MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI - SHAIRI: USIONE UKADHANI

JIFUNZE KISWAHILI

Full Version: SHAIRI: USIONE UKADHANI
You're currently viewing a stripped down version of our content. View the full version with proper formatting.
Dunia rangi rangile, methali hii muhimu
Usione jambo lile, ukadhani la dawamu
Kila chombo na wimbile, hilo mwenzangu fahamu
Usione ukadhani
Usione mtu yule, hana maisha matamu
Ukamsonda kwa ndole, kama kaila haramu
Aso hili ana lile, nakujuza muadhamu
Usione ukadhani
Ati kamaliza shule, ana vyeti kemkemu
Aranda huku na kule,mithili mwenye wazimu
Hawi wa hivyo milele, siku yake itatimu
Usione ukadhani
Usimuone na yule, juu ni yake sehemu
Halipuuzwi nenole, hadhi yake maalumu
Hadumu hivyo milele, mpanga mambo Karimu
Usione ukadhani
Usimwone mwenye ndwele, haponi ukakalimu
Dhana hizo ziondole, kichwanimwo zisidumu
Hwenda mzima afile, mwele akatabasamu
Usione ukadhani
Maisha tangia kale, kueleweka vigumu
Yataka mwenye makele, kichwani alo timamu
Ndipo kunga amanyile, kwa mambo anozuumu
Usione ukadhani
Tama hapa niketile, nashusha yangu kalamu
Haya ndugu yashikile, upate mastakimu
Ila kiyatupa kule,utachekesha kaumu
Usione ukadhani