MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI - SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 05

JIFUNZE KISWAHILI

Full Version: SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 05
You're currently viewing a stripped down version of our content. View the full version with proper formatting.
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU           
SEHEMU YA 05
Basi baada ya mda kidogo kweli Tito akawa ameshawasili nyumbani kwa akina Mpenzi wake ambaye ni Zamda.Lakini hadi anafika pale haelewi hili wala lile litakalomkumba.Kwasababu Kwanza Furaha imemuijia pale anapoambiwa kwamba Wazazi  pamoja na wadogo zake na kaka wote wametoka Kwahiyo ni nafasi kubwa Kabisa kwake ili kesho aweze kuondoka na furaha kubwa akikenua hadi jino la mwisho lionekane.
    Lakini japokuwa Kweli Tito anapokuja Kulala na Zamda akiwa na furaha Lakini kwa Zamda Kwakweli Roho ikawa inamuuma sana Kwamba amemchongea kwa mzee wake kwa kumdanganya kwamba wametoka.Ni jambo ambalo analifikiria sana ila ndiyo hivyo Hana namna ya kufanya na la sivyo Baba Zamda alishasema kwamba akikataa atafanya juu chini hadi amshike na kumpeleka jela.Kwasababu bado Zamda anajulikana ni kama mwanafunzi.
    Tito anapowasili pale nyumbani na anakutakana na Zamda akiwa amekaa hapo mlangoni akiwa anamsubiri kwa hamu kweli kweli. Basi baada ya kufika Pale kidogo wakawa na maongezi kwa hapo nje kidogo.
   'Zamda anaongea huku amemshika Tito bega la Mkono wa kushoto huku akisema hivi ".Daaaa Mpenzi wangu umekumbuka hii njia nilikueleekezaga kama siku moja hivi tu.
Ndiyo naikumbuka vizuri. Weeeee chezea nafasi hii leo tuliyoipata Yaaani hakuna kulipia chochote.
Basi tuingie ndani Kwasababu huku nje nako watu wanapitapita kila saa wakituona hapa itakuwa Hatari.
  Basi Nakweli Tito akawa amekubali kuingia ndani na huku akiwa anajiamini kwamba huko ndani anakoingia hakuna kiumbe hata kimoja vitaonekana kesho na hawatomkuta labda wakute tu huyo mtoto wao hapo.
   Moja kwa moja wakawa wameingia hadi ndani na kisha wakawa wamekaa kwenye kochi ambalo Kwakweli ukilikalia halijulikani tena kama kochi Bali linakuwa ni kama kigoda tu ambacho kimewekewa kigodoro kidogo tu.Yote hiyo ni kutokana na uchakavu wa kochi Hilo namna ulivyo. Hiyo inaonesha haswaaaa namna umasikini ulivyokithiri Katika familia ya akina Zamda.Lakini kwa Tito hakuwaza kwamba kochi baya Au laaa na wala hakumuuliza Zamda bali ikabidi waendelee na Mambo mengine yaliyowakutanisha mda ule.
    Basi baada ya kukaa tayari maongezi yakawa yameanza hivi na huku kazi kidogo ya kuanza kutomasana ikaanza hapo hapo Bali hata kujali lolote lile.Mda huo Baba,na wengine wako. Chumba kingine wakiwa kimya kusikiliza nini kinaendelea.Kwahiyo tayari Tito akaanza tena Mambo yake akiwa anataka wafanye mautamu hapo hapo.Hivyo akaanza milainisho polepole kwa Zamda hadi na kweli Zamda akawa amejifanya kwamba tayari ameshalegea.Baada ya hapo kisha Tito akawa anasema Hivi.
  Sasa my situingie tu huko chumbani unakolala.
  "Zamda anajibu huku akiwa amelala chali kwenye kochi lile la amka tutandike huku akisema Hivi".Hapana my hapahapa. Kwani hapa kuna nini.kwanza hapa ndiyo kuna upepo huko chumbani kuna Joto sana siunajua hamna Umeme hapa tungewasha hata fen tu.Hapa Hapa bana inafaa.
Basi Sawa,ila
 ila nini my "Zamda akawa ameinuka na kumshika Tito Kwenye kichwa huku Mkono wa kulia akiwa anaupeleka kifuani mwa Tito huku mdomo akiwa anauelekeza mdomoni kwa Tito Yaani ili aweze kumpatia mate kidogo ili   kuweza kumlewesha tu.Kimya kikatokea kwa sekunde kadhaa."
  Lakini kwa Upande wa pili Mambo yanapoendelea hapo ndani kati ya Tito na Zamda huko nje tayari Baba,Mpundu wanajiandaa namna ya kuingia na kuweza kumshika vizuri huyo Tito. Basi mda huo Mambo ndiyo yamenoga kwelikweli huko ndani.Mama Zamda akawa ameambiwa kwamba asiongee chochote kabisa.Lakini baba yake Zamda huwa anasumbuliwa na kikohozi kikali sana na kikimwijia inatakikana akohoe mda huo huo ili aweze kuepusha madhara mengine kujitokeza baada ya kutokukohoa mda huo.
