MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI - NADHARIA YA UHUSIANO: ISHARA ZA PROPOSISHENI NZURI (4)

JIFUNZE KISWAHILI

Full Version: NADHARIA YA UHUSIANO: ISHARA ZA PROPOSISHENI NZURI (4)
You're currently viewing a stripped down version of our content. View the full version with proper formatting.
ISHARA ZA PROPOSISHENI NZURI

Proposisheni nzuri yapaswa kujadilika na vilcvile kuthibitika. Hi proposisheni itambuiike kuwa bora, basi yapaswa kutimiza mambo haya mawili. Kujadiliwa au kukubaliwa kwa proposisheni ni jambo ambalo litakalotegemea maoni ya watu tofauti tofauti na msukumo walio nao hasa wa kimamlaka, kulihusu jambo hilo na uwezo wao wa kuwasawishi wasikilizaji. Pia proposisheni nzuri yapaswa kuwa na masharti ya kweli au uongo, kisha thamani iliyopo katika proposisheni hiyo ili ifahamike kama ni nzuri au la.
PROPOSISHENI NZURI YAPASWA KUJADILIKA
Mjadala wake ni muhimu ili mambo husika yakubalike au yakatalike katika proposisheni. Msemaji humhimiza msikilizaji katika mjadala dhidi ya proposisheni. Proposisheni kama zitakataliwa au kukubaliwa, ukweli utakubalika hata kama hautathibitika na wanaoshiriki katika mazungumzo. Kwingineko uongo utabaki kuwa si kweli hata kama tutasawishika kuukubali. Kwa mfano: ‘‘Nchiya Kenya niyenye ufisadi’.
Kauli hiyo, ina proposisheni kuwa:
1) Kuna nchi fulani iitwayo Kenya.
2) Nchi hiyo huwa na ufisadi.
Ufisadi wa Kenya ni suala linaloweza kujadilivva kisha likakubaliwa au kukataliwa. Kwingineko, wanaoshiriki katika ufisadi watashikilia msimamo kuwa hakuna hatia yoyote katika ufisadi kwani ni njia mojawapo ya kujisaidia katika umiliki mali kwa kuwanyanyasa vvengine. Kisha, wanaonyanyaswa kupitia kwa ufisadi watahisi kuwa ni jambo ovu na wanapaswa kukabiliana nalo ili kulimaliza haraka iwezekanavyo.
 
Huenda ikawa walio na uwezo watazidi kuwanyanyasa walio wanyonge.
PROPOSISHENI NZURI YAPASWA KUTHIBITIKA
Ukweli wa kauli ni muhimu ili kuthibitisha ukweli wa proposisheni ipasavyo. Uongo wa proposisheni kama hauwezi kuthibitishwa basi vilevile, hata ukweli wake hauwezi kuthibitishwa. Kwa mfano: ‘Kunanyesha’ Kauli ya hiyo, ina proposisheni kuwa:
1) Msemaji huenda ikawa ametazama nje na kuona kuwa kunanyesha.
2) Pengine kuna mingurumo ya radi na matone ya mvua yanayoanguka.
Ni jambo ambalo laweza kuthibitishwa kuwa ni kweli au ni uongo, kwa kutazama nje au kwa kuzingatia
yaliyotajwa na wanaotangaza kuhusu hali ya anga. Mfano mwingine ni kuwa: ‘Yesu Kristu atarudi tena ’.
Proposisheni hapo, ni kuwa:
1) Msemaji ni muumini wa dini ya kikristo.
2) Msemaji huyasikiliza mahubiri ya injili.
3) Msemaji ana imani kwa Yesu Kristo.
4) Msemaji anaamini kuwa Yesu Kristo atarudi.
Kauli kama ya hapo juu; haiwezi kuthibitika kuwa ni ya ukweli au uongo kwa sababu yategemea imani ya watu hasa kutoka dini tofauti. Hivyo basi, ni vigumu kuthibitisha kuwa ni ya kweli v au si ya kweli.

Akmajian na wenzake (2004: 254) wanasema kuna proposisheni ambayo huelcza jambo moja maalum na pia kuna proposisheni ambayo huelezwa kwa ujumla wake. Proposisheni ya jumla yaweza kufanywa ya kweli na mambo tofauti.
Kwa mfano: ‘Nakuahidi kuwa nitafika.’ Proposisheni hii itakuwa ya kweli kama nitatimiza ahadi yangu na kufika. Itakuwa ya kweli pia kama ni mimi nitakaye timiza jambo hilo na wala sitamtuma mtu mwingine.
Proposisheni inayoeleza jambo moja maalum, hulenga jambo mahususi na mtu fulani mahususi.
Kwa mfano: ‘Neil Armstrong ndiye aliyekuwa mtu wa kwanza kufika katika maeneo ya mwezi’ Proposisheni hii ni ya kweli kwani ni jambo linalojulikana kuwa lilitendeka na limo katika hifadhi.

Leech (1969:39-40), anasema kuwa kuna proposisheni mbili maarufu kama; mzunguko na ukinzani. Mzunguko ni aina ya proposisheni ambayo ni ya kweli kulingana na yanayojadiliwa katika jambo linalodokezwa.
