MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI - UHUSIANO WA FANI NA MAUDHUI KWA MUJIBU WA WATAALAMU MBALIMBALI

JIFUNZE KISWAHILI

Full Version: UHUSIANO WA FANI NA MAUDHUI KWA MUJIBU WA WATAALAMU MBALIMBALI
You're currently viewing a stripped down version of our content. View the full version with proper formatting.
UHUSIANO WA FANI NA MAUDHUI KWA MUJIBU WA WATAALAMU MBALIMBALI
Uhusianoa wa fani na maudhui umekuwa ukiangaliwa na wanazuoni wa fasihi katika mitazamo tofauti, mtazamo mkuu unaoangaliwa na wanazuoni katika uhusiano wa fani na maudhui umo katika makundi makubwa mawili ya kimtazamo. Makundi hayo ni ya mtazamo wa KIYAKINIFU na mtazamo wa KIDHANIFU.
A: Mtazamo wa kidhanifu.
 Wanazuoni wanaoegemea katika mtazamo huu hudai kuwa fani na maudhhui havina uhusiano wowote. wanaagalia uhusiano wa vijenzi katika utengano ambao fani inaweza kujikamilisha bila ya kutegemea maudhui na maudhui pia huweza kujikamilisha bila ya kutegemea fani.
Wanaeleza uhusiano wa fani na maudhui kuwa ni sawa na ule wa kikombe na maji au chai iliyomo ndani ya kikombe hicho. Baadhi ya wananadharia hao wanahusisha mahusano haya na yale ya sehemu ya ganda la chungwa lililo nje ya nyama ya chungwa. Wanazuoni wanaoungana mkono na nadharia na mtazamo huu ni hawa.
Fr.F.M.V NKWERA
Nkwera anadai kuwa fani na maudhui havina uhusiano wowote kwa kufananisha na maziwa na kikombe. Kikombe anakiona na kukichukulia kama chombo kinachotumika kuhifadhi maziwa. Hivyo kikombe anakifananisha na fani kuwa ni umbo la nje la kazi ya fasihi. Maziwa anayafananisha na maudhui kuwa ni umbo la ndani la kazi ya Fasihi. Kwa madai yake ni kuwa maziwa yanaweza kutenganishwa na kikombe na kila kimoja kubaki peke yake.
S.D. KIANGO NA T.S.Y. SENGO.
Wanazuoni hawa pia wanaunga mkono mtazamo wa kidhanifu, wanadai kwamba fani na maudhui havina uhusiano wowote katika kazi ya fasihi.Wanazuoni hawa wanafananisha fani na maudhui sawa na chungwa kwa madai kwamba chungwa linaweza kutenganishwa na nyama ya ndani ya chungwa inayoliwa ambayo inafananishwa na maudhui ambalo ndilo umbo la ndani la kazi ya Fasihi. Aidha wanafananisha maganda ya chugwa yanayomenywa ili kupata  nyama ya ndani ya chugwa  sawa na fani ambalo ni umbo la nje la kazi ya Fasihi.
Madai hayo ni kwamba kwa kuwa magamda ya chugwa yanaweza kutenganishwa na nyama ya ndani ya chugwa basi hata fani na maudhui katika kazi ya fasihi vinaweza kutenganishwa na kila kimoja kusimama katika upekee wake. Hivyo, wanadai fani na maudhui havina uhusiano.
PENINA MUHANDO NA NDIYANAO BALISIDYA
Wanazuoni hawa nao wamo kwenye kundi hili la wenye mtanzamo wa kidhanifu, madai yao makubwa kuhusu mahusiano ya fani na maudhui ni kwamba fani katika  kazi ya fasihi ni umbo la ndani basi kwa hali hiyo fani na maudhui vinaweza kutenganishwa kwa hiyo fani na maudhui havina uhusiano kwa vile kila kimoja kinaweza kusimama peke yake.
UDHAIFU WA MTAZAMO HUO
Udhaifu unaojitokeza katika mtazamo huu ni ule wa kutazama fani na maudhui kwa mtazamo wa utengano hili ni kosa kubwa sana kwa kutenganisha vile ambayo havitenganishwi.
B : Mtazamo wa kiyakinifu
Wanazuoni wa fasihi wanaoegemea katika mtazamo huu wanadai kwamba fani na maudhui hutegemeana, huathiriana na kukamilishana. Wanazuoni wanaounga mkono mtazamo huu ni kama vile;
M.M.MULOKOZI NA K.K.KAHINGI
Wanazuoni hawa wanadai kuwa fani na maudhui haviwezi kulingana na kuathiriana unaposoma kazi ya fasihi kwa kupata miundo, matendo, madhari, wahusika na matumizi ya lugha. Hivi ni vipengelele vilivyomo ndani ya fani ndipo msomaji anaweza kupata maudhuni ya kazi ya mwandishi kama vile dhamira, ujumbe (fundisho), falsafa ya mwandishi, msimamo na mtazamo wake kwa hivyo basi huona kwamba fani hutegemea maudhui na maudhui ya fasihi hutegemea fani hivyo, fani  na maudhui haviwezi kutenganishwa kwani hutegemeana na kuathiriana kama tulivyoona hapo juu.
 F .E.SENKORO.
Mwanazuoni huyu pia anaungana na wanazuoni wa mtazamo wa kiyakinfu wanaodai kwamba fani na maudhui haviwezi kutenganishwa. Senkoro katika madai  yake anafananisha uhusiano wa fani na maudhui kama sarafu yenye sura mbili mfano wa sarafu ya shilling 200 yatanzania ili iweze kukamilika na kuwa yenye matumizi halali katika serikali halali ya tanzani inalazimika kuwa na picha ya karume na kuwa upande wa pili kuwa na picha ya simba na mtoto wake kutokuwepo au kukamilika sura moja ya sarafu hiyo basi sarafu hiyo haziwezi kutumika kama sarafu halali.
Kwa hali hiyo inamaanisha kwamba upande mmoja wa sarafu huwa ni sawa na kufananisha na maudhui katika kazi ya Fasihi. Hivyo basi ili sarafu ikamilike ni lazima pande mbili zikamilike na hiyo ndiyo hali iliyopo katika fasihi kwamba ni lazima fani na maudhui kukamilishwa ndipo kazi ya fasihi hukamilika na huwezi kutenganisha fani na maudhui.
Mambo muhimu yanayojitokeza katika fani ni.
  • Muundo – mtiririko wa mawazo na matukio.
  • Wahusika
  • Mtindo –  mbinu za kiuandishi
  • Uteuzi wa maneno
  • Picha za ishra
Wakati katika maudhui vitu vinavyojitokeza huwa ni:-
  • Dhamira
  • Ujumbe
  • Falsafa
  • Migogoro
  • Mtazamo
  • Msimamo wa mwandishi.
Kwa kuhitimisha basi fani na maudhui haiwezi kutenganishwa kwani hutegemeana, huathiriana na kukamilishana. Fasihi kama tunavyoona inajegwa na maumbo mawili ambayo ni fani na maudhui.