  Basi Baba Zamda kafika tu pale mlangoni kikozi kikali kikambana akajikuta Hana breki na kukohoa hapo hapo kwa mfululizo mara nne kwa Haraka Haraka. Huko ndani Sasa Tito akawa ameshituka na kusema Hivi.
Zamda mbona hiki kikohozi mbona kama kimekoholewa karibu hivi. Au ni mzee wako nini.?.
Sidhani kama watakuwa ni wenyewe mda bado wa kurudi.
Weeee Zamda hiki kikohozi kiko karibu kabisaaaaaaa Kwa huyu mtu ambaye amekohoa.
"Basi  baada ya sekunde chache tu baba Zamda akawa anafungua mlango.Kwasababu mlango ule Zamda aliuegesha kijanja tu kisha Tito anasikika akisema Hivi".
Jamani majirani mwiziiiiii,mwiziiiii "anasema Hivyo Kwasababu anajua Zamda kamuambia kwamba hamna watu kabisa. Baba Zamda akawa anasema Hivi"
   Shwaiiini weweeee tangia lini mtu akaiba Nyumba yake aliyoijenga Au alikopangisha.Yaani wewe ndiye tunayekutafuta kwa udi na uvumba.Kwasababu wewe Unataka kujifanya mkunga kwa kuwa na vidole virefu tu Wakati kuna vigezo hujakamilisha."Baba Zamda akawa  anachukua taa na kummlika Tito vizuri usoni ili aweze kuishika sura yake vizuri huku akiwa anasema hivi "Yaani mmeamua kuja kufanyia uchafu wenu hapa hapa mlivyokosa haya kabisaaaaaaa. Yaani Zamda kabisaaaaaaa.
Hapana Baba.
Hapana nini "Baba anaigiza kama anataka kumpiga  Zamda huku akisema".sasa hapo unachakujitetea?.Wajitetea nini Kwasababu siku nyingine Hivyo Hivyo unaenda huko eti kwa rafiki kumbe ndiyo huyu." Tito akajikuta ameropoka neno kwakusema ".
  Baba tusamehe.
  Kwanini Nisamehe washenzi nyiye.
Hatukujua ."Baba Zamda akamjibu kwa hasira kweli kweli akisema Hivi"
Yaani wewe ndiyo nakutafuta kwelikweli kama mtu aliyekuwa na nyama ya porini Yaani wewe lazimaaaaa ukanyeee ndoooo miaka thelathini jela.Unatoka na mwanafunzi. Ahaaaaaaa umejikoroga kwelikweli.
Sikujua kama ni mwanafunzi Jamani,sikujua kabisaaaaaaa Jamani."Tito maji yamemfika shingoni Kabisa na Hana namna hadi analia kilio cha Mbwa aliyepigwa kwa kuingia msikitini".
Sawasawa Sasa hivi ndiyo umeshajua tayari. Sasa hapa tu Kwa usalama wako na uwe na amani katika Maisha yako hiyu Zamda,Baba unaenda nae huko huko unakoishi.Kwanza unaitwa nani  Wewe?.
"Hakudanganya jina ikabidi aseme lenyewe kabisa kumbe  ndiyo kajiwekea minyaa machoni mwenywe.Akasema hivi".Naitwa Tito.
Lahaula wala kuwaata Yaani Zamda umepewa mimba na mkiristo kabisaaaaaaa. Mimi mzee wa msikiti watanionaje Jamani, uso wangu nitauficha wapi Jamani yarabi kosa gani hili kubwa nimekufanyia.Zamda kabisaaaaaaa mkiristo Yaani ukaona kabisaaaaaaa wakiristo ndiyo wana mapenzi ya dhati kuliko waislamu."Akarudia kumuuliza Tito Hivi".atiiiiii embu rudia umeniambia unaitwa naniii.
" Akiwa anasema kwa kuogopa".Tito.
 Sasa bana hapa hamna maelezo mengine kabisaaaaaaa na Mimi sitaki niaibike kabisaaaaaaa. Kwahiyo bwana Chakufanya ni hivi Tito na Zamda nyinyi mmeshakuwa ni watu wazima. Sasa  Basi Zamda chukua virago vyako Yaani matambara yako mfuate huyu wakuitwa Tito huko anakoishi.Sitaki maelezo mengine Hapa. Na hii kesi sitaki ifike mahakamani nataka iishe Sasa hivi kwa maamuzi niliyoyatoa.
ila baba samahani Mimi siyo mkazi wa Ngata.
Ohooooo, Hilo ndilo tetezi lako siyo.Yaani Nasema hata uwe unaishi nyuma ya dunia kwamba ndiyo mbali sana lazima uondoke tu na huyu Zamda. Kabisa sitaki sitaki masuala mengine Hapa. Wapi kwani unaishi unavyosema wewe huishi Ngata.
Naishi Kimbu.