Kwa mfano: ‘ Wavulana hukimbia shuleni’. Proposisheni katika mfano huo, unadokeza kuwa:
1) Wavulana hucnda shulcni.
2) Hivyo basi inathibitika kuwa wao hukimbia kuelekea shuleni.
3) Wavulana ambao hukimbia shuleni huenda shuleni.
Ina maana kuwa ni wavulana wote, wala sio baudhi yao au mmoja maalum. Proposisheni nyingine huwa
na madai ambayo yamefanana, nyingine madai yaliyopatana kwa jinsi mambo fulani yaliyofasiriwa na nyingine huwa na madai yanayofiiata mantiki ili kupata wazo la ujumla au pia muungano.
Kwa mfano:
1) ‘Watu ambao wana bahati wanabahati’ – kufanana.
2) ‘ Wenye magari humiliki magari’ – Yafuata mantiki.
3) ‘Mawazo yanayofaa watu huwafaidi wanasayansi
’. – Yafuata ufasiri wa jambo.
4) ‘Tufaha hupendwa na watoto ambao ni wa matajiri’. — Yafuata mantiki pamoja na ufasiri wa jambo.
Ukinzani ni aina ya proposisheni ambayo ni ya uongo kulingana na yanayodaiwa katika jambo lililodokezwa.
Kwa mfano:
1) ‘ Kunanyesha na hakunyeshi ’.
 2) ‘Nduguye John mdogo ni mkubwa kwake kwa umri ’.
Proposisheni hizi zina ukinzani kwa sababu haiwezekani kuwa jambo moja litatendeka na kinyume chake kwa pamoja. Maana ya umbo la kimantiki italingana na mfumo wa mantiki utakaoshughulikiwa.
Vilevile, proposisheni hizi zikielezwa kwa upana zaidi zitarejelea Proposisheni, yadokeza kuwa: maeneo tofauti.
Kwa mfano: ‘Kunanyesha Embu na hakunyeshi Nairobi’. Hivyo basi’ itakuwa hakuna ukinzani tena. Katika proposisheni kuna ukweli ulio na mantiki ambao pia ni ukweli ulio changanuzi ambao ukweli wake hutegemea maana yake.
Kwa mfano:
1 ‘Kapera huyu hajaoa’. – mzunguko.
2) ‘Kapera huyu ameoa’ – ukinzani.
PROPOSISHENI KATIKA MISINGI YA KWELI AU UONGO
Cambridge (2008: 1563-1564), wanasema kuwa ukweli ni jinsi ya ubora uliopo katika jambo lililo la kweli. Ni uhakika uliopo kuhusu hali, tukio au mtu. Husisitiza kuwa jambo ni la kweli, au ni hali ya kuwa katika ukweli. Cambridge (2008: 509), wanaendelea kusema kuwa uongo ni jambo lisilo halisi lakini hufanywa kuonekana kuwa kweli ili kuhadaa watu. Vilevile, kusema uongo kuhusu jambo, ni sawa na kusema jambo
lisilo sahihi, lililo kataliwa au lisilo aminika.
Wilson (1967: 76-79) anasema kuwa proposisheni ni ya kweli kama itatimiza mambo yafuatayo:
1) Mtu anafahamu maana ya jambo liliosemwa.
2) Mtu awe na njia mwafaka ya kuthibitisha jambo lililopo katika proposisheni.
3) Mtu awe na ushahidi unaofaa ili aweze kuliamini jambo hilo.
Kwa mfano: ‘Ni kweli kuwa dunia ni mviringo Kama mtu hafahamu maana katika kauli hivyo basi, hawezi kuthibitisha kuwa ni ya kweli au la. Vilevile, kama mtu hana ushahidi wa kutosha kuhusu jambo, basi itakuwa vigumu  kuthibitisha kuwa kauli hii ni ya kweli. Ni bora kuhakikisha kuwa kila mtu anafahamu maana ya kauli hii na njia mwafaka ya kuthibitisha kisha wanasayansi watafanya utafiti wao ili kuwa na ushahidi thabiti.
Kauli za aina tofauti hueleza mambo kadha kuhusiana na ukweli au uongo wa jambo fulani. Kama vile:
1) Kauli za kuamuru na za mtazamo.
2) Kauli chambuzi.
3) Kauli za thamani.
4) Kauli dhanifu.
AINA ZA KAULI
Fleming (1988:59-63) anasema kuwa kuna aina nne za kauli. Aina hizi ni kama zifuatazo: Kuamuru na mtazamo, chambuzi, thamani na dhanifu.
Kauli hizi tutazijadili kwa kuzieleza maana zake kisha kuzitolea mifano mwafaka kwa kila mojawapo ya aina hizi, ambayo itafafanua zaidi lengo la kauli zenyewe katika mawasiliano. Madhumuni ya kauli hizi hasa ni kumpa msikilizaji athari fulani baada ya kuzisikiza na mwishowe kuzifasiri kama ilivyo kusudiwa. Kwanza, kauli za kuamuru na mtazamo ni zile ambazo hutoa amri au hueleza mambo yanayomhusu msemaji kama; matumaini au analolitamani.
