MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI - ISTILAHI ZA SARUFI YA LUGHA YA KISWAHILI

JIFUNZE KISWAHILI

Full Version: ISTILAHI ZA SARUFI YA LUGHA YA KISWAHILI
You're currently viewing a stripped down version of our content. View the full version with proper formatting.
ISTILAHI ZA SARUFI YA LUGHA YA KISWAHILI.
Ø  Alomofu
Mojawapo ya viwakilishi viwili au zaidi vya mofimu  moja  ambavyo  hujitokeza  katika mazingira tofauti ya mtoano. Haya ni mazingira ambamo kiwakilishi  kimoja tu hujitokeza na si kingine cha dhana hiyo. Mathalani katika lugha ya Kiswahili mofimu
 –MU- huwa inajitokeza katika maumbo ya maneno kamainavyoonekana hapa chini:
  1. a) m-ti
  2. b) m-chawi
  3. c) mw-ana
  4. d) mw-enge
  5. e) mu-uguzi
  6. f) mu-umba.
Vipashio M, MW, na MU vyote ni viwakilishi vya MU katika mazingira tofauti. Hii ina maana kwamba m,mw na mu ndizo alomofu au viwakilishi vya mofimu mu katika mazingira ya maumbo  yanayoanza na konsonanti na yale yanayoanza na irabu. Hakuna mifano katika lugha hii  ambako viwakilishi hivyo vinabadilishana nafasi katika mazingira hayo. Hii ndiyo hufanya mazingira hayo yaitwe mtoano.
Ø  Irabu
Ni aina ya sauti ya lugha inayotamkwa bila kuwepo na kizuizi chochote kwenye mkondo wa hewa  kutoka mapafuni  kupitia kinywani na/au puani.
Mfano wa irabu ni. a,e,i, o,u.
Ø  Mofimu
–Ni kipashio kidogo kabisa chenye uamilifu katika umbo la neno. Tunapozungumzia uamilifu tuna maana ya jukumu/wajibu/kazi/dhima. Mfano. mofimu “li, na, ta” katika maneno, alikuwepo, anaongea, ataingia zinaonesha dhima ya kutaja wakati/ njeo.
Ø  Mofu
_Kipashio cha kimaumbo kinachowakilisha mofimu. Katika Kiswahili  mfano wa mofu  yenye viwakilishi   vya kimatamshi na kimaandishi  ni kama huo uliooneshwa katika (4) hapa chini ambapo mofu moja inawakilisha mofimu mbili (2)
               4 (a) taa-chombo kinachowashwa ili kutoa mwanga
                 (b) taa-aina ya samaki.
Katika (4), tunaona mfano wa mofu yenye fonimu tatu za kimaandishi, yaani herufi t-a-a. Mofu hii inawakilisha mofimu mbili  kama ilivyooneshwa  katika 4 (a) na (b).
Ø  Mzizi
  Umbo-msingi la neno ambalo haliwezi kuchanganuliwa  tena katika  sehemu nyingine ndogo bila kupoteza uamilifu na utambulisho wake wa kisemantiki. Mfano. -l-, -chez-, -og- ni mizizi katika. maneno kula/mlo, mchezo, wanaoga. Zipo aina kuu nne za mzizi ambazo ni mzizi asilia, mzizi wa mnyambuliko,mzizi huru na mzizi funge. (Kuhusu mzizi asilia na mzizi wa mnyambuliko, rejea maelezo ya awali)
 Mzizi huru:
Ni mzizi ambao unajitegemea, yaani unaweza kusimama peke yake na ukaleta maana ya wazi. Nomino nyingi ni za namna hii, kama meza, kabati, giza n.k. lakini kuna aina nyingine za maneno  ambazo pia zina mzizi  huru kamasahau, saini, keti, hiari, tahadhari n.k.
Mzizi funge:
Ni mzizi ambao hauwezi kusimama peke yake na ukaleta maana ya wazi . kama. –pig-, -kat-, -som- (n.k).
Ø  Silabi
 Ni sehemu ya neno ambayo huweza kutamkwa mara moja  na kwa pamoja kama fungu moja la sauti. Ifuatayo ni mifano ya silabi katika maneno.   A-gha-la-bu, we-nda-wa-zi-mu,  u-si-ni-fu-a-ti-li-e,  u-m-fya-tu-li-e.,  m-zu-ri,  si-ta-ku-a-cha. Ukiona kipande chochote ambacho hakitamkiki kwa sauti moja, jua hakina sifa ya kuitwa silabi. Kuna aina kuu mbili za silabi:
  1. i) Silabi Funge
Ni silabi ambayo huishia na konsonanti  na ambayo haina kilele  cha msikiko au mvumo mfano: m, n (mtu, nta) .
  1. ii) Silabi huru:
Ni silabi ambayo  huishia  na irabu  au kama ni konsonanti  peke yake basi yenyewe itakuwa  pia ni kilele cha msikiko au mvumo wa sauti.( Ikumbukwe kuwa silabi zina sifa ya kifonolojia hivyo hutambulika zaidi kwa kuzitamka na kuzingatia mafungu ya sauti)
Ø  Sarufi Maumbo/mofolojia
– Ni tawi la isimu ambalo hujishughulisha na uchanganuzi wa kanuni na mifumo inayohusu  upangaji wa mofimu mbalimbali kuunda maneno katika lugha.
