MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI - DHIMA (MATUMIZI) YA REJESTA

JIFUNZE KISWAHILI

Full Version: DHIMA (MATUMIZI) YA REJESTA
You're currently viewing a stripped down version of our content. View the full version with proper formatting.
DHIMA (MATUMIZI) YA REJESTA
(i) Rejesta Hutumika Kama Kitambulisho
Rejesta hutofautisha mtindo wa lugha miongoni mwa wazungumzaji. Rejesta inawatambulisha wazungumzaji kuwa wao ni kundi fulani.
Mfano: Rejesta yawahunzi inawatambulisha kuwa wao ni tofauti na wavuvi ambao nao pia wana rejesta yao. Rejesta ya kanisani au msikitini ni tofauti na rejesta ya jeshini, n.k.
(ii) Rejesta Hupunguza Ukali wa Maneno
Rejesta inapotumiwa na kundi la watu, huficha jambo hilo linalozungumziwa lisieleweke kwa wengi. Hivyo hadhira inapuuzwa kwa sababu siyo watu wengi wanaoelewa.
(iii) Rejesta Inatumika Ili Kurahisisha Mawasiliano
Rejesta inatumika ili kurahisisha mawasiliano au kupunguza muda wa kuwashughulikia watu au wateja wengi. Kwa mfano mganga anayegawa dawa hospitalini anaposema “mbili asubuhi, mchana na jioni” akiwa na maana kuwa mgonjwa anywe vidonge viwili asubuhi, viwili mchana na viwili jioni. Hapa amefupisha ili aweze kuwahudumia kwa wakati mfupi wagonjwa wengi wanaosubiri kupata dawa.
(iv) Rejesta Hupamba Lugha Miongoni mwa Wazungumzaji
Kwa mfano,
Rejesta ya Hotelini.
Mhudumu: Nani wali kuku?
Mteja: Mimi hapa!
Mhudumu: Nani ugali-ng’ombe?
Mteja: Mimi hapa!
Mazungumzo haya kati ya mhudumu na mteja licha ya kurahisisha mawasiliano, vilevile yanapamba mazungumzo hayo.
(v) Rejesta Huweza Kuwa Kiungo cha Ukuzaji wa Lugha
Kutokana na matumizi ya rejesta mbalimbali, lugha inayohusika inaweza kuunda msamiati wake. Kuna baadhi ya maneno ya lugha yanayotokana na rejesta mbalimbali.