MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI - SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 03

JIFUNZE KISWAHILI

Full Version: SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 03
You're currently viewing a stripped down version of our content. View the full version with proper formatting.
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU           
SEHEMU YA  03
Kidawa naye akiwa amevaa kisketi kilichoishia mapajani cha rangi nyekundu juu juu kama vile mzungu.Miwani kaivaa na nywele zake za kuazima zilizoshuka hadi mgongoni Basi ndiyo alizidi kuonekana kama vile mzungu.Kwa umbo lake Kwakweli nalo si haba kwa namna alivyokuwa amevalia.
Baada ya kufika sehemu ile aliyokuwa amekaa Zamda na kweli wakawa wamemkuta ni Zamda Kweli."Wakawa wamesimama kwa kumzunguka Zamda .Nakweli Zamda Anaonekana yuko kakaa na jamaa hapo meza imejaa vinywaji kedekede.Jamaa aliyekaa naye hakuwa mkubwa sana Bali anavyoonekana ni kama vile Ana umri wa miaka ishirini na mbili Hivi. Baada ya Zamda kuwaona Kidawa na Mwantumu wamemzingira akawambia Hivi ".
Karibuni mezani." Kisha Kidawa akasema Hivi "
Kumbe ni Kweli hawavumi Lakini wamo.duuuuuuuuuuuu nikawa naona kama vile pacha wako.ndipo Nikaja nikakumbuka kwamba wewe haunaga pacha kumbe ndiyo Zamda mwenyewe. Duuuu Amakweli uvumilivu umekushinda.
Sikuelewi unaongelea nini Kwasababu Mimi hapa nimewakaribisheni kwa maneno mazuri tu Lakini Chakushangaza nyiye mko kishari shari tu."Mda huo Jamaa ambaye yuko meza moja na Zamda wala hakuwa anaongea chochote Wakati Kidawa anatoa maneno yake. Kisha Mwantumu akasema Hivi ".
Kumbe ndiyo maana wakaimba mchana malaika usiku mashetani."Baada ya hapo Kidawa na Mwantumu wakawa wameamua kuondoka na kwenda kutafuta nao sehemu yao ya kujiketisha ili wawasubirie mabahasha wao.Ndipo hapo Sasa mpenzi wake Zamda ambaye kwa jina anaitwa Tito akawa amemuuliza swali huyo Zamda Hivi".
Mbona Hawa wadada kama vile unawajua nawanakujua afu mnaamshiana maneno maneno tu."Akiwa anatoa glass mdomoni na kuiweka juu ya meza ili aweze kuongea kwa kujinafasi. Ilikuwa hivi".
Baby wala usiwaze kuhusiana na Hawa.Walikuwaga mashoga zangu sana kipindi hicho si kwa Sasa .kwanza nimeshangaa wananifuata hapa. Kwasababu kuna Kipindi tulifikia tu urafiki tukawa tumeukata."Tito akamuuliza Hivi".
Kwasababu gani urafiki wenu ulivunjika?.
Mhhh aa... ni Stori ndefu sana ila kwa ufupi tu ni Kuhusiana na utofauti wa kitabia.Kwamba tabia zangu na tabia zao ni vitu viwili tofauti sana tena sana. Ndipo nikaamua kujitenga katika kikundi kile na kubaki Mimi kama Mimi hadi Sasa niko na Wewe.
OK kama ni hivyo sawa Mimi nikajua ni maugomvi mengine tu.Kwasababu nyiye wanawake huwa mnakuwaga na visasi vya kishenzi kwelikweli. Aaaaàaa....embu tuachane na hiyo mada kwanza.
Sawa itakuwa vizuri kweli tukiongelea Mambo yetu kwa mda huu.
OK Zamda kama nikivyokwambia huku nimekuja kikazi tu huku.Kwahiyo kama siku chache hivi naweza kugeuza Hivi. Aaaaaa....pia nataka nitafute siku ambayo nitapata nafasi ya kutoka na wewe mchana tuende hata Guesthouse hivi tukatulie kwanza.Kwasababu leo ni kama tumekuja kunywa tu.Au wewe unaonaje hiyo Nafasi itapatikana?.
Aaaaa....Kweli my nitaangalia kama nafasi itapatikana...... Mmmh nitakutaarifu kweye simu My.
