MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI - UCHAMBUZI WA WIMBO WA “KWANGWARU”

JIFUNZE KISWAHILI

Full Version: UCHAMBUZI WA WIMBO WA “KWANGWARU”
You're currently viewing a stripped down version of our content. View the full version with proper formatting.
MSANII: HARMONIZE FT DIAMOND PLATNUMZ
WIMBO: KWANGWARU
UTANGULIZI
Wimbo wa “Kwangwaru” ni wimbo ulioimbwa na Harmonize akishirikiana na Diamond Platnumz wote ni wasanii kutoka lebo ya WCB Tanzania. Tahakiki hii imejikita zaidi katika vipengele vya maudhui na siyo vipengele vya fani.

DHAMIRA KUU
Dhamira kuu katika wimbo wa Kwangwaru ni MAPENZI.
Msanii anajielekeza kumpamba na kumwelezea mpenzi wake maneno matamu kuhusu mapenzi. Msanii anamweleza na kumuasa mpenzi wake mambo kadha wa kadha ambayo msanii anaamini akifanyiwa na mpenzi wake ataridhika na kutulia zaidi ya yote kudumu katika mapenzi. Msanii anaeleza ujuzi ambao mwanamke wake akimpatia faragha atadumu na kuyafanya mahusiano yao yawe yenye amani.

Msanii anaanza kwa kumpatia mpenzi wake maneno matamu na ahadi kedekede. Msanii anasema kama angekuwa na pesa angeweza kumhonga mpenziwe vitu vya thamani sana. Anamuasa mpenzi wake asilaghaike na wenye pesa kwani wanamlaghai tu, msanii anasema “…usiwaamini, ukishawapa wanakwenda…”
Msanii anajiapiza kwa mpenziwe kwamba anampenda na hakuna atakaye mpenda zaidi yake.
Msanii anasema “…wakija wapoteze jifanye kama huwaoni…”. Msanii anamuasa mpenzi wake asijaribu kumsaliti wala kumuudhi kwani msanii anakiri wazi kuwa hana moyo wa msamaha endapo atasalitiwa hili linajidhihilisha pale ambapo msanii anasema “… moyo wangu mwarobaini u mchungu ukiudhiwa…samehe mara sabini huo uzungu sijaumbiwa…”

Msanii anajaribu kuishirikisha jamii ujuzi wake katika mapenzi ya faragha kwa kutumia lugha ya mnato na ya mficho mno. Msanii anatumia tafsida kuelezea mapenzi ya faragha na zaidi tendo la “ngono”.
Msanii anatumia sentensi kama
“… nikumbate baridini…”
“…nipatie vya kitandani nipe mpaka kwenye kiti…”
“…kitandani nikoleze kwa miuno ya kingoni…”
“…kisha uniongeze ulivyofunzwa unyagoni…”
“…weka mate niteleze kama nyoka pangoni…”.
Msanii anaeleza yote hayo ambayo anaamini kama atafanyiwa na mpenzi wake basi atatulia na hataweza kumsaliti.

MAPENZI YA DHATI
Dhamira ya mapenzi ya dhati imejitokeza kwa msanii kumuasa mpenzi wake asimsaliti kama yeye ambavyo hata msaliti. Msanii anahitaji kuthaminiwa na kuhudumiwa ipasavyo na mpenzi wake na kwamba yupo tayari kutoa chochote kile ili tu kudumisha mahusiano hayo.
NAFASI YA MWANAMKE KATIKA JAMII
Msanii amemchora mwanamke kama chombo cha starehe cha kumfurahisha mume. Mambo mengi ambayo anayahitaji msanii kutoka kwa mpenzi wake ni mambo ambayo yanalenga zaidi kumstarehesha mwanaume na kumridhisha kimapenzi. Mwandishi anamtaka mpenzi wake aoneshe ujuzi wa hali ya juu aliofunzwa unyagoni tena ” ujuzi wa kingoni”.
Msanii anamchora mwanamke kama mtu mwenye tamaa ya pesa na mali na ambaye anashawishika kirahisi kwa umaarufu wa mwanaume. Hili linajidhihirisha pale msanii anaposema kama angekuwa na pesa angemhonga vya thamani pia anasema “…ama niwe fundi wa kuigiza kama kanumba, masanja, joti usiwe mbali nami…”.
IMANI NA FALSAFA YA MSANII
Msanii anaamini kama mwanamke na mwanaume watatimiza wajibu wao ipasavyo katika mapenzi basi mapenzi yatadumu na hakutakuwepo na kusalitiana.

KUFAULU KWA MSANII
Msanii amefaulu kuelezea hisia zake kwa namna ya pekee mno. Ujumbe wake rahisi kueleweka kwa jamii ya sasa ambayo wengi wa wapenzi wa kazi zake ni vijana hivyo dhamira ya mapenzi ni muafaka japo angeweza kuzungumzia dhamira zingine kama uchapakazi na kujituma.

KUTOFAULU KWA MSANII
Msanii amejenga imani yake katika dhana ya kusadikika kwamba mwanaume anatulia katika mapenzi kwa kuridhishwa na mpenzi wake jambo ambalo halina ushahidi wa kutosha kuwa wanaume wanaosaliti mahusiano yao hawaridhishwi.

Msanii anasema kwamba hawezi kusamehe saba mara sabini na kwake anaona kufanya hivyo ni ” uzungu”. Hii inaweza kuleta picha ya kwamba msanii anahamasisha watu kukosa uvumilivu na ustahimilivu katika mapenzi.