MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI - SIMULLIZI : MIMI NI MUAFRIKA ……SEHEMU YA 13…

JIFUNZE KISWAHILI

Full Version: SIMULLIZI : MIMI NI MUAFRIKA ……SEHEMU YA 13…
You're currently viewing a stripped down version of our content. View the full version with proper formatting.
…SEHEMU YA 13…
The great fort (ngome kubwa)
Gavana Richald Robeni alikuwa ameketi katika sebure yake, ndani ya kasri lake kubwa la kifahari, uso wake ulikuwa na huzuni,alikuwa amepoteza watu muhimu katika maisha yake, mke wake alipoteza maisha mbele ya macho yake,baada ya kupigwa risasi na Angel, mtoto wao kipenzi ambaye kwa sasa alikuwa ni adui wake mkubwa.
“,Africans must pay!, lazima walipe kifo cha mke wangu, nitamuua Angel kwa mikono yangu mwenyewe ……”,Richald Robeni aliongea,akiwa amejipumzisha, mara baada ya kumzika mke wake, alichukua simu yake kubwa ya mkonga, akapiga simu.
“,Hallow! “,upande wa pili wa simu ulijibu.
“,Aim Richald Roben, gavana ya Goshani, i need your help, nyie kama jirani yangu, mimi huku pigana na Africans, zimeua askari yangu nyingi sana pamoja na mke yangu,nahitaji msaada yenu, one hundred soldiers inatosha sana …”,gavana aliomba msaada kwa majirani zake,kisiwa cha Gano kilichopatikana bahari ya hindi, kisiwa cha waswahili ambacho kiliongozwa na wakoloni wa kichina.
“,Oooh,pole sana,wewe rafiki yangu sana, kila siku unaniuzia pembe za ndovu na mkonge, lazima nikusaidie, nusu saa ijayo jeshi langu litafika katika koloni lako……”,gavana wa kisiwa cha Gano aliyejulikana kwa jina la Hwang Lee aliongea,kisha akakata simu.
Angalau gavana Richald Robeni aliweza kupata faraja, akatabasamu kwa mara nyingine tena, tabasamu ambalo lilificha siri nyingi za uchungu na majonzi.Nusu saa ijayo alitegemea kupokea askari wa kichina mia moja, watakao muongezea nguvu kwenye vita dhidi ya waafrika ambao walitaka uhuru wao,jambo ambalo lilikuwa ni gumu kama samaki kuishi nchi kavu.
…………………………………
Angel Richald, mtoto wa gavana, aliamua kusahau kila kitu kilichokuwa kimetokea, alikuwa amejitoa kwa moyo mmoja kumsaidia mpenzi wake Mpuzu pamoja na jeshi lake, waweze kupata ushindi dhidi ya Waafrika.
“,Kila mtu ajaribu kulenga shabaha,mti ambao nimeuwekea jani la njano,hakikisha mkononi umeshika bunduki, kama ambayo ninayo mimi ……”,Angel aliongea, akanyoosha juu bunduki yake ya smg kila mmoja akaiona,kisha akaikamata vizuri,aweze kuendelea na somo lake.
“,Hii inaitwa magazini,hii ni taiga,hii ni darubini yako,pakia magazini, shika kwa nguvu bunduki yako,hakikisha umeibana kwa nguvu kwenye kwapa lako,kisha tazama darubini,mlenge adui yako,then vuta taiga,shoot him,mpige adui!”,Angel Richald aliendelea kutoa mafunzo yake kwa vitendo,baada ya kutoa maelezo marefu, alikaa vizuri, akafanya kama alivyowaelekeza, wote wakiwa wanamtazama, akavuta taiga na kuruhusu risasi.
“,Paaaaa, paaaa, paaaaa! “,alifyatua risasi tatu, akausambaratisha katikati mti mkubwa wa ubuyu uliokuwa umbali wa mita mia mbili, kutoka eneo la kulengea shabaha.
“,Is it clear?, mmenielewa vizuri? “,Angel aliuliza.
“,Ndiyo tumekuelewa! “,jeshi la waafrika liliitikia, jeshi ambalo lilibakiwa na askari arobaini tu,likiwa limechanganyikana na vijana, wazee wenye nguvu, mdogo wake Mpuzu aliyeitwa Mwamvua pamoja na Angel mwenyewe.
“,Kama mmenielewa ,ngoja tujaribu kufanya shambulio, fateni amri yangu …”,Catherine aliongea, akasimama vizuri, akajiandaa kutoa amri,akiwa mtaalamu pekee wa silaha za kizungu katika jeshi la Waafrika,alitambua kuwa silaha za jadi zisingewafikisha mbali katika vita.
“,Pakia magazini, ikoki bunduki yako,lenga shabaha ya adui wako kwa kutumia darubini,fireeee them, fyatua risasi ……”,Angel alitoa amri, kisha akaruhusu shambulio.
“,Paaaa, paaaa, paaaa, paaa………”,risasi zilisikika,jeshi la Waafrika lilifanya kama lilivyoelekezwa,walishambulia miti waliyoelekezwa, mahali kulipowekwa alama, miti yote ikapasuliwa, Angel akayaziba masikio yake, mlio ulisikika ulikuwa mkubwa, ukasindikizwa na sauti za mwangwi msituni.
“,Yeeeeeee, ngwaluna, gwaluna, “(tumeweza, tumeweza) “,walishangilia kwa furaha, wakitumia lugha yao ya asili, wakaluka kwa furaha kama masai wa kule Monduli mkoani Arusha, nchini Tanzania.
