MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI - SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 34

JIFUNZE KISWAHILI

Full Version: SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 34
You're currently viewing a stripped down version of our content. View the full version with proper formatting.
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU 
SEHEMU YA 34
Basi kama kawaida yake Zamda siyo mtu wa kujikweza sana.Aliamua kufungua kioo na Kisha akafunga mlango na Kuanza Kutoka Kwenye Gari Hilo lililokuwa ni gari aina Discover 3
Kwahiyo Zamda akiwa amevaa dera lake lililokuwa limemkaa Kweli Kweli kutokana pia na mwili wake namna ulivyo kichwani kajifunga kitambaa cha kuonesha ustara wake.Lakini  Zamda akawa amemwambia yule mfanyakazi wake ambaye alikuwa na watoto wa Zamda  ambapo yule mfanyakazi anaitwa Hilda.Zamda akamwambia Hilda Hivi.
Hilda usishuke na watoto,
Sawasawa mama.
Kaa nao hapo Hapo.
Sawasawa mama.
Tulia kwanza Mimi niongee na huyu mtu .
Sawasawa mama.
Nakweli Hilda akawa amekaa na wale Watoto wa Zamda Yaani Glady,Rubai na Gift ambapo Gift ndiyo yule mtoto wa pili wa Zamda.
Zamda Alishuka na kwenda kwa Huyo mtu huku akiwa anaangalia sura ya mtu huyo kwakuivutia kumbukumbu za mbali kabisaaaaaaa.Alifika kisha Zamda akamsalimia Mwanadada huyo kwakusema Hivi.
Mambo vipi Dada?.
Safi.Zamda ni wewe kabisaaaaaaa.
Ndiyo, ila mbona Mimi sikukumbuki vizuri?.
Daaa Kwakweli Zamda huwezikunikumbuka Kwasababu mwili wangu wa kipindi hicho siyo kama huu nilionao kabisaaaaaaa. Yaaani nimekuwa kama Mtoto.
Hapana. Ila ni vyema ukaniambia jina lako kwanza Ndiyo hata naweza kukukumbuka vizuri.
Mimi ni rafiki yako tulisomaga shule ya sekondary ya Ngata.
Ngata!!!??.
Ndiyo.Mimi ni Kidawa.
"Zamda alishangaa sana kwakusema"Haaaaaaaa.Kidawa ni Kweli kabisaaaaaaa ni Wewe.
Kweli ni Mimi.
" Walikumbatiana kweli kweli Zamda na Kidawa Kwasababu Kipindi hicho walikuwa ni marafiki wakubwa sana japokuwa waliwahi kugombana kidogo walipokuwa shule sekondary ya Ngata wakiwa na shoga yao mkubwa mwingine ambaye ni Mwantumu .Kwakweli hadi machozi yaliwatoka wote. Kisha Zamda akaendelea kusema hivi ".
Kidawa siamini kama ni wewe kabisaaaaaaa. Mbona umeisha Hivyo Jamani Yaani umekuwa  kama mtoto Yaani sijui Ana miaka Kumi na Tano.
Zamda Yaani ni maisha tu shoga wangu.
Kwahiyo Ngata uliondokaga kitambo sana?.
Ndiyo mda Sana tena sana .
Daaaa Sasa hapa mjini Kidawa unajishughulisha na nini?.
Ndiyo Kama unavyoona hili beseni hapa ni la kwangu nauza matunda.
Daaaaaaa Kidawa kweli kweli kabisaaaaaaa?.!
Ni kweli.
Vipi kuhusiana na yule rafiki yetu mwingine yuleeeee.
Unamzungumzia Mwantumu siyo?.
Duuuuuuuuuuuu, kwa Mwantumu Kwakweli.
Kwani yuko wapi Yeye ?.
Aaaaa Kwakweli Zamda kuhusiana na Mwantumu ni Stori ndefu Sana.
Kivipi iwe stori ndefu Tena.
AAA kwa ujumla Mwantumu si Mwantumu tena kwasasa.
Bali ni nani.
Ni marehemu.
" Zamda alishtuka sana Kwakweli kwakuweza kusikia maneno Yale ya Kidawa kuhusiana na Mwantumu. Kisha Zamda akasema Hivi'.Marehemu!!!???.
Ndiyo maana Yake Zamda, Mwantumu alishafariki kitambo sana.
Kweli kabisaaaaaaa.
Ndiyo Ukweli huo kuhusiana na Mwantumu.
Amakweli udongo haushibi.
Na haushibi kweli.
Sasa nini kilisababisha hadi kifo chake?.
Alikuwa anaumwa sana.
Anaumwa sana.
Ndiyo.Yaani aliumwa sana kipindi kile ulivyopotea tu pale mtaani kwetu na Yeye akawa ameanza kuumwa.
Nini haswaa kilikuwa kinamsumbua.
Daaaaaaa, ni ugonjwa mkubwa Sana.
Ugonjwa mkubwa kivipi Kidawa?.
Ni huu Ugonjwa wa kisasa.
Ugonjwa wa kisasa!!??.
Ndiyo.
