MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI - SIMULLIZI : MIMI NI MUAFRIKA ……SEHEMU YA 15… MWISHO

JIFUNZE KISWAHILI

Full Version: SIMULLIZI : MIMI NI MUAFRIKA ……SEHEMU YA 15… MWISHO
You're currently viewing a stripped down version of our content. View the full version with proper formatting.
…SEHEMU YA 15…
Msitu wa mikoko:7:00am
Msafara wa magari hamsini ya kikoloni uliwasili msitu wa mikoko, gari la kwanza likiwa na jenerali wa jeshi la kichina aliyeitwa Liang Xung,alikuwa ameketi viti vya nyuma, ndani ya gari,mbele yake alikuwa ameketi gavana Richald Robeni, pamoja na mlinzi wake ambaye alikuwa akiendesha gari.

“,Tumefika, msitu ndiyo huu! “,mlinzi wa gavana Richald Robeni aliongea, akasimamisha gari lake,akageuza shingo nyuma,palepale akapigwa na risasi, akafa palepale.
“,Mikono juu! “,gavana wa kichina aliongea, alikuwa amemnyoshea bastola kichwani gavana wa kiingereza, Richald Robeni na yeye alipitia mafunzo ya kijeshi, akataka kuchukua bastola yake lakini alionekana.
“,Nitakumaliza kama nilivyomfanya mwenzako, usisubutu kuweka mikono yako mfukoni! “,jenerali wa kichina aliongea, akamtoa nje, akiwa amempiga roba na kumuwekea bastola kichwani.
“,Wamemkamata gavana yetu, wanataka kufanya mapinduzi na kuchukua koloni letu,tupambane, lets fight ……”,jeshi la waingereza walisikia mlio wa risasi ndani ya gari lililokuwa na gavana wao, wakashuka kwenye magari yao, kabla hawajalisogelea gari, gavana wao akatoka nje akiwa chini ya ulinzi, wakakasilika, makundi yote mawili yakanyosheana silaha,jeshi la kichina pamoja na jeshi la wenyeji ambao ni wazungu wa kiingereza.
“,Mkifanya lolote nammaliza kiongozi wenu! “,kiongozi wa kichina alizungumza, akaamua kubadili mbinu, jeshi la waingereza walikuwa ni wengi, akaamua kuchukua utawala mapema sana kabla ya kwenda kupigana na Waafrika.
“,Put downs your guns! (Wekeni silaha zenu chini …)”,jenerali Liang Xung aliongea, jeshi la waingereza wakagoma kuweka silaha chini, kwa sasa makundi yote yalikuwa yametengana, jeshi la waingereza walikuwa wamesimama upande wa kusini, wakati jeshi la wachina wakiwa wamesimama upande wa kaskazini.
“,Put down your guns , mnataka niuwawe! “,gavana Richald Robeni akafanya kosa lingine tena, likaugharimu utawala wake, alitoa amli, vijana wake wakaitii kwa shingo upande, wakaweka silaha zao chini, askari takribani kumi wa kichina wakakusanya silaha zote za waingereza, wakaziweka upande wao.
“,Fireeee them, waueee! “,jenerali wa kichina alitoa amli kwa jeshi lake, alikuwa katili kama gavana wake.
“,What! “,Richald Robeni alishangaa sana, alizani atasamehewa, kumbe sivyo!.
“,Paaaa,papapa,paaaa,paaaa! !”,jeshi la waingereza walishambuliwa na risasi,wakafa kama nzige, hawakuwa na uwezo wa kujitetea, walijuta kusalamisha silaha zao.
“,Paaaaaa! “,gavana Richald Robeni na yeye akasambaratishwa ubongo wake, akafa palepale.
“,Yeeeeee! Goshani is our kingdom!(Goshani ni ufalme wetu) “,askari wa kichina walishangilia,koloni la nchi ya Goshani lilikuwa mikononi mwao,vita iliyokuwa imebakia ilikuwa dhidi ya jeshi la Waafrika, vita ambayo waliiona ni rahisi kuliko vita yoyote ile ambayo walikuwa wamepigana,jenerali wao alikuwa amesimama mbele, msururu mrefu wa askari ukamfuata kwa nyuma, macho yao yalitazama mita mia moja mbele, kulia, kushoto na juu ya miti, walikuwa makini sana tofauti na jeshi la waingereza.
Msitu ulikuwa mnene, ulijaa vichaka kila kona, ulitisha, jenerali Liang Xung machale yakamcheza,akaogopa kutangulia mbele,akatanguliza vijana wake kumi, yeye akakaa katikati, msafara ukaendelea.
…………………………………
Jeshi la Waafrika walishtuka usingizini, milio ya risasi iliwashtua sana, kila mmoja akachukua bunduki yake, akaikoki, akajiandaa kufanya shambulio.
Umbali wa mita kadhaa walianza kusikia kelele za watu, Angel akasogeza sikio lake juu ya ardhi, ardhi ilikuwa inatetemeka,wote wakatazama juu, makundi ya ndege yalikuwa yanahama kutoka mwanzo wa msitu, kuja katikati ya msitu.
“,Wanakujaa, jiandaenii, nikitoa amri, shambulia adui! “,Angel aliongea, baada ya dakika tano,jeshi la kichina lilikuwa mbele yao, sare zao zilikuwa na rangi nyeupe pamoja na madoa mekundu, walifanana kwa kila kitu,jeshi la Waafrika wakapigwa na butwaa, askari waliokuwa mbele yao hawakutambua walitokea wapi.