Kwa mfano:
1. ‘Tumikia Mungu na umheshimu Mfalme.’
 2) ‘ Tupendane sote kama ndugu.’
Kauli kama hizo hazina kusudi la kuwa ni za kweli au uongo kwani hasa zaeleza mitazamo ya watu kuhusu mambo fulani. Hivyo basi, mtu anaweza kughairi na kukosa kumtumikia Mungu na kutomheshimu vilevile. Pia, ana hiari ya kutopenda wengine kama ndugu.
Kauli hizi hueleza jambo kuhusiana na mtazamo wa mzungumzaji na wala sio jambo la hakika. Kwa
mfano:
1. ‘Wanaume wote ni sawa.’
2. ‘Wanaume wote ni huru.’
Ili kuthibitisha kauli hizi, itabidi kutazama mambo yote ya kijumla katika wanaume, kama vile; urefu na werevu kisha kuchunguza mambo haya kama ni sawa.
Vivyohivyo, ni jambo bora kubainisha ni jambo lipi litakalosababisha wao kuwa huru. Kama, mwanamume
amepewa hadhi ya juu katika jamii, kuwa yeye ndiye atakayefanya uamuzi wa mambo yote katika familia basi, mwanaume atakuwa na uhuru wa kufanya lolote alitakalo.
Ujumbe waweza kupashwa kupitia kwa kauli ambapo itakuwa muhimu kufahamu ujumbe wenyewe ni wa aina ipi, na jinsi ya kuweza kutambua na kuwa na ushahidi kama jambo ni la kweli au la. Kwa mfano: ‘Mungu ni Baba yetu anayetupenda.’
Kauli kama hii yaweza kuwa ni ya mtazamo ambayo itamaanisha kuwa:
1) Tunapaswa kupendana sote kama ndugu.
2 ) Tushukuru kwa mambo mema katika maisha yetu.
Kauli hiyo, hatuwezi kuithibitisha kuwa ni ya kweli au ya uongo, kwa sababu ukweli wake au uongo wake utategemea mtazamo wa mtu binafsi. Kauli za majaribio ni zile ambazo huwa na ujumbe kuhusu dunia kwa misingi ya tajriba za watu tofautitofauti katika dunia.
Kwa mfano:
1) ‘Mji wa London umo nchini Uingereza.’
2) ‘Dunia huzunguka jua
Jambo lenye uhakika huelezwa kwa kauli hizi na tunaweza kuamua kuwa ni za kweli au za uongo. Kunao
uhakika wa kauli.
Kwa mfano: ‘Jua litachomoza miale yoke kesho.’
Uwezekano uliopo ni kuwa watabiri wa hali ya anga walitabiri kuwa siku itakayofuata kutakuwa na jua. Vilevile, huenda jua likose kuchumuza, kwani Labda hali ya anga yaweza kubadilika. Kwingineko, tunaweza kuwa na jambo ambalo laweza kuhakikishwa.
Kwa mfano: ‘Wanaume wote ni binadamu’. Hii ni kauli ya kweli kabisa kwa sababu jina mwanaume ni la kiumbe ambaye ni binadamu. Hata hivyo hili ni jambo linalojulikana wazi na watu wote kuwa wanaume wote ni binadamu. Tunapaswa kufanya uchunguzi fiilani, ili kuthibitisha baadhi ya kauli.
kwa mfano:
1) ‘Kutanyesha kesho.’
2) ‘Shangazi ni mgonjwa.’
Katika kauli ya kwanza, kipimahewa chaweza kutumika ili kuthibitisha jambo hilo kuwa kutanyesha kesho.
Katika kauli ya pili, shangazi atafanyiwa uchunguzi wa maabara hospital ini ili kuthibitisha ugonjwa wake ni upi. Kabla ya kuthibitisha kauli hizo, kupitia kwa uchunguzi, basi zitakuwa tu ni kauli zenye uwezekano wa
kuwa kweli na baadaye zitathminiwe kuwa ni za kweli au za uongo. Pili, kauli chambuzi ni zile ambazo baada ya kutathminiwa huwa za zingatia kanuni fulani za kimantiki. Kauli hizi hazina ujumbc kuhusu mambo ya ulimwengu na wala haziwezi kuthibitishwa kupitia kwa tajriba ya mtu.
Kwa mfano: ‘Chochote ambacho ni chekundu kina rangi.’ Kauli yenyewe yaeleza kuhusu wekundu, kuwa ishara ya rangi nyekundu kama itatumika basi itabidi kutumia rangi ambayo ni nyekundu kwa kuerejelea kifaa kilekile kimoja.
Kwa mfano: ‘ Taa za trafiki huwa ni rangi nyekundu, rangi ya machungwa na rangi ya kijani kibichi’.
Hivyo basi, katika kuzichora rangi mwafaka zitatumika katika kuwakilisha kila rangi. Vilevile’ katika mfano mwingine:
1) ‘Kuanguka kwa kitu fulani humaanisha kuelekea chini, kama kitu kitaanguka kuelekea juu, basi jambo hilo haliwezekani kamwe, kwani ni jambo ambalo ni kinyume cha kawaida ya mambo.’