“,Haya sasa, that is over! suala hilo kwisha kabisaa, this is another thing, hiki ni kitu kingine tunapaswa kujifunza,ni rahisi kutumia, sio kama bunduki ……”,Angel aliongea, akachukua mabomu mawili aliyoyakuta katika moja ya maiti za askari wa kizungu, akawaonyesha juu.
“,What is this? “,Angel aliuliza kwa lugha ya kizungu, kwa muda sasa walikuwa wamekaa naye, alikuwa amefahamu maneno mengi ya kiswahili, wao pia walikuwa wamejifunza maneno mengi ya kizungu.
“,bomu! “,
“,Mlipuko, “,
“,Risasi! “,
“,kibuyu! “,
“,Hicho ni kibuyuu! “,
Kila mtu alitamka neno lake, watu wa mwanzoni walipatia, wengine wakakosea kidogo, lakini watu wawili wa mwisho walikosea na kutaja vitu vya ajabu, Angel akajikuta anacheka, kwa sasa alikuwa na furaha, alijiona mmoja kati ya waafrika, alianza kusahau kuhusu kifo cha mama yake aliyemuuwa kwa mikono yake mwenyewe.
“,Hili ni bomu dogo, linauwezo wa kuuwa watu takribani ishirini kwa wakati mmoja, hii hapa ni pini, ukiichomoa kwa kuivuta kisha ukawarushia maadui zako, utakua umemaliza kila kitu, litalipuka na kuwaua, ndio silaha pekee inayoua vibaya! “,Angel aliongea kwa kiswahili safi kilicho nyooka, alianza kuongea kiswahili kizuri cha wazawa,kama vile alikuwa amezaliwa Afrika mashariki.
“,Oneni kwa makini navyofanya!, “Angel aliongea tena, jeshi lake likawa makini kumsikiliza, kwa sasa walimuamini, wakaheshimu mawazo yake, Angel alichomoa pini, kisha akalitupa bomu mita mia moja katikati ya msitu.
“,Puuuu, puuuuu! “,mlipuko ulisikika, miti ilipasuliwa mingine ikadondoka chini, vumbi zito likatimka,waafrika wote wakabaki midomo wazi, walikuwa hawatambui nguvu za silaha za wazungu.
“,Chakula, chakula, muda wa chakula,iyeeeee! iyeeee!, muda wa chakula ……”,la mgambo lililia, mmoja kati ya vijana wenye nguvu alipiga kelele, akiwa ameongozana na wenzake sita, walilejea kutoka msituni kufuata chakula,walikuwa na mikungu mitano ya ndizi pamoja na maembe. Jeshi la waafrika wakaahirisha shughuli zao, mafunzo yao yalikuwa yamekamilika, wakaenda kuwapokea ndizi, ndizi zingine zikapelekwa juu ya mti mkubwa wa ubuyu, maficho ya waafrika wote, ndani ya mti huu kulikuwa na matawi pamoja na mapango ambayo yalitumika kama maficho wakati wote wa vita.
“,we have to be careful, tuwe makini kabisa, muda wowote watarudi, kama sio leo basi kesho asubuhi, “Angel aliongea, akatazama juu angani, yalikuwa ni majira ya jioni, jua lilikuwa limeanza kuzama.
“,Usjali mke wangu, muda wowote tuko tayali kupambana ,ulinzi uko salama kabisa…”,Mpuzu aliongea, akamuondoa shaka mpenzi wake wa kizungu aliyemfanya ajiamini na kuanzisha vita hii ya kupigania uhuru, kwa sasa alikuwa amekamatilia bunduki yake iliyojaa risasi.
“,Wifi usjali, nipo kwa ajili yako …”,Mwamvua, mdogo wake Mpuzu aliongea, akaikoki bunduki yake, akamuhakikishia usalama.
“,Hahaaa, lakini tuwe makini sana, wale ni askari wazoefu na wamepitia mafunzo mbalimbali ya kijeshi, kwahiyo wanatuzidi askari, silaha pamoja na udhoefu, cha muhimu ukiua, hakikisha silaha yake unaichukua ……”,Angel aliongea.
“,Usjali shemeji, mimi nipo kwa ajili ya ulinzi na kutoboa matumbo yao kwa mishale, kwa yoyote yule atakayeisogelea kambi yetu …”,Ishimwe rafiki yake Mpuzu aliongea, akiwa ameshika silaha zote mbili, bunduki pamoja na upinde wake, aliupenda sana, hakuwa tayali kuuacha.
“„Sawa nimewaelewa, “Angel aliongea,wakakumbatiana, kwa sasa walipendana sana.
…………………………………
Gavana Richald Robeni alishtuka, akanyenyuka sebureni kwake, akatoka nje, alikuwa amesikia sauti ya risasi, nje ya ngome yao, baada ya dakika tano, mlipuko wa bomu ukasikika, nje ya ngome yao, moshi mzito ukaanza kuelekea angani, aliuona vizuri sana…
“,What is that? (ile ni nini) “,aliuliza kwa kizungu.
“,ni mlipuko, pamoja na risasi kutoka katika msitu wa mikoko …”,mmoja kati ya askari wa kikoloni aliongea, gavana akatafakari, kisha akatikisa kichwa, alikumbuka jambo fulani, akatambua chanzo cha mlipuko huo.
“,Ndiyo maana askari wetu waliouawa hatujawakuta na bunduki yetu, bunduki yote imechukuliwa na African, but they won’t win this battle, hawatatushindaa! “,gavana alifoka kwa hasira, kisha akarudi zake ndani, akijiandaa kwa vita siku inayofuata.
…ITAENDELEA …