MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI - ETIMOLOJIA YA MANENO ' RIZIKI' na 'ARZAKI'

JIFUNZE KISWAHILI

Full Version: ETIMOLOJIA YA MANENO ' RIZIKI' na 'ARZAKI'
You're currently viewing a stripped down version of our content. View the full version with proper formatting.
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA MANENO ' RIZIKI' na 'ARZAKI'

Neno *riziki* katika lugha ya Kiswahili ni nomino [ *Ngeli: i-/zi-]* yenye maana zifuatazo:

1. Mahitaji ya msingi kama vile chakula anachopata mtu aghalabu baada ya kufanya kazi; malipo, ujira.

2. Baraka anazopata mtu katika maisha kutoka kwa Mwenyezi  Mungu; neema.

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *riziki* limetokana na neno la Kiarabu *rizqun* (soma: *rizqun/rizqan/rizqin رزق* ) lenye maana zifuatazo:

1. Kila kinachomnufaisha mtu kama vile chakula na mavazi.

2. Kinacholiwa kikafika tumboni; kilichoruzukiwa, marzuuq مرزوق maruzuku.

3. Mvua, sababu ya kupatikana chakula.

4. Ujira anaolipwa mtu kwa kazi aliyoifanya; mshahara.

3. Upole na huruma.

4. Moyo wa huruma.

5. Anachoruzukiwa mtu na Mwenyezi Mungu.

Kinachodhihiri ni kuwa neno hili ( *rizqun/rizqan/rizqin رزق*) lilipoingia katika lugha ya Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *riziki*  maana yake katika Kiarabu haikubadilika.

Neno *arzaki* katika lugha ya Kiswahili ni nomino [ *Ngeli: i-/zi-]* iliyo wingi wa neno riziki.

Neno hili *arzaki* (soma: *arzaaqun/arzaaqan/arzaaqin ارزاق* ) katika lugha ya  Kiarabu ni wingi wa neno 'rizqun' kama lilivyofafanuliwa hapo juu.

Kinachodhihiri ni kuwa neno hili *arzaaqun*(soma: *arzaaqun/arzaaqan/arzaaqin ارزاق*) lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *arzaki* maana yake katika lugha asili - Kiarabu haikubadilika.

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*