …”,
“,But why this!, kwanini silaha zao hazipo mahali hapa?…”,
“,Enemies have taken them, maadui watakua wamechukua silaha zao, they want to fight us with guns, wanataka watuue kwa bunduki, they can’t kill us , tuondoke …”,
Walimaliza kujibizana wakiwa na huzuni, wakavaa kofia zao, wakakamata bunduki zao, wakaanza kusonga mbele, kufuata barabara.Macho yao yalikuwa makini, kuangaza kila kona wasije wakashambuliwa, mioyo yao ilianza kujawa na uoga, tofauti na awali, kwa sasa Waafrika walikua hatari sana, wenye mioyo ya ukatili kwa askari yoyote yule wa kikoloni, walikuwa hawana budi kuwa makini, kuepuka kifo.Walikimbia mita chache tu, baada ya dakika tano tu, wakashtuka tena ghafla, walikutana na maiti nyingine za wenzao waliouawa kikatili, ishirini ndani ya shimo, wakiwa wamechomwa na mapanga sehemu mbalimbali, baada kunaswa na mtego wa shimo, wengine walipigwa na mishale …
“,Shit! We are finished, wametega mitego kila kona, we have to be careful …”,
“,Why,hizi people nyeusi imekuwa katili sana, kama pata him or her, we are going to eat them, lazima kula nyama zao! “,
Walifoka, kila mmoja aliongea neno lake, gavana Richald Robeni pamoja na mke wake walishika vichwa vyao kwa huzuni, askari wao walikuwa wameuawa kikatili, wakaanza kuondoka tena, malikia Magreth, mke wake gavana, aliwaza tu kuhusu usalama wa mwanae, alitaka kufanya kila njia, asije akauawa na jeshi la kikoloni, kwani walikuwa na hasira sana baada ya wenzao kuuawa.
“,Lets move on, tusonge mbele …”,
“,Yes boss, let’s go to look for this stupid race, …”,
Gavana Richald Robeni alilihimiza jeshi lake kutokukata tamaa, mke wake akasimama, akaanza kusonga mbele, gavana akafuatia, kisha kundi lote la askari wa kikoloni wakafuata kwa nyuma,dakika mbili zilipita, dakika tatu zikapita,walikuwa njiani wakikimbia kusonga mbele
“,Paaaaa! “,
“,I’ m…dying, nakufa…aa ……”,
“,My mother!, mamaaa!, don’t die,aim sorry mom…”,
Ghafla risasi ilisikika, ikapenya katika kichwa cha malikia Magreth, ubongo wake ukasambaratika, Angel Richald ndiye aliyekuwa ameshika bunduki, akiwa juu ya mti, alifyatua risasi bila kujua kuwa kiongozi wa kundi, alikuwa ni mwanamke, tena mama yake mzazi, ukelele wa uchungu ukasikika, akakata roho palepale, Angel alipiga kelele za huzuni bila kutegemea,hakutegemea kumuua mama yake,mikono yake ilikufa ganzi, mwili ukakosa nguvu, akaachia bunduki yake aina ya smg, ikadondoka chini, askari wa kikoloni walipandwa na hasira, akiwemo baba yake mzazi na Angel, gavana Richald Robeni, hakutegemea kama mwanae alikuwa msaliti kiasi kile, akamuua mpaka mama yake mzazi, jeshi lote la kikoloni walisikia kelele za Angel, wakatambua mahali risasi ilipotekea ,waliinua silaha zao juu kwa pamoja, kushambulia mti mkubwa ambao Angel pamoja na askari wengine wa Kiafrika walikuwa wamejificha …
…ITAENDELEA …
Je, nini kitaendelea? Angel, msichana mrembo aliyejiunga na Waafrika kuwasaidia kupigania uhuru wao, kamuua mama yake bila kutegemea, mama yake akiwa msitari wa mbele kuingia msituni ili adhibiti askari wa kikoloni wasimuue mwanae, usikose sehemu ijayo, R. I.P Queen Magreth …