“,Yaaaaala…aa, nakufa…aa …”,
“,Paaa,paaa,paaa!”,
Askari wa kichina waliokuwa wametangulia mbele walidumbukia ndani ya shimo la mtego,wakachomwa chomwa na miti iliyochongoka ndani ya shimo,wakafa palepale,walikuwa askari kumi,jeshi la kichina wakapiga risasi hovyo,waafrika wakalala chini,alimanusura ziwapate vichakani.
“,Ni mtego! wamekufa kikatili, shiit! “,jenerali alishangaa sana, kama si machale kumcheza na kurudi nyuma, angekuwa miongoni mwa askari waliopoteza maisha.
“,Let’s go on, tuendelee na safari but you have to be careful, muwe makini sana! “,jenerali Liang Xung aliongea,msafara ukaendelea, yeye akiwa amesimama katikati, walipiga hatu mbili tu,shambulio lingine likafanyika.
“,Puuuuuu! “,askari mmoja aliyekuwa ametangulia mbele alijikwaa kwenye kamba ya mtego akajitupa mweleka, gogo likatoka juu na kumpiga tumboni, damu zikamtoka mapuani, mdomoni na masikioni, alikufa palepale. Jeshi la kichina likaogopa, likarudi nyuma, wote wakaogopa kusonga mbele.
“,Songa mbelee, tumewauaa askari wa kingereza pamoja na gavana wao, hawa weusi ndiyo watushindee?, let’s move on, songa mbelee! “,jenerali wa kichina aliwafokea vijana wake, kila mmoja aliogopa kutangulia mbele, Angel alikasirika sana, baada ya kusikia baba yake ameuawa, japo hakuelewana na baba yake, lakini alikuwa bado anampendaa.
“,Fireeee them,fireee, piga risasi, shambuliaaa! “,alitoa amli kwa hasira, akarusha bomu lake dogo ambalo lilikuwa mkononi mwake
“,Puuuuuu ,puuu”,lililipuka na kuuwa askari wa kichina kumi na tano, miili yao ikiwa imekatika vibaya sana, kila kiungo mahala pake.
“,Paaaaa, paaaa, paaaa, paaa! “,Waafrika walifanya shambulio la ghafla,wakaua askari hamsini wa kichina, wakabaki askari thelathini na tano, wakafyatua tena risasi zikagoma, risasi zilikuwa zimeisha kwenye magazini za bunduki zao, hapo ndipo mwisho wao ulikuwa umefika, walikuwa hawana silaha nyingine yoyote, isipokuwa Ishimwe aliyekuwa na upinde wake pembeni, akauchukua na kuanza kufyatua.
“,Pyuuuuu! “,Ishimwe alifyatua mshale, alimanusura umpige shingoni jenerali wa kichina, akatazama mahali mshale ulipotokea, akapiga risasi hovyo, askari wote waliobakia wakasambaratisha vichaka na risasi,vikawaka moto.
“,Puuu, puuuuu! “,mlipuko ulisikika, askari wa kichina walilusha mabomu mawili vichakani, Angel akapigwa na bomu, akafa palepale, Mwamvua akafa palepale, Ishimwe na Mpuzu wakajisalamisha, wakanyosha mikono juu, walikuwa wamebaki wawili tu, machozi yaliwatoka,ndugu zao walikuwa wamekufa kikatili,walipigwa na bomu, kila kiungo kilikuwa mahali pake.
“,bhanetuuu bhafwaaa, bhanetuuu bhafwaaa, bhagabho bhachuu bhafwaaa! “,(watoto zetu wamekufaa, waume zetu wamekufaaa! “,Waafrika, wanawake, wazee na watoto waliokuwa juu ya miti walilia, jeshi la kichina likasikia kelele zao juu ya mti mkubwa wa ubuyu, askari wakapanda juu ya mti, wakawatoa Waafrika wote, wote wakawekwa chini ya ulinzi,safari ya kutoka msituni ikaanza,Waafrika wakiwa na majonzi,kwa sasa walikuwa chini ya uongozi wa Wachina.
…………………………………
Gavana Hwang lee alifika nchini Goshani ,alifurahishwa na taarifa za ushindi,jeshi lake lilimchukia,aliwatesa na kuwaua askari wake mara kwa mara,kwa kosa dogo tu,walimpania muda mrefu kumuua.
“,Paaaaaa,paaa!”,risasi mbili zilifyatuliwa, moja ilimpiga gavana,nyingine akapigwa kichwani mlinzi wake ,wote wakiwa wanashuka kwenye helikopta kuikanyaga ngome kubwa(great fort), ardhi ya nchi ya Goshani
“,Yeeeeee!aim your governer,now and onwards!”,(mimi ni gavana wenu,sasa na kuendelea)”, jenerali Liang Xung alipiga kelele za shangwe,alikuwa amekamilisha mauaji,askari wake wakamkimbilia na kumnyenyua,walimpenda sana,akawa gavana mpya wa Goshani pamoja na Gano,yaani ni kisasi juu ya kisasi.
…MWISHO…
Mpuzu na Ishimwe walipatiwa vyeo jeshini,baadaye wakapigania uhuru,wakashinda,Mpuzu akawa raisi,Ishimwe akawa waziri mkuu,wote walikuwa wazee,Gavana Liang Xung alizaa na mwanamke wa Kiafrika,wakapata Mtoto anaitwa Yuan Liang,Wachina walipofukuzwa Goshani,akarudi china na kuacha mtoto pamoja na mke wake,Yuan liang akawa yatima,soma Yuan Liang ujue mengi zaidii!
HADITHI HII NI MALI YA HAKIKA JONATHAN,PAKUA HAKIKA JINATHAN APP PLAYSTORE,AU TEMBELEA www.hakikajonathan.co.tz kwa burudani motomoto