2 ) ‘Nina tufaha mbili katika mkono wa kulia na tufaha mbili katika mkono wa kushoto.’
Kauli ya kwanza , ina habari za kisanyansi ambazo zimetafitiwa na kuthibitishwa kuwa kila kitu huanguka kuelekea chini.
Kauli ya pili, yatufahamisha kuwa ninazo tufaha nne, kwani tunafahamu kuwa katika majaribio, mbili kuongeza mbili ni nne.
Tatu, kauli za thamani ni zile ambazo hutumia maneno kwa sababu ya kutathmini au kuependekeza jambo fulani.
Kwa mfano:
1) ‘Ni mtu mzuri.’
2) ‘Haupasrwi kufunya hivyo.’
3) lN i saw a kuwaua wauaji.’
Vigezo vya kutathmini vitategemea uamuzi wa mtu binafsi kuwa kitu ni chenye thamani au la. Uamuzi huu
utategemca vigezo kama mtu ni mwaminifu, mkarimu, mwenye ujasiri, mwenye uwazi katika kusema na kutenda mambo.
Kwa mfano: ‘Maria ni mwanamke mzuri.’ Mtu fulani kumpendekeza Maria kuwa ni mzuri labda vigezo vilivyo hapo juu vilitathminiwa na kuwa vimo katika tabia za Maria. Tunapata mtazamo kuwa yeye ni mwanamke mzuri. Ithibati katika kauli za thamani itategemea tajriba za watu au maarifa kuhusu uhakika wa jambo na
vilevile vigezo vya thamani.
Kwa mfano:  ‘Kuna wale watakaokuwa na vigezo tofauti vya kumtathmini Maria na kwa wao Maria atakuwa mwanamke mbaya.’ Huenda hawakuuona ubora wowote katika tabia za Maria, hivyo kupingana na kauli kuwa Maria ni mzuri. Kwingineko, katika kueleza mifano mingine inayoafikiana na iliyopo hapo juu ni kuwa: ‘Serikaliyetu ni nzuri.’ Kauli hii pia italenga vigezo ambavyo vitatumika kuitathmini serikali yetu, kama vile: ‘Ukarabati wa barabara, elimu ya bure kwa shule za msingi na za upili.’ Vigezo hivi vikitumika, basi tutaipa serikali yetu thamani kwa mtazmo wa kuisifu, na kama vigezo tofauti vitazingatiwa, kama vile: ‘Ufisadi na unyanyasaji wa wafanyikazi,’ tutapata kuwa tunaipa serikali yetu kashfa na kukosa thamani ya kuisifu. Nne. kauli dhanifu ni zile ambazo uthabiti wake utategemea mambo ambayo yatachukulivva kuwa ni ya kufaa. Mambo haya ni yale ambayo hayajakubaliwa lakini yanaweza kujadiliwa kuwa yatakubaiiwa au la. Hueleza mambo ambayo si ya kawaida katika ulimwengu na ambayo ni ya kumiujiza. Kauli nyingi dhanitu hupatikana katika mambo ya kidini. Hata hivyo, kuna kauli dhanifu ambazo hazina uhusiano na mambo ya kidini na hasa zimo katika mambo kamilifu, kama vile: Haki, urembo, na ukweli. Pia, kauli za ubinafsi na hiari.
Kwa mfano: ‘Mungu atawaokoa walio waadilifu.’
Watu watajadili kuwa kauli hii ni sawa au si sawa, ni kweli au ni uongo. Kauli dhanifu inapaswa kukubalika kimaana na kudhibitiwa ili kuwasiliana kuhusu mambo yaliyomo katika ulimwengu wa kawaida na usio wa kawaida.
Kwa mfano: ‘Ni jukumu la mtu binafsi kulichagua alitakalo maishani.’ Kauli hii yaeleza kuwa binadamu ana hiari ya kulichagua jambo alipendalo kulizingatia yeye bila kushurutishwa na mtu yeyote kulifanya asilolitaka. Kwa mfano: ‘Kila mzazi anapaswa kumwelimisha mwanawe.’
Kulingana na kauli hii ni haki ya kila mtoto kupata elimu ambapo kila mzazi anapaswa kugharamia kwa kulipa karo na mahitaji mengine ya kielimu.
Comford (1957: 287- 290) anamnukuu Plato na kusema kuwa kulingana naye, chochote kilicho halisi hakina budi kuwa kweli, kwani si kitu kingine chochote bali ni kitu maalum kilicho halisi, kama vile: ‘Mwendo kama kitu ambacho ni halisi.’ Kauli hii ina maana kuwa mwendo ni kusonga kwa kitu kutoka mahali kilipokuwa na kupiga hatua fulani hadi mahali pengine. Hivyo basi, kwa kuzingatia kauli hii kuhusu mwendo tutatoa mifano kuwa:
1) ‘Mwendo ni kitu ambacho hakipo.’
2) ‘Mwendo ni kitu ambacho kipo.’
