MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI - ETIMOLOJIA YA NENO "UJUMI''

JIFUNZE KISWAHILI

Full Version: ETIMOLOJIA YA NENO "UJUMI''
You're currently viewing a stripped down version of our content. View the full version with proper formatting.
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO "UJUMI''

Neno *ujumi* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino: [Ngeli: u-/u-*] yenye maana zifuatazo:
1. Kanuni zinazohusu ubora na ubaya wa kazi ya sanaa.(Vyanzo: *Kamusi ya Karne ya 21* na *Kamusi ya Kiswahili Sanifu - TUKI*).

2. Tathmini inayobainisha ubora au ubaya wa kazi za sanaa. (Chanzo: *Kamusi Kuu ya Kiswahili*).

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *ujumi* linatokana na neno la Kiarabu *ujmu* ( *soma: ujmun/ujman/ujmin عجم*) wingi wa neno la Kiarabu *a-ajamiyyu (a-ajamiyyun/a-ajamiyyan/a-ajamiyyin اعجمي)* lenye maana zifuatazo:

1. Mtu asiye fasaha katika kuzungumza aghalabu lugha ya Kiarabu hata kama ni mwarabu.

2. Asiye mwarabu, mtu wa Uajemi (Iran); muajemi.

3. Mtu asiyeweza kusema; bubu.

4. -siyo na mlio/sauti aghalabu mawimbi au bunduki.

Kinachodhihiri ni kuwa neno *ujmun  عجم* lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *ujumi* lilichukua maana mpya *kanuni zinazohusu ubora na ubaya wa kazi ya sanaa, tathmini inayobainisha ubora au ubaya wa kazi za sanaa* na kuacha maana za neno hili katika lugha ya Kiarabu.

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*