MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI - YA KALE YA KUKUMBUKWA! UPAMBAUKAO HUTWA (KWAHERINI)

JIFUNZE KISWAHILI

Full Version: YA KALE YA KUKUMBUKWA! UPAMBAUKAO HUTWA (KWAHERINI)
You're currently viewing a stripped down version of our content. View the full version with proper formatting.
YA KALE YA KUKUMBUKWA!
  UPAMBAUKAO HUTWA
         (KWAHERINI)

1. Upambaukao hutwa, na kutwapo huwa giza,
Mtana hupetwa petwa, ukanyang'anywa mwangaza,
          *Yaliza haya yaliza!*

2. Na sisi ule mtana, uliotupambauza,
Ulotupa kujuana, na mengi kuyafanyiza,
Leo waanza kununa, mitima kuiumiza,
          *Laliza hili laliza!*

3. Hikumbuka tangamano, vyema tulivyolikuza,
Mi nanyi 'kawa mfano, wa lulu katika chaza, 
Kisha leo saa hino, hiona twalikatiza,
            *Laniliza! Laniliza!*

4. Hikumbuka ukarimu, na wema wenu nduguza,
Jinsi mulivyonikimu, myaka saba hatimiza, 
Nahisi najidhulumu, Tanzania kuipeza,
          *Ndipo hamba laniliza*

5. Ingawa menilazimu, na nyinyi kujiambaza,
Yondokayo ni sehemu, sehemu najibakiza,
Moyo wangu umo humu, Tanzania 'tausaza,
          *Japo hivyo laniliza!*

6. Ni yangu matumaini, kwenu nayapendekeza,
Kwamba hwenda si jioni, nuru ingajipunguza,
Pengine wingu angani, ndilo lilojitandaza,
            *Litakoma kutuliza?*

7. Na iwapo si hakika, hili nilowaambiza,
Jambo moja liso shaka, tusoweza lipuuza,
Utwao hupambauka, hauwezi ukaiza,
          *Hapo halitatuliza.*

*ABDILATIF ABDALLA,*
*S.L.P. 35110,*
*DAR ES SALAAM.*
*SEPTEMBA 8, 1979.*

*NA KUCHAPO LITAKUCHWA*
( *KWA HERI YA KUONANA* )

1. Na kuchapo litakuchwa, likafungamana giza,
Na mchana ukaachwa, usiku ukajikweza,
Asubuhi ikafichwa, jioni ikatokeza,
  *Yasikulize nyamaza.*

2. Nyamaza yasikulize, tuombeane Muweza,
Mitima aitulize, mapenzi kutujaliza,
Kwako kwetu atujaze, ya heri kutueneza,
  *Usijilize nyamaza.*

3. Pia nasi kwa mfano, kwako tukielekeza,
Tuwazapo kongamano, kwenye yale mabaraza,
Kwenye mbinu kwenye ngano, machozi watwambukiza,
      *Ndipo nasema nyamaza.*

4. Sisahau umuhimu,  mengi umeniongoza,
Hasa kwa ile sehemu, diwani nilimaliza,
Ya mwenzetu marehemu, *Nyamaume* kuikuza,
    *Nyamaza bwana nyamaza.*

5. Kilio hiki si chako, ni changu unaniliza,
Na giza hili si lako, ni langu lanikwamiza,
Mayonzi haya si yako, ni yangu yaniumiza,
        *Ukilia waniliza.*

6. Kwa heri sisemi nenda, na siwezi kukataza,
Wendapo naona inda, nagubikizwa na kiza,
Nina nyang'anywa uwanda, uga gani nitacheza,
      *Hapo kulia nyamaza.*

7. Wendako usisahau, nyuma kututumbuiza,
Kwa salamu angalau, heba ukatuliwaza,
Wemao hatusahau, buriani nanyamaza,
    *Wacha kulia nyamaza.*

*SHAABAN C. GONGA,*
*S.L.P. 9031,*
*DAR ES  SALAAM.*
*09 - 09 - 1979.*

*USHAIRI HARIJOJO?*
1. Kwa isimuye Rabana, Muumba na Muumbule,
Aliyeumba mchana, usiku uufatile,
Naomba kwake auna,  nudhumu niipangile,
*Wapi ushairi ule, umekwenda harijojo?*

2. Ushairi wa maana, tulorithi kwa wakale,
Wenye mizani na vina, maudhui yatimile,
Urari, lugha mwanana, Kiswahili kiso ndwele,
*Wapi ushairi ule, umekwenda harijojo?*

3. Ushairi wenye taji, walotufunza wavyele,
Ulosheheni umbuji, na hekima teletele,
Si leo wa mfa maji, anayepiga kelele,
*Wapi ushairi ule, umekwenda harijojo?*

4. Beti nne kaditama, ukomo niufikile,
Mtima unaniuma, pingiti nizionile,
Zimetanda zinavuma, ni shangwe vigelegele!
*Wapi ushairi ule, umekwenda harijojo?*

*KHAMIS S.M. MATAKA,*
*S.L.P 70249,*
*DAR ES SALAAM.*
*18 - 09 - 2003.*