Ni ugonjwa gani huo wa kisasa?
UKIMWI.
"Zamda akawa ameshituka na kusema hivi"UKIMWI kabisaaaaaaa.
Ndiyo maana Yake Zamda.
Daaa mungu msaidie rafiki yangu Kwakweli huko aliko.Kwahiyo Kidawa Sasa unaishi wapi kwasasa?.
Huko mwisho wa jiji kabisaaaaaaa hukooo.
Mwisho wa jiji Unamaanisha Horima kabisaaaaaaa kule.
Ndiyo.
Haaaaa mbona mbali sana Sasa kule unakuja na nini hadi huku?.
Kwa miguu tu.
Haaaaa kwa miguu kabisaaaaaaa.
Ndiyo Zamda Sasa nitafanyaje.Kwasababu niseme nipande gari nitamaliza Hela na unaweza kukuta Hayo matunda yasinunuliwe hata kidogo huko Kwenye gari.
Daaaaaaa sawa Shoga Wangu wa kitambo embu nipatie namba zako.
Sina hata simu kabisaaaaaaa .
Kabisaaaaaaa huna Simu Kidawa!!??.
Kweli Zamda sina  simu.
Duuuuuuuuuuuu Sasa tutakutanaje hapa Mjini kwa style hiyo.
Tutakuna tu Zamda.
Sawasawa. Embu shika Basi hii Hela Kidogo hii itakusaidia kwa mambo madogo madogo Hivi."Zamda alimpatia Kidawa shilingi laki moja ya Kinani. Kisha Kidawa akasema Hivi".
Shukrani sana Zamda, Yaani shukurani kubwa Sana.
Sawasawa haina shida.
Ubarikiwe sana Zamda.
Inshaallah.
Basi acha Mimi nirudi nimekuja hapa chapu.
sawasawa Zamda uzidi kubarikiwa sana.
Basi mda huo Zamda akawa amemuaga huo Kidawa na Kisha Zamda akawa amerudi zake huko kwenye gari lake.
Kwakweli Kidawa roho ilimuuma sana kwa kuweza kumuona Zamda akiwa anaendesha gari tena la bei ghali namna hiyo Kabisa.
Ni miaka kumi na tano imepita tangu Zamda na Zaidu kuoana.Yaani kuanza kuitana mke na mume.Kwakweli ndoa yao ilizidi kukoa moto sana na kuwa nzuri yenye utulivu mzuri kwelikweli kama utajiri wao amabo walikuwa nao.
Ambapo kwa Zaidu tayari naye aliweza kusoma hadi kuja kufanikisha kumaliza shahada yake ya Kwanza na ya pili yaani akawa ana masters yaani shahada ya udhamili ambayo ilikuwa ni shahada ya udhamili ya Fasihi katika chuo kikuu kilichokuwa kikijulikana kwa jina la University of Literature (U.L), yaani Chuo kikuu cha Fasihi ambacho kilikuwa kinapatikana hapo hapo katika jiji kuu la Kinani.
Zaidu kutokana na ustadi wake wa Fasihi aliweza kupewa nafasi katika chuo kikuu hicho cha Fasihi cha Kinani.Ambapo nafasi aliyokuwa amepewa ni nafasi ya Muhadhiri Msaidizi katika chuo kikuu cha Fasihi.
Heshima ya cheo hicho  alipewa ni baada ya kuweza kushinda tunzo takribani Saba katika mashindano mbalimbai ya kitaaluma. Ukianza na mashindano ambayo makubwa kabisa aliyafanya na kushinda tuzo ya dunia ya uandishi wa hadithi za kufikirika na zisizo za kufikirika.
   Kwahiyo Bibiye Zamda hadi kipindi hicho alifanikisha kuwa na Watoto wanne.Watoto hao ambao ni Glady akiwa ndiyo wa kwanza kutoka kwa marehemu Tito na wa pili ni huyo Gift ambaye ni wa marehemu Tito pia,mtoto wa tatu ambaye ni Rubai na Ndiyo Mtoto wa kwanza kwa Kijana Zaidu na wa nne na wa mwisho ni Aisha. Kwahiyo Zaidu kwa watoto wake kabisa akawa  anao wawili wakike na wa kiume.
Lakini Kwakweli Watoto wote aliishi nao na kuonesha moyo mzuri kwao kama vile wote ni wa kwake.Huyo Glady na Gift wote waliona kabisaa Zaidu Ndiyo Baba yao.Wote aliwapeleka Katika shule zenye kufundisha vizuri  sana na zenye rekodi nzuri sana  za ufaulu katika Taifa la Kinani.