Itakuwa vyema Zamda .Aaaa Mimi najua kwamba unaweza Ukashangaa sana kwamba mapenzi yetu bado hata siku ngapi hazijaisha ila nakuambia tuende guest house unaweza Ukashangaa kidogo Au hata moyo wako kusita kabisaaaaaaa. Au siyo.
Hapana.... Hapana. Chamsingi tu mda ukipatikana ndiyo hivyo. Mimi ntatumia njia yoyote hata kama wazee watakuwepo nyumbani niweze tu kuwapanga kwa namna yoyote ile ili waweze kunielewa na Natumai kwa ujanja wangu watanielewa tu.
Haya ni Kweli navyokuona ni mjanja mjanja Kweli. Lakini Angalia usijeukauzidisha viwanja na viwanja vingine na watu wengine.
Hapana bana my sitokufanyia hivyo kwani natambua uwepo wako hapa kwa Mimi na Wewe.
Yawezekana wewe ukawa ni mjanja wa viwanja kweli kweli Kwahiyo hata na washikaji wengine lazima utakuwa na ujanja nao wakutoka nao kwa viwanja vingine.Nanivyojua na kusikia kuhusiana na Stori za watoto wa mkoa wa Ngata namna walivyo si haba nao.Kama ni kuvuma wanavuma na kusikika kabisaaaaaaa wanasikika.
Aaaaaaaaaaaaaaa.. My hizo ni Stori tu kila mtu Ana mawazo yake na mapendekezo kwamba awe na tabia gani.
Ni Sawa ila ndiyo Hivyo namna watu wa huko mkoa wa Kimbu tunavyojua kwamba huku Ngata wasichana Noma.mmmmmh.....Basi tuachane na hayo maongezi Natumai tumeafikiana kwamba jumapili hivi kwamba utafanya juu chini hadi tukutane.
Ndiyo usihofu nitakujulisha.
OK Kwasababu Kesho kuna mahali tunaenda ni mbali Kweli Kweli kikazi Yaani kidogo tunaweza kutoka hata huu mkoa wa Ngata.Itabidi nikupeleke nyumbani chapu afu Mimi niendee mageto.
OK Haina shida.
Basi Nakweli ujana maji ya moto Sasa sijui uzee Ndiyo utakuwa ni maji ya vuguvugu.Hivyo ndivyo namna Zamda alivyoanza kuwa wakutoka usiku ili kuelekea maeneo mbalimbali akiwa na jamaa yake ambaye wamekutana tu siku si chache baada ya kumkuta na Zamda naye alishaanza vitabia fulani Hivi japokuwa kuonjwa bado hawajamuonja ile sana japokuwa Ndiyo tayari geti lillishafunguliwa Yaani kufuli na komeo lote limetolewa. Sasa kazi wakutaka kuishi humo ndani.Huyo Tito naye ni kama kaonja Mara moja tu Hivi.
Kwa ufupi tu ni Kwamba Ngata,Kimbu ni mikoa ambayo inapatikana katika nchi za Afrika mashariki.Ila nchi hii ni kama yakufirika ambayo inajulikana kwa jina la Kinani.Kinani ni Taifa huru Kabisa katika pwani ya Afrika mashariki ambalo kabla ya uvamizi wa kikoloni lilikuwa na tabia ya uongozwaji na viongozi wa aina mbalimbali. Wakiwemo mamwinnyi na wengineo.Kwahiyo nchi ya Kinani kwa Hapa hii nchi ya kufikirika ambayo Kwakweli mipaka yake ni mipaka ya mapambo ya maua ya kuonesha ishara ya Upendo Yaani Upendo baina ya mtu na mtu fulani.Kwaujumla mipaka yao ni mipaka ya maua ya kuonesha ishara ya mapenzi katika taifa hilo.Taifa hili la Kufikirika lina mikoa mbalimbali tangu kujipatia Uhuru wake Ambalo kila mkoa una tabia yake.Mkoa kama vile Kimbu unatabia yake,mkoa kama vile Ngata unatabia yake na mikoa mingine mingineyo ambayo tutakuna nayo ina tabia mbalimbali.Tabia nyingine zikiwa ni tabia nzuri na nyingine zikiwa ni tabia mbaya.Kwahiyo mikoa Yote na maeneo yote nitakapokuwa naitaja Hapa yote hiyo itakuwa ni mikoa ya kutoka Kwenye nchi ambayo ni ya kufikirika ambayo ni Kinani na hata mingine nitaitaja kutoka nje ya nchi ya Kinani Lakini kote huko ni sehemu za kufikirika tu.
