MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI - ETIMOLOJIA YA MANENO ' ADHAMA' NA 'ADHANA

JIFUNZE KISWAHILI

Full Version: ETIMOLOJIA YA MANENO ' ADHAMA' NA 'ADHANA
You're currently viewing a stripped down version of our content. View the full version with proper formatting.
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA MANENO ' ADHAMA' NA 'ADHANA'.

Neno *adhama* [ *Ngeli: i-/zi-]* katika lugha ya Kiswahili lina maana zifuatazo:

1. *Nomino*: Hali ya kitu kuwa na ubora.

2. *Nomino:* Mamlaka ya juu kabisa; enzi, ukuu.

3. Heshima kubwa, utukufu katika jambo.

4. Jambo la heshima kubwa.

*Mfano* : Kupewa fursa ya kuhutubia Mkutano huu ni adhama kubwa kwangu.

Katika lugha ya Kiarabu,  neno hili adhama (soma: adhwamatun/adhwamatan/adhwamatin عظمة ) ni nomino yenye maana zifuatazo:

1. Ukubwa, ukuu.

2. Kiburi, kujiona.

3. Majivuno.

Neno adhana [Ngeli: i-/zi-] katika lugha ya Kiswahili ni *nomino* yenye maana ya: mwito unaonadiwa na mwadhini msikitini kwa lengo la kuwaita Waislamu kwenda kufanya ibada.

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili adhana (soma: adhaanun/adhaanan/adhaanin أذان ) lina maana zifuatazo:

1. *Nomino*: Tangazo la jambo lolote lile.

2. *Nomino* : Mwito kwa waislamu kwenda kufanya ibada ya Swala.

Kinachodhihiri ni kuwa wakati maneno *adhama* (soma: *adhwamatun/adhwamatan/adhwamatin عظمة*) na *adhana* (soma: *adhaanun/adhaanan/adhaanin أذان* ) yalipoingia katika lugha ya Kiswahili na kutoholewa kuwa maneno *adhama* na *adhana* maana zake za msingi katika lugha ya Kiarabu hazikubadilika.

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*