Basi ikiwa siku hiyo ikiwa ni Siku ya jumapili mishale ya saa nane mchana. Siku hiyo Jeni alihudhuria katika chakula cha mchana huko Nyumbani kwa Zaidu. Kipindi hicho tayari Zamda ukimuangalia siyo yule Kabisa. Yaani mwili umekuwa mkubwa Kweli Kweli na kuzidi kuonesha sura ya kiutuukubwa Zaidi.Zaidu naye ndiyo hivyo mzee wa Nyumba naye kama kawaida amejaaliwa mwili ambao si wa kuzeeka baki kwa namna ndefu na mstachi unavyoonekana tayari utajua kwamba huyu mtu ni mkubwa kiumri.Jeni Naye kama kawaida yake aliweza kung'ang'ania mjini tu.Yote hiyo ni baada ya mchumba wake ambaye alikuwa ni polisi alikuja kufariki ni baada ya siku hiyo mchumba wake alikuwa ameenda katika malindo yake huko Walikuwa na polisi wenzake wengine.Ambapo walikutana na Kikundi kibaya sana Yaani kilikuwa na nguvu sana na kuweza kuuliwa askari watatu mojawapo akiwa ni mchumba wa Jeni na wengine wakawa wamefanikiwa kukimbia ndipo wakaenda kutoa taarifa huko kazini kwao.
Kwahiyo kwa siku hiyo Kwakweli ilikiwa ni siku maalumu sana kwa wakutani hap watatu Yaani Zamda, Zaidu na Jeni.Wakiwa wamekaa katika Jumba la kifahari la Zaidu.
Mda huo wakiwa katika kila mtu na kiti chake meza hapo inaonekana ina chakula cha kutosha Kabisa na matunda ya aina mbalimbali. Basi mda huo Zaidu akiwa amevaa suruali yake ya bluu Hivi na tisheti nyeusi, Zamda kama kawaida yake Bibiye wa madera,Mda huo akiwa amevaa dera lililokuwa na rangi nyekundu na njano na liliyokuwa limechorwachorwa maua ya love.Jeni naye suruali nyeusi na tisheti nyekundu. Basi mda huo Zaidu akiwa ameshika kikombe akinywa juice huku akisema Hivi.
Unajua Jeni Natumai kwasasa ni miaka kama vile Kumi na Tano hivi Tangu Mimi na Zamda ambaye Ndiye mke wangu kuoana.
Ndiyo ndiyo Zaidu.
Aaaaaaa Zamda mke Wangu.
"Zamda aliitika kwa madaha Kweli Kweli huku akiwa na Glass iliyokuwa na juice tele.Alisema Hivi".Beee mume Wangu.
Najua Unajua kabisaaaaaaa kwamba Jeni ndiyo chanzo cha sisi hadi kuitana hapa mke na mume.
Ni kweli mume wangu hilo nalijua sana tena sana.Ndiyo maana huwa Nasema Jamani Jeni umenifungulia vizuri sana njia ya maisha yangu.Kwahiyo nipende kusema tu shukurani sana sina hata kingine cha kukulipa.
Aaaaaa shukurani pia kwako wewe kwkaunifanya na Mimi hadi kuwa hapa.
Sawasawa.
" Zaidu akasema Hivi ".Kwakweli Jeni Mimi ni shukurani aisseeee Sijui nikupatie Shukrani ngapi Jamani. Kwasababu ni mengi ambayo umenifanyia kwaajili ya faida yangu.
Sawasawa Zaidu. Pia Zaidu hata Mimi Kwakweli niseme tu Kwakweli ni shukurani nyingi sana za kukupa wewe Kwasababu kwa wewe ndiye  kama mtu ambaye unaniweka mjini na hadi mda huu Mimi kuitwa eti Boss wa salon zote ziitwazo Jeni Hair Salon hapa mjini. Unajua siamini kabisaaaaaaa.
Aaaaa unajua Jeni niseme tu kwamba sisi wote katika msafara huu hadi leo hii tuko hapa kila mtu hapa ana msaada wake mkubwa sana kwa mwenzake.
" Zamda akasema Hivi "Ni Kweli mume wangu.Kwasababu maisha yetu yalikuwa ni ya kama duara vile.Yaani huyu kamsaidia yule na yule kamsaidia Huyu Basi Yaani ni full misaada tu kabisaaaaaaa.
Ni Kweli mke wangu.
Basi wote mda huo  Kwakweli Walikuwa na Furaha sana kwa marafiki hao watatu ambao kwamba kila mtu anaonekana Kweli amemsaidia mwenzake kwa namna yoyote ile Au njia yoyote ile.
Hapa Sasa ndiyo pale pakujua kwamba saa nyingine katika Maisha Kwakweli unaweza kulia sana Ukisema kwamba maisha ni magumu sana na unaanza kuamua kukata tamaa na kutokana na hali uliyo nayo.Hapana si vyema kukata tamaa angali u mzima.Yaani roho ikiwa bado inadunda kamwe haifai kukata tamaa Kabisaaaaaaa.
Kuna mda machozi yatakutoka sana hadi mda mwingine unatokwa na macho ya damu Lakini bado tu hakuna kukata yamaaa.
Tukumbuke tu maisha ni Safari ndefu ambayo Kwakweli Safari hiyo huwa na Vituo vingi  sana.
TAMATI
MWISHO.
FACEBOOK PAGE: saidikaitastories.com
LINK:https://www.facebook.com/kaitastory/
MAWASILIANO: 0783372139
E-MAILConfusedaidikaita7@gmail.co