Basi Nakweli tabia ya Zamda nayo ilizidi kukua na kukua Zaidi. Yote hiyo ni Kwasababu ya Tito tu.
Basi siku Hiyo ikiwa ni siku ya jumapili hali ya hewa kwa siku hiyo ilikuwa Shwari kabisaaaaaaa Kwa mambo yote yanaweza kufanyika kwa furaha.Mkoa wa Ngata umejaaliwa Bahari fulani Hivi  ambapo Kwakweli watu hufurahika nayo sana bahari hiyo kwa siku za Mwisho wa wiki na kadhalika.
Ni siku mstarehe na saa maalumu kwa wapenzi wawili kwa mara nyingine kuweza kukutana katika Nyumba maalumu kwa kazi maalumu Tangu waanze mapenzi yao.Wapenzi hao nao si wengine ni Zamda na Tito.
Mda huo ikiwa ni saa Kumi alaasiri kwa saa za Afrika mashariki wakionekana wakiwa kitandani. Wakiwa katika chumba maalumu Furaha kwelikweli ikiwa inatoka katika nyuso zao na maneno yakiwa ni kama ya uaridi unukiaji wake ulivyo na ndivyo maneno Hayo yalivyo. Furaha ile inaonekana kabisaaaaaaa ni kutokana na kazi nzuri waliyotoka kupeana mda si mrefu katika kitanda Hicho.kwakazi hiyo aliyeifanya vizuri ni kwa hisani ya huyo kijana Tito.
Hivyo basi starehe waliyopeana mda si mrefu hapo wakaweza kuyasahau hata ya dunia kama vile kwamba hata duniani nako kuna Matatizo.
Mda huo ikionekana wako katika kitanda cha hadhi Fulani hivi Zamda yuko kichwa chake kakilaza kifuani mwa Tito na Tito  mda huo akiwa anampapasa pole pole huyo Zamda. Kwa ujumla wanavyoonekana kwa  mda huo ni kama vile Ndiyo wamezaliwa Leo. Basi matomasano yanapoendelea maongezi yakawa kidogo yamekatisha matomasano yale. Maongezi yao yalikuwa kama ifuatavyo.
"Mda huo Zamda Akionekana ana furaha kweli kweli kwa kazi aliyoifanya Tito kwa masaa ya kutosha huku akisema Hivi".Baby Yaani leo kama ni kunifikisha hapa Kweli umenifikisha mahali Penyewe kwelikweli.
" Tito akiwa bado kichwa cha Zamda kiko kifuani mwake na Yeye kalala huku kanyooka mithili ya nyoka aliyepigwa na baridi kwa mishale ya asubuhi katika maeneo ya equatorial. Tito akasema Hivi ".Mmmh Kweli Honey wangu?!.mbona mi naona kawaida tu kama sijui nini tu.
" Zamda akawa ametoa kichwa chake juu ya kifua cha Tito na Kisha akakilaza kitandani huku Jicho la Zamda likiendelea urembuaji ukawa umezidi na Kwa namna tu alivyojaaliwa Jicho na urembuaji huo ukawa ni kama mithili ya kinyonga akiwa msituni huku akiwa anapapasa kifua cha Tito japokuwa si kifua chakusema kinatisha himaya Bali ni cha kawaida Kwaujumla kimepigwa sakafu Lakini Zamda wala hakujali Hilo Chamsingi alichokuwa anataka ni kufuata tu msemo usemao Kwamba mjini kiuno.Huku Zamda akiwa anasema hivi ".kweli my hujapata utamu wangu kabisaaaaaaa.
" Tito akawa amekitoa kicheko kama vile hataki na kuonekana kwamba ni kicheko cha kifahari kweli kweli. Kisha Tito akasema Hivi ".aaaaaa.....Zamda Kwakweli kila mkoa umejaaliwa Bahati yake na bahati hiyo pia huwa kuna sifa pia yake katika mkoa huo.Ukisema Ngata tu watu wanapajua Kwahiyo ndiyo maana watu Wanasema Jamani nitacheza ligi zote ila fainali lazima niende Ngata nikapate Jiko mashaallah Viuno Ndiyo siyo masebene disco tu.Mda fulani hapo utamu Kwakweli ulinipatia hapa hadi nikasema Jamani huyu nimpeleke nyumbani nikamtambulishe.Yaaani Jamani haya Mambo utafikiri umesomea vile kumbe kipaji tu.Lakini ndiyo Nikaja nikakumbuka ahaaaaaaaaa kwamba kumbe wewe bado wakuitwa wakusoma baba hapo ndipo mawazo yangu yakawa yameishia njiani." Kisha Zamda akamjibu Hivi ".
usihofu namaliza siku si chache sana siutanipeleka tu nyumbani. Kama Kweli baby wanipenda hapo ndipo nitaelewa Sasa.