Kulingana na kauli hizo, ya kwanza si ya kweli kwa sababu mwendo ni kitu ambacho kipo ilhali kauli ya pili ni kweli kwani yasema kuwa kipo, ni jambo la kweli na hutendeka. Msemaji anatafakari kuhusu kauli ambazo ni za uongo kama zina maana yoyote. Ni vigumu  kwa mtu kuzungumza mambo ambayo hayapo na
ambayo mtu hana uhakika nayo. Hivyo basi, kauli zote ambazo si za kweli hazina
maana yoyote.
Kwa mfano:
1) ‘Chuo Kikuu cha Nairobi kimo mjini Dar es salaam.’
2) ‘”Rais wa Marekuni ni mwanamke.’
Kauli hizo, ni za uongo kwa sababu, kama tunavyofahamu proposisheni tunazozipata kutoka kwa kauli hizi si kweli, kwani katika kauli ya kwanza, Chuo Kikuu cha Nairobi kimo mjini Nairobi nchini Kenya. Dar es salaam ni mji uliopo nchini Tanzania. Kauli ya pili, si ya kweli vilevile kwani Rais wa Marekani anayetawala kwa wakati huu ni mwanamume na wala si mwanamke.
Kauli ambazo ni za kweli huwa na:
1) Jambo ambalo ni la kimsingi katika kauli hiyo.
2) Kitendo kinachoelezwa na kitenzi.
3) Mfumo wote unaohusika na kauli hiyo.
Ni bora basi kuzungumza mambo yaliyohalisi na yaliyopo. Kauli ya kweli na ya uongo, vile vile huwa na kiima na kiarifu chake. Hivyo basi sio kwamba kauli ya uongo haizungumzii chochote hata kama haina maana yoyote, kwani ina kiima chake na kiarifu chake kama vile kauli ya kweli ilivyo. Uamuzi baina ya wanaowasilisha ujumbe na wanaopokea ujumbe ni muhimu kwa sababu wanaweza kuamua kuhakikisha jambo lisilo la kweli likawa la kweli. Watafanya hivyo kwa kusisitiza kuwa ni kweli, ilhali wanajua kuwa ni uongo.
Linsky (1952:15-16) anasema kuwa ukweli katika sentensi wahusu ukubalifu wake katika uhalisi. Sentensi ni ya kweli kama itaweza kuthitibisha hali ya mambo yaliyopo kuwa ni ya kweli.
Kwa mfano: ‘Theluji ni nyeupe’ Tunapaswa kutafakari ni katika masharti yapi ambapo kauli hii ni ya kweli au ni uongo. Proposisheni hii basi ni ya kweli kama theluji ni nyeupe na ni ya uongo kama theluji si nyeupe.
Hata hivyo, tunafahamu wazi kuwa ni kauli ya kweli kwa sababu sote tunajua kuwa theluji ni nyeupe. Ili kupata maelezo mwafaka ya ukweli ni vyema kuhusisha mawazo ya kisemantiki, kama vile; kukidhi mahitaji.
Kwa mfano: ”Nchini mwetu elimu imetiliwa maana na asasi za mambo ya kielimu kuongezeka, ili kukidhi mahitaji ya kielimu.’ Tumeelezwa hapo awali kuwa jukumu la kukidhi mahitaji ni muhimu katika semantiki. Hivyo basi mfano huo, unaeleza kuwa ni mahitaji ya kielimu ambayo hutimiza uchu wa binadamu kwani hutaka kupata elimu zaidi wakati wote. Kauli hiyo, ni ya kweli kwani yaeleza proposisheni kuwa:
1) Elimu ni muhimu nchini mwetu.
2) Asasi za kielimu nchini zimeongezeka.
Vilevile kauli, inakidhi mahitaji ya kielimu ambayo wananchi wengi nchini mwetu wanazidi kuyahitaji.
Kempson (1975: 33-34) anasema kuwa kauli yenye maana katika lugha asili ni kauli yenye masharti ya ukweli katika sentensi za lugha hiyo. Kwa mfano: ‘Mtoto alimkimbilia mamake.’
Kauli hiyo, ina proposisheni kuwa:
1) Aliyckimbiu ni binadamu mwcnyc umri nidogo.
2) Amcfanya kitendo cha kukimbia.
3) Ameelekea kwa mzazi wake ambaye ni wa kike.
Hata hivyo, kauli hii yapaswa kutimiza masharti ili kudai ukweli uliopo katika kauli hiyo. Kauli ambayo inaeleza maana hubainisha kuwa kuna uwezekano wa sentensi hiyo kuwa ya kweli. Katika sinoniminia ambapo sentensi au maneno tofauti yatakuwa na maana sawa, basi masharti yake ya ukweli yatakuwa sawa, kwa hivyo kama sentensi moja ni ya ukweli, vilevile nyingine basi itakuwa ni kweli.
Kwa mfano:
1) ‘Msichana huyu ni mrembo.’
2) ‘Banali huyu ni mrembo. ’
Kauli hizi zina maana sawa kwa sababu msichana pia anaitwa Banati, kauli ya kwanza ni ya kweli, na ya pili vilevile ni ya kweli. Proposisheni zinazotokana na kauli hizi ni za kweli ambazo ni:
1) Kuna msichana ambaye yumo mahali fulani.
