MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI - ETIMOLOJIA YA NENO 'AHERA/AKHERA'

JIFUNZE KISWAHILI

Full Version: ETIMOLOJIA YA NENO 'AHERA/AKHERA'
You're currently viewing a stripped down version of our content. View the full version with proper formatting.
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'AHERA/AKHERA'

Neno *ahera/akhera* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino: [Ngeli: i-/-zi*] yenye maana ya:

1. Mahali panapoaminiwa kuwa ndiko roho za wafu zinakoenda.

2. Maskani ya roho za wanadamu baada ya mauti/kifo.

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *ahera/akhera*( *soma: aakhiratun/aakhiratan/,aakhiratin آخرة )* ni nomino ya Kiarabu yenye maana zifuatazo:

1. Kinyume cha Dunia. Kuna aya katika Qur'aan Tukufu isemayo: "Miongoni mwenu wapo wanaoitaka Dunia, na miongoni mwenu wapo wanaoitaka Akhera." (Qur'aan Tukufu, Sura ya 3 (Surat Aali Imraan, Aya ya 152).

2. Kinyume cha mwanzoni; mwishoni.

3. Maskani ya roho za wanadamu baada ya kifo.

Kinachodhihiri ni kuwa neno hili *aakhira* lilipoingia katika  Kiswahili na kutoholewa limezoeleka kutamkwa *ahera* na *akhera* likibeba maana moja ya maskani ya roho za wanadamu baada ya kifo.

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*