MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI - ETIMOLOJIA YA MANENO 'AKARABU/AKRABU'

JIFUNZE KISWAHILI

Full Version: ETIMOLOJIA YA MANENO 'AKARABU/AKRABU'
You're currently viewing a stripped down version of our content. View the full version with proper formatting.
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA MANENO 'AKARABU/AKRABU'

Neno *akarabu* hutamkwa pia *akrabu* katika lugha ya Kiswahili lina maana zifuatazo:

1. *Nomino [Ngeli: i-/zi-]* mshale katika uso wa saa unaoonyesha ama saa, dakika au sekunde.

2. *Nomino [Ngeli: i-/zi-]* mshale unaoonyesha uzito katika mizani.

3. *Nomino [Ngeli: i-/zi-]* mshale unaoonyesha upande fulani katika uso wa dira.
Msemo: *Akarabu/Akrabu Kaskazini:* Upande wa Kaskazini.

4. *Nomino [Ngeli: i-/i-]* mkusanyiko wa nyota unaofanya umbo la *nge* angani.

5. *Nomino [Ngeli: i-/i-]* alama ya nge katika mfumo wa unajimu wa kutumia nyota.

Katika lugha ya Kiarabu, neno *akarabu/akrabu* limekopwa kutoka nomino ya Kiarabu  *aqarabun/aqaraban/aqarabin عقرب* yenye maana zifuatazo:

1. Mdudu mdogo mwenye sumu nyingi anayechoma kwa mwiba wa sumu ulio katika ncha ya mkia wake.

2.  Moja ya nyota zilizo angani iliyo kati ya nyota za *Mizani* na *Mshale* na wakati wake unaanzia  tarehe 24 Oktoba hadi tarehe  21 Novemba.

3. Aina ya samaki mwenye kichwa kikubwa ambaye hupatikana katika *Bahari ya Kati* (Bahari ya Mediteranea).

4. Mikanda ya viatu aina ya Kandambili.

Kinachodhihiri ni kuwa neno hili *aqarabun/aqaraban/aqarabin عقرب* ) lilipokopwa na kutoholewa kuwa neno *akarabu/akrabu* lilichukua baadhi ya maana za lugha ya asili - Kiarabu na kuacha maana zingine na pia lilipata maana mpya ya upande
*Akarabu/Akrabu Kaskazini:* Upande wa Kaskazini.

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*