2) Msichana mwenyewe ni mrembo.
3) Msichana kwa jina lingine pia huitwa banati.
MAANA KATIKA SENTENSI
Fodor (1977:27-28) anascma kuwa ili kueleza maana ya sentensi ni vyema kuainisha uwezo wake katika ilokusheni na proposisheni zake.
Hali za kauli tofauti huwa za kweli au za uongo. Mtu anapotoa kauli hujihusisha na ukweli uliopo katika proposisheni ili aweze kudai kuwa ni ya kweli. Vilevile, mtu anapofahamu kauli huelewa kuwa mzungumzaji anadai kuwa kitu ni cha kweli na kisha kukifahamu ni kitu kipi anachokidai kuwa ni cha kweli.
Kwa mfano: ‘Kitabu hiki kitakufaa kwa marejeleo.’
                       ‘Sherehe hiyo ilikuwa nzuri sana.’
Proposisheni hizo, ni za kweli kama:
1) Kitabu ni cha marejeleo wala sio cha kuandikia.
2) Kitabu chenyewe kina ujumbe hasa ninaohitaji kurejelea.
3) Sherehe ilikuwepo.
4) Sherehe yenyewe ilinipendeza mimi.
Kama proposisheni zitakuwa hazitimizi mambo haya yanayodaiwa na kauli hizi, basi zitakuwa ni za uongo.
Proposisheni katika sentensi mara nyingi hurejelea masharti ya ukweli katika kauli.
Palmer (1981:196) anasema kuwa chukulizi ya kimsingi katika sentensi au proposisheni huwa ni za kweli au uongo, lakini ukweli au uongo wake hutegemea mtazamo wa mtu binafsi.
Sentensi ya kweli hueleza jambo kinagaubaga kama lilivyo.
 Kwa mfano: ‘John anampenda Mary.’ Kauli hii ni ya kweli ikiwa John anampenda Mary.
Sentensi hii ina proposisheni kuwa :
1) Kuna msichana kwa jina Mary.
2) Kuna mvulana kwa jina John.
3) Mvulana anampenda
Msichana.
Vilevile katika mfano mwingine unaoafikiana na huu ni:
     ‘Barafu huwa baridi.’
Kauli hiyo, ni ya kweli kwa sababu sote tunajua kuwa barafu ni baridi kwa kuigusa na kuhisi kuwa ina baridi.
Kauli hiyo ina proposisheni kuwa:
1) Kuna kitu kwa jina barafu.
2) Barafu yenyewe huwa ni baridi daima.
Proposisheni yapaswa kutimiza masharti fulani ili iwe ya kweli.
Kwa mfano: ‘‘Nguruwe wana mabawa.’ Kauli hii ni ya uongo kwa sababu, sisi sote tunafahamu kuwa nguruwe hawana mabawa. Nguruwe ni aina ya mnyama na kawaida ya wanyama ni kuwa hawana mabawa. Hatahivyo, kuna Popo ambaye tunafahamu kuwa si ndege wala myama kwani ana mabawa hivyo anafanana na ndege ilhali hujifungua wana kama mnyama. Hivyo basi, proposisheni katika kauli hii si ya kweli hasa kama inamrejelea Nguruwe aliyetajwa katika mfano. Kwa kiasi fulani kuna ukweli kuwa nguruwe ni mnyama, lakini kwa upande mwingine kuna uongo kusema kuwa nguruwe wana mabawa kwani hawana.
Kamau, (2008:50-51), anasema kuwa masharti ya ukweli hutegemea muktadha wake katika matumizi.
Mawasiliano hutumika na kueleweka hasa kupitia kwa proposisheni zake. Mtu akitumia lugha bila kuzingatia baadhi ya sheria za lugha hiyo, mawasiliano hayana matatizo.
Kwa vile; matamshi yanapaswa kuwa sawa na mpangilio wa maneno uwe na mantiki. Anaendelea kusema
kuwa kulingana na wanaisimu masharti ya ukweli yanaweza kubainisha uhusiano uliopo baina ya sentensi yoyote ile na proposisheni yenye mantiki.
Kwa mfano:
1) ‘Karanja ni mrefu zaidi ya Kimani.’
2) ‘Kimani ni mrefu zaidi ya Maina.’
Hivyo basi, ni wazi kuwa Karanja ni mrefu zaidi ya Maina kwa sababu Karanja mwenyewe ni mrefu zaidi ya Kimani ambaye pia ni mrefu zaidi ya Maina.
Basi ni kweli kabisa kusema kuwa Karanja ni mrefu zaidi ya Maina. Vilevile, katika mfano mwingine unaoafikiana na huu.
Kwa mfano:
1) ‘Njoki ni mrembo.’
2) ‘Utamuoa Njoki.’
Hivyo basi, ni bayana kuwa Njoki ni mrembo na ndiye utakaye muoa wewe kwa sababu ni msichana ambaye ni mrembo.
Basi ni kweli kusema kuwa msichana mrembo ambaye utamuoa ni Njoki.