Hhahahahahhaha, Yaani Kimbu ninayoijua Mimi.Wallah mwanangu kama ni jahanamu umejikokea moto mwenyewe. Yaani huko ambako watu wanalewa kwelikweli.Kwahiyo huku unaishi kwa nani?.
Nimepangisha tu Hapo Kati.Ila kesho ndiyo nilikuwa na mpango wa kuondoka
Ahaaaaaaaa mpango wa kuondoka ndiyo maana ukaja kumuaga vizuri alafu utuachie mzigo Hapa."Mda wote huo Mpundu hakuwa anaongea lolote.Kwakawaida yake siyo mtu ambaye ni mwongezi sana Bali ni mtekelezaji sana. Baada ya kuona Baba amezidisha maneno akaamua kusema hivi ".
Wewe Zamda Haraka kachukue begi lako la nguo na vitu vyako vingine msafara uanze Sasa hivi na huyu Jamaa yako."Kwa namna Zamda anavyomjua kaka yake ambaye ni Mpundu Haraka Haraka akainuka na kwenda kufungasha virago vyake ili Sasa Msafara wa kuondoka uanze. Mda huo Tito amekaa hapo kwenye kochi kichwa kakiinamisha chini mitihili ya mfiwa baba na mama kwa mkupuo mmoja.Kwahiyo baada ya mda kidogo tunaona Kweli Zamda anatoka na mabegi yake na kachukua mtandio wa kujifunika ili hata watu wakimuona huko mtaani wasijue ninani Huyu.Akaja na mizigo yake hapo kisha wakaanza kuwaaga wazee Lakini kwa mda huo mama Zamda alikuwa ameambiwa na baba Zamda kwamba asifungue mdomo hata kidogo mwanzo mwisho la sivyo talaka inamhusu ya Haraka Haraka.Baaada ya kuagana pale kisha baba Zamda akasema Hivi".
Safari njema muendako msijemkasema mnapata mabalaa huko muendako Kwasababu sijawapa Baraka. Kwaherini ila ndiyo ukubwa huo.
Mwendo wa Haraka Haraka waliondoka pale nyumbani na kuelekea sehemu alikopangisha Tito ili kwenda kupanga ni namna gani watafanya ili pakikucha waanze nanini na wamalize nanii.
Basi wakiwa tayari wameshafika katika chumba ambacho Tito amepangisha,mabegi yakawekwa hapo chini na Kisha wakawa wamekaa katika godoro.Kwasababu hapo ndani anakoishi Tito anagodoro tu Ambalo godoro Hilo ni la rafiki yake tu.Ambapo Mara nyingi Tito anapokuja kikazi katika mkoa wa Ngata huwa anamsaidia kumpatia godoro na kupangisha inakuwa ni gharama ya Tito.kulikoni kwenda Kulala Kwenye Nyumba za wageni ambazo ni Hela kubwa Kweli Kweli kwa siku nzima. Basi mda huo  wakawa wanamaongezi kama ifuatavyo.
"Mda huo Tito kakaa kwenye godoro akiwa karibu na Zamda.Tito kainamisha kichwa chini kama kondoo akiwa matembezini huku akikikuna kwelikweli .akawa anasema Hivi".Sasa Zamda nitaenda kumueleza mama nini Kuhusiana na huu msala ambao umeusababisha wewe?.
Tito siyo mda wakuanza kulalamishana hapa, Kwasababu Mimi nilikuwa naogopea Kwamba kilichokuwa kinafuatia  pale ni wewe kushikwa na kupelekwa jela miaka thelathini.Hujui kama umeokoka Kabisa katika hili janga?.Ungefungwa miaka thelathini.
Ni Sawa ila daaa na huko nako umeniweka machachani kabisaaaaaaa.
Yaani sikuelewi nimekuweka machachani kwamba huko Kimbu una mke mwingine au Kwasababu hata sikuelewi unachomaanisha.
Simaanishi Hivyo.
Bali wamaanisha Vipi.
Namaanisha kwamba huko mama ataenda kukinukisha kirambasi kwelikweli. Kwasababu anajua Kabisa nimemuaga bana Eeeee Mimi naenda Ngata kikazi kwa miezi  kadhaa Lakini kazi yenyewe na mshahara sijui ndiyo huu nampelekea.
Kwahiyo unachotaka wewe ni nini kifanyike?.
Yaishe tu Zamda.
Sawasawa Eeeee yaishe.
Kwahiyo Zamda kabisaaaaaaa umekubali kwenda kimbu na Mimi ?!..
Sasa wewe swali gani waniuliza Hilo.Naenda na wewe unafikiri nitaenda wapi Sasa.Niende jela kwani mimi nimejiwekea mimba mwenyewe?.
Haya Basi tulale ili tusubiri pakuche na tujue nini kitaanzwa.
Hayaa tulale.
Kwakweli kwa usiku wa siku ile Zamda na Tito hakuna hata ambaye alikuwa na hamu yoyote ile kwa mwili wa mwenzake bali walilala mithili ya watu wako msibani.