09-28-2022, 06:01 AM
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO "DAFRAO''
Neno *dafrao* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino: [Ngeli: i-/zi-*] yenye maana zifuatazo:
1. Tukio la kugongana uso kwa uso kwa vyombo vinavyotembea.
2. Chuma kigumu kinachofungwa Mbele ya gari ili kuzuia uharibifu wakati magari yanapogongana.
Neno hili *dafrao* linatokana na neno la Kiarabu *dafraau دفراء* na lenye maana zifuatazo:
1. Kilichodhalilika.
2. Kitu kilichooza, kikanuka na kutoa wadudu.
3. Aina ya mmea wa kitropiki. Kwa Kiingereza huitwa *scoparia.*
Kinachodhihiri ni kuwa neno *dafraau دفراء* lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *dafrao* maana yake kati lugha ya asili - Kiarabu ilibadilika na kupata maana mpya zilizotajwa.
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*
Neno *dafrao* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino: [Ngeli: i-/zi-*] yenye maana zifuatazo:
1. Tukio la kugongana uso kwa uso kwa vyombo vinavyotembea.
2. Chuma kigumu kinachofungwa Mbele ya gari ili kuzuia uharibifu wakati magari yanapogongana.
Neno hili *dafrao* linatokana na neno la Kiarabu *dafraau دفراء* na lenye maana zifuatazo:
1. Kilichodhalilika.
2. Kitu kilichooza, kikanuka na kutoa wadudu.
3. Aina ya mmea wa kitropiki. Kwa Kiingereza huitwa *scoparia.*
Kinachodhihiri ni kuwa neno *dafraau دفراء* lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *dafrao* maana yake kati lugha ya asili - Kiarabu ilibadilika na kupata maana mpya zilizotajwa.
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*