Akimajian na wenzake, (2004:243-244) wanasema kuwa kauli katika lugha huwa na maana halisi na hueleza mambo ya kweli au uongo.
kwa mfano: ‘‘Watu wote ambao ni wagonjwa ni watu.’
                    ‘Gari lile lina rangi nyekundu, hivyo basi ni lekundu.’
                    ‘Baadhi ya watu ambao ni wagonjwa si watu.’
                   ‘Gari lile ni lekundu lakini halina rangi.’
Kauli hizo, zina proposisheni za kweli na za uongo.
Kauli ya kwanza na ya pili ni za kweli kwa sababu watu watabaki kuwa watu hata kama ni wagonjwa.
Vilevile, kama gari ni  lekundu basi lina rangi.
Kauli ya tatu na ya nne ni za uongo kwa sababu watu wakiwa wagonjwa hawabadiliki kamwe, bali huwa ni watu daima hata wakipata afueni.
Vivyo hivyo, haiwezekani kuwa gari lekundu halina rangi kwani tayari imeelezwa kuwa gari lenyewe lina rangi nyekundu.
Mahusiano ya kweli huwa na tabia zake ambapo tabia ya kimsingi ni kuwezesha jambo lingine kutendeka.
Sentensi moja husababisha sentensi nyingine kuwa ya kweli ikiwa ukweli wa sentensi ya kwanza umehakikishwa kuwa upo.
Vilevile, sentensi moja husababisha sentensi nyingine kuwa ya uongo kama uongo wa sentensi ya kwanza umehakikishwa kuwa upo.
Kwa mfano:
1) “John ni kapera.’
2) “John hajaoa.’
Proposisheni iliyo katika kauli ya kwanza, yasababisha kuwepo kwa proposisheni katika kauli ya pili. Kapera ina maana ya mwanamume ambaye yumo katika umri wa kuoa lakini hajaoa. Kauli hizi zina proposisheni kuwa:
1) Kuna mtu anayejulikana kwa jina John.
2) John mwenyewe hajaoa.
3) Kutooa kwa John kunamfanya yeye kuwa kapera.
Hivyo basi, proposisheni zilizopo juu ni za kweli kwani kama John ni kapera basi hajaoa. Katika mfano mwingine unao ambatana na huu.
Kwa mfano:
 1) “Sindano nifupi mno.’
2) “Sindano haina urefu wa kutosha.’
Ukweli uliopo katika kauli ya kwanza wahakikisha ukweli kuwepo katika kauli ya pili. Kauli hizi zina proposisheni kuwa kama sindano ni fupi mno ni kweli kuwa haina urefu wa kutosha.
Fasold (2006:142) anasema kuwa maana katika sentcnsi ni proposisheni. Proposisheni ni wazo lililotimia,
ni kauli anibayo yaweza kuwa ya kweli au uongo. Proposisheni ni ya kweli kama kiarifu chake kinaeleza sawasawa kinachorejelewa na kiima. 
Kwa mfano: ‘Catherine Ndereba alikimbia kwa kasi na kushinda mbio hizo.’
Kauli hiyo ina proposisheni kuwa:
1) Runa mwanariadha kwa jina Catherine Ndereba.
2) Mwanariadha mwenyewe alikimbia kwa kasi sana.
3) Mwanariadha huyo alijipatia ushindi katika mbio hizo alizoshiriki.
Mwanariadha kwa jina la Catherine Ndereba arnbaye alikimbia kwa kasi, kisha akawa mshindi katika mbio hizo alizoshiriki, itakuwa ni ya kauli ya kweli kama alishiriki katika mbio hizo na kushinda, ilhali itakuwa ni ya uongo kama hakushiriki kamwe katika mbio hizo.
Masharti ya ukweli ni muhimu kwani huunganisha jambo analojifunza mtu na jambo linalosemwa, kwa sababu nikitoa kauli kama niliyoitaja hapo kumhusu Catherine Ndereba huna budi kuamini kuwa ni mwanariadha na aliwahi kuwa mshindi katika mbio alizoshiriki.
Fretheim (2000:39-40) anasema kuwa kauli hukusudia kumfahamisha msikilizaji ujumbe alio ukusudia msikilizaji na kuwa anao uhakika fulani kuhusu proposisheni itakayofahamika kupitia kwa kauli aliyoitamka. Maelezo tofauti hutumika kurejelea proposisheni moja ambayo huelezwa kwa kauli tofautitofauti.
Kwa mfano:
1) ‘Maria hawezi kumsaidia Piera kupata kazi.’
2) ‘Maria anasema kuwa hawezi kumsaidia Piera kupata kazi.’
3) ‘Maria anaamini kuwa hawezi kumsaidia Piera kupata kazi.’
4) ‘Maria anajuta kuwa hawezi kumsaidia Piera kupata kazi.’
 
Kauli hizo ni za kweli kwani zaeleza hisia za Maria kumhusu Piera. Maria haoni uwezekano wowote kamwe
wa kumsaidia Piera kupata kazi. Kauli hizi zina proposisheni ya Maria kutomsaidia Piera kupata kazi kamwe, ambapo jambo hili limeelezwa kwa njia anuwai. 




