07-04-2021, 04:08 PM
Katika mofolojia ya Kiswahili nomino zinaundwaje? Fafanua kwa majibu yako kwa mifano
MAJIBU
Kuna taratibu mbalimbali zinazotumika katika kuunda nomino. Baadhi yake ni kama vile:
▪ Kuongeza kiambishi mwanzoni mwa kitenzi.
Mifano:
– (Ku)taka: mtaka
– (Ku)tema: mtema
– (Ku)tafiti: mtafiti
– (Ku)asi: mwasi
▪ Kuongeza viambishi mwishoni mwa kitenzi
Mifano:
– (Ku)badili: badiliko
– (Ku)abiri: abiria
– (Ku)afiki: afikiano
▪ Kubadilisha kiambishi mwishoni mwa vitenzi.
Mifano:
– (Ku)bikiri: bikira
– (Ku)hudumu: huduma
– (Ku)faidi: faida
– (Ku)fedhehi: fedheha
▪ Kubadilisha viambishi katikati ya kitenzi.
Mifano:
– (Ku)haribu: har«a»bu
– (Ku)safiri: sa«fa»ri
▪ Kutobadilisha chochote.
Mifano:
– (Ku)dai: dai
– (Ku)hesabu: hesabu
MAJIBU
Kuna taratibu mbalimbali zinazotumika katika kuunda nomino. Baadhi yake ni kama vile:
▪ Kuongeza kiambishi mwanzoni mwa kitenzi.
Mifano:
– (Ku)taka: mtaka
– (Ku)tema: mtema
– (Ku)tafiti: mtafiti
– (Ku)asi: mwasi
▪ Kuongeza viambishi mwishoni mwa kitenzi
Mifano:
– (Ku)badili: badiliko
– (Ku)abiri: abiria
– (Ku)afiki: afikiano
▪ Kubadilisha kiambishi mwishoni mwa vitenzi.
Mifano:
– (Ku)bikiri: bikira
– (Ku)hudumu: huduma
– (Ku)faidi: faida
– (Ku)fedhehi: fedheha
▪ Kubadilisha viambishi katikati ya kitenzi.
Mifano:
– (Ku)haribu: har«a»bu
– (Ku)safiri: sa«fa»ri
▪ Kutobadilisha chochote.
Mifano:
– (Ku)dai: dai
– (Ku)hesabu: hesabu