Lazima nitakupeleka tu nyumbani. Tena kuhusu suala la kwenda kukutambukisha Yaani hapa ninaogopea tu kuhusiana na hilo suala la shule." Zamda akasema Hivi ".
Nimekuuliza hivi kwa makusudi tu.
Umekusudia nini Zamda?.
Aaaammmm ni Mara kama ya Pili nahisi tangu kukutana Mimi na Wewe ila hatujawahi kutumia kondomu na pia hujawahi hata kuniambia kuhusiana na suala la kutumia kondomu kabla hatujaanza kufanya kupeana utamu.
Kwani Zamda Tangu lini pipi ikaliwa na ganda lake japokuwa ni tamu kwelikweli?."Zamda akawa amecheka kisha akauliza hivi".
Heheeeeeeeeeeeeeeeeee wewe sema hivyo eeti kwamba naogopa nini afu uje usikie mimba ndiii hii hapa na ni yakwako itakuwaje?." Baada ya Zamda kugusia Mambo ya mimba akawa ameshituka na kumwambia Zamda hivi".
Embu kwasasa hayo Mambo tusiyaongelee Sana. Kwasababu nahisi kama siyo mda Wake Hivi. Kwanza samahani mda umekaribia kuna mtu niliahidiana naye kikazi nikakutane naye Kwahiyo itakuwa vyema nikimuwahi.
Lakini Honey haya Mambo hutokea tu bila hata kujua ni lini yametokea. Ukichanganya na hivi wala hatutumii kondomu sijui itakuwaje.
"Tito akionekana tayari anatoka kitandani huku akiangalia suruali yake vizuri na kuchukua bukta yake Kisha akaivaa na suruali yake akawa ameivaa huku akimwambia hivi Zamda".Mambo mengine yatajulikana huko huko mbeleni usipende kuandaa mbereko kwakuona kwamba una mimba kubwa kama mlima Kimbu Bali andaa mbereko baada ya kujifungua. Sijui kama umenipata.
Sawasawa nimekupata Tito ila kwa Mimi tumbo langu ndilo litanijuza Majibu sahihi kwa mda wa kipindi fulani ambao litatakiwa liwe Hivyo.Afuu my siku si chache tu tunaanza Mtihani nipatie basi Hela hata ya nauli na chakula.
Sawa nitakupatia,nitakutumia kwenye simu mda ukifika wewe utanijuza tu.
Basi baada ya kila mtu kumaliza kuvaa nguo wakapeana kiss na wakawa wametoka  nje na kumuaga mhuhudumu wa kwanza na mhudumu wa Pili.
Wahudumu hao nao si haba kweli wamejaaliwa.wakawa wanamaongezi kama yafuatayo.
" Mhudumu wa kwanza kwenye kiti cha pande mbili Hivi Yaani zote twageuka huku akimwambia mhudumu wa Pili hivi". Mmmh!. Shoga wangu jumapili wateja wengi Kwakweli Yaani ni kupishana tu atoke huyu aingie yule.Yaani ni mwendo wa jackpot tu Hapa.Furaha iliyoje hapa."Kisha mhuhudumu wa pili akasema Hivi ".
Yaani leo Ndiyo jumapili watu wamejibania wiki nzima huko makazini na leo tena wajibanie." Kisha Mhudumu wa kwanza akasema Hivi ".
Ila daaa na wewe unawakomba kwelikweli.
Wala mbona kawaida tu wewe. Wanadata na hii wowowooo wewe .Yaani kama kuna mmoja hadi nikamuonea huruma eti oooo Dada umejaaliwa Jamani sinikuchukue tu wewe ukaishi na Mimi.
Afu ukamwambiaje Sasa?.kwanza siungekubali tu chapuchapu
Weeee nikamwambia kaka samahani usijeukajutia katika Maisha yako tu acha nikwambie tu ukweli ni kwamba  hapa niko kikazi wewe nipe Hela Yangu na wewe ondoka zako.
Noma sana iyo Tena.
Weeeeee mungu kaumba Wewe.