MAREJELEO
Abraham, S. (1996). A Theory o f Structural Semantics’. Mouton and Company Publishers.
Akmajian, A. na Wenzake. (2004) Linguistics. An lntrodution to Language and Communication. Fifth
Edition: MIT Press, Cambridge.
Atichi, A.R. (2004) The Semantic Distinctiveness of Kenyan English: UON. Unpublished MA Thesis.
Atoh, F.O. (2001) Semantics Analysis of Dholuo Nowns: The Semantics Field Approach. UON. Unpublished MA Thesis.
Blass, R. (1990) Relevance Relations in Discource. A Study in Special Reference to Sissala: Cambidge University Press.
Brown, G. na Yule, G. (1983) Discource Analysis: Cambridge University Press.
Bussman, H. (1996) Route ledge Dictionary o f Language and Linguistics: International Thompson Publishing Company.
Cambridge (2008) Cambridge Advanced Learners Dictionary. Cambridge University.
Carston, R. (2002) Thoughts and Utterances. The Pragmatics of Explicit Communication. MA: Blackwell Publishers Ltd.
Comford, F. M. (1957) Platos Theory o f Knowledge: Routeledge and Kegan Paul Ltd.
Crystal, D. (2003) A Dictionary o f Linguistics and Phonetics. Fifth Edition. Oxford: Blackwell Publishers.
Falsod, R. W. (2002) An lntrodution to Language and Linguistics. Cambridge University Press.
Fleming, (1998) Google Search. Powered by The Ultimate Programming Weblog. Sillntematinal: 

http:// worldnet Princeton. Edu/Pert/Webwn.
Fodor, J. D. (1997) Semantics: Theories o f Meaning in Generative in Generative Grammar:
Harper and Row , Publishers.
Fretheim, A. (2000) Pragmatic Markers and Propositional Attitude: John Benjamin Publishing Company.
Green, G. M (1996) Pragmatics and Natural Language Understanding. Second Edition: Lawrence Erlbaum Associates Publishers.
Greenbaum, S. na Wenzake. (1985) A comprehensive Grammar o f English Language: Longman Group UK Ltd.
Griffin, E. M (1991) A First look at Communication Theory. Wheaton College: Me Graw- Hill,
Inc. Company.
Hofmann, T. R. (1993) Realms o f Meaning: An Introduction to Semantics: Longman Group UK
Ltd.
Ifantidou, E. (2001) Evidentials and Relevance. Volume 86: John Benjamin Publishing
Company.
Kamau, S. K. (2008) An Analysis o f Truth Conditions in Pragmatics: Relevance Theory
A p p r o a c h . UON. Unpublished MA Thesis.
Kasher, A. (1998) Pragmatics. Critical Concepts. Volume V: Communication, Interaction and Discourse: Routeledge Publishers.
Katie, W. (2001) A Dictionary o f Stylistics: Longman Group UK Ltd.
Katz, J.J. (1977) Propositional Structure and Illocutionary Force. A Study of the contribution of Sentence meaning and Speech Acts: The Harvest Press.
Kempson, R. M. (1975) Pressuposition and The Delimination o f Semantics: Cambridge University Press.
Larson, M. L. (1984) Meaning-Based Translation: A Guide to Cross-Language Eqivalence: University Press of
America, Inc.
Leech, G. (1974) Semantics: Penguin Books Limited.
Leech, G. N. (1971) Towards a Semantic Description o f English: Longman Group Ltd.
Linsky, L. (1952) Semantics and the Philosophy o f Language: University of Illinois Press.
Longmans (1968) Longmans English Larousse: Longmans, Green and Co. Ltd.
Munga, C. M. (2009) Sence Relations in Gikuyu: A Lexical Pragmatics Approach. UON
Unpublished MA Thesis.
Ndug’u, M. N. (2009) Mada na Fokasi katika Kiswahili: Mtazamo wa Muundo wa Taarifa.
UON. Unpublished MA Thesis.
Ogola, C. A. (2006) A Pragmatic Analysis of Intercultural Communication Failures. UON,
Unpublished MA Thesis.
Palmer, F. R. (2006) An Introduction to Language and Linguistics: Cambridge University Press.
Rouchota, V, na Jucker, H. (1998) Current Issues in Relevance Theory: John Benjamin
Publishing Company.
Saeed, J. L. (2003) Semantics. Second Edition: Blackwell Publishing Ltd.
Schroeder, H. (2005) Do we Speak the same Language? A cognitive Pragmatic Explanation of
Cultural Misunderstanding. In Across Borders: Benefiting from Cultural Differences.
Conference Proceedings. 17^-18th March: 2005.
Sperber, D na Wilson,
D. (1995) Communication and Cognition, 2nd Edition: Blackwell Publishers.
Sperber, D na Wilson,
D. (2004) A Handout on Relevance Theory (1985-2002): Blackwell Publishers.
Tuki (1990). Kamusi ya Isimu na Lugha. Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili: Educational Publishers and
Distributors Ltd.
 
Tuki (2006) English-Swahili Dictionary. Third Edition: Book Printing Services Ltd.



Chanzo>>>>>>