MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI - ETIMOLOJIA YA MANENO ' ABTADI' na 'ABTALI'

JIFUNZE KISWAHILI

Full Version: ETIMOLOJIA YA MANENO ' ABTADI' na 'ABTALI'
You're currently viewing a stripped down version of our content. View the full version with proper formatting.
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA MANENO ' ABTADI' na 'ABTALI'

Neno *abtadi* katika lugha ya Kiswahili lina maana zifuatazo:

1. *Nomino* : Shujaa wa vita.

2. *Kitenzi elekezi:* fanya jambo kwa mara ya kwanza ili wengine wafuate; tangulia, anza.

3. *Kitenzi elekezi:* *alika kitu au shughuli _* ninabtadi safari yangu kwa kumuomba Mola; Bismi - Llaahi n'abtadi_ *ninaanza kwa jina la Mwenyeezi Mungu.*

Neno *abtali* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino*  yenye maana zifuatazo:
1. Kwa mujibu wa *Kamusi Kuu ya Kiswahili* neno hili *abtali* lipo katika umoja na wingi wake ni *maabtali* . Neno hili *abtali* lina maana ya *askari au mpiganaji ambaye ni shujaa na mzoefu wa kupigana.*

2. Kwa mujibu wa *Kamusi ya Kiswahili ya Karne ya 21,* neno hili *abtali* ni nomino yenye maana ya *wapiganaji* .

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *abtadi* limetokana na kitenzi cha Kiarabu *abtadiu* *ابتدأ *  kitenzi cha Kiarabu cha wakati uliopo cha nafsi ya kwanza *(ninaanza)* .

Neno *abtali* , katika lugha ya Kiarabu ni wingi wa neno *batwalun بطل* lenye maana ya mshindi, shujaa.

Kinachodhihiri ni kuwa neno hili ( *abtadiu أبتدأ*) llipoingia katika lugha ya Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *abtadi*  maana yake inayohusu kitenzi katika lugha ya asili - Kiarabu haikubadilika bali ikachukua dhana mpya ya *shujaa wa vita* (Kamusi Kuu ya Kiswahili).

Ama neno *abtali*, ambalo katika lugha ya  Kiarabu lina maana ya *washindi/mashujaa*,  wakati *Kamusi Kuu ya Kiswahili* ikiliweka katika umoja ambao wingi wake ni *maabtali* wakilipa maana ya *askari au mpiganaji ambaye ni shujaa na mzoefu wa kupigana* , Kamusi ya Kiswahili ya Karne ya 21 imelitambua kuwa lipo katika wingi na imelipa maana ya *wapiganaji* badala ya ile maana yake katika lugha yake ya asili - Kiarabu ya *washindi/mashujaa.*

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*