Ø  Sarufi Miundo/sintaksia
Ni tawi la isimu ambalo hujishughulisha na uchanganuzi wa taratibu na kanuni zilizopo baina ya maneno katika lugha.. Sintaksia huangalia zaidi mpangilio na mfuatano wa maumbo ya maneno katika kutoa taarifa iliyokusudiwa.
Ø  Sarufi maana /umbo maana/semantiki
Ni tawi la isimu ambalo  hujishughulisha na uchanganuzi wa  taratibu na kanuni  za maana ya maneno na tungo katika lugha. Umbo la neno hukubalika kisarufi iwapo lina maana, hivyo ni kazi ya semantiki kuhakiki maana za maneno.
Ø  Sarufi matamshi/umbo sauti/fonolojia
Ni tawi la isimu ambalo hujishughulisha na uchanganuzi  wa sauti za lugha.
Ø  Unyambulishaji/unyumbulishaji
Upachikaji wa viambishi kwenye mzizi ili kujenga neno. Mfano. mzizi.-pend- unakuwa.-pendo, upendo, pendana, wapendanao.
Ø  Shina
Ni sehemu ya neno lenye mzizi na viambishi tamati. Mfano: nitamfungashia =fung-mzizi; fungash-shina.
Ø  Isimu
Ni sayansi ya lugha/taaluma ambayo hujishughulisha na uchambuzi wa vipengele mbalimbali vya lugha kwa kutumia mbinu za kisayansi.
Ø  Chagizo
Ni nafasi inayojazwa na maneno yanayoeleza zaidi kuhusu tendo.Hivyo chagizo ni kikundi (kirai) kielezi  kinachopatikana katika kiarifu na ambacho huweza kudondoshwa  na bado sentensi ikabakia na maana  ya msingi.
Ø  Kijalizo
Ni maneno yote ambayo hutokea katika sentensi ili kutoa taarifa ya ziada. Maneno hayo huweza kufutwa na sentensi ikabaki na maana ya msingi.
Ø  Kiambishi
Ni kipashio cha neno ambacho hupachikwa kabla, au baada ya mzizi wa neno.( Lugha ya Kiswahili  haina kiambishi ambacho huchopekwa ndani ya mzizi, viambishi hivi vipo katika lugha ya Kiebrania, Kiingereza, n.k)
Ø  Kiarifu
Ni sehemu ya sentensi ambayo kiini chake ni tendo linalotendwa; mojawapo ya sehemu kuu mbili katika sentensi, nyingine ikiwa ni Kiima. Katika usemaji wa kawaida wa Kiswahili kiarifu huja baada ya kiima.
Ø  Kiima Kiarifu
Ni aina ya uhusiano katika muundo baina ya mtendaji wa tendo na tendo lililotendwa.
Ø  Kiimbo
Ni umbo la sauti linalotokana na jinsi  sauti inavyopanda  na kushuka katika usemaji.
Ø  Shada
Ni mkazo unaowekwa silabi ya pili toka mwisho katika lugha ya Kiswahili.
Ø  Kirai
Ni mpangilio wa neno au maneno wenye neno kuu moja.Mahusiano kati ya neno kuu na maneno mengine ndiyo hutupatia aina ya kirai. Yaani kama neno kuu ni nomino basi tunapata kirai nomino,(n.k)
Ø  Kishazi ­­
Ni tungo yenye kitenzi kinachojitosheleza kitaarifa au kisichojitosheleza kitaarifa. Kitenzi kinachotoa taarifa kamili hutoa kishazi huru na kile kilichoshushwa hadhi hutoa kishazi tegemezi.
Ø  Konsonanti
Kitamkwa ambacho utamkaji wake huathiriwa na kuzuiwa  kwa hewa ambayo ama inatoka mapafuni au inaingia  ndani, kama /g / , /m/ ,/k/,  /b/,  /s/,  / f/
Ø  Nadharia
 Taratibu, kanuni na misingi iliyojengwa kwa mawazo kwa madhumuni ya kuwa kigezo cha kuelezea jambo au mambo kadhaa.
Ø  Krioli
 Mchanganyiko wa maneno na vipengele  vya lugha mbili (au zaidi) tofauti ambao umekomaa na kuunda lugha ya mawasiliano kati ya wazungumzaji ambao  hapo awali walikuwa na lugha zao tofauti. Kwa kawaida krioli hutokana na pijini. Tofauti ya krioli na pijini ni kwamba wakati hiyo iliyotajwa mwanzo huwa ina sarufi kamilifu na msamiati  mahsusi, hiyo ya pili huwa haina kitu kama hicho.
Ø  Lahaja
Mojawapo kati ya lugha ambazo kusema kweli huhesabika kama lugha moja isipokuwa zinatofautiana katika baadhi ya vipengele fulani fulani, kama vile lafudhi, fonolojia, msamiati usiokuwa wa msingi au miundo, (Ni tofauti ya usemaji miongoni mwa jamii ya watu wanaosema lugha yenye asili moja). Lugha ya Kiswahili ina lahaja nyingi , na Kiswahili sanifu ni mojawapo ya lahaja hizo. Kuna
Lahaja Rasmi=lahaja ambayo imekubaliwa kutumiwa  katika mazingira au muktadha  rasmi.
Lahaja Sanifu=lahaja ambayo imesanifiwa  ili iweza kutumika katika mawanda mapana  zaidi na kwa shughuli  mbalimbali  zilizo rasmi na zinazoihusu jamii ambyo lugha yake ina lahaja nyingi.
Ø  Lugha chotara
Ni lugha ambayo imetokana na mchanganyiko wa lugha mbili au zaidi.
Ø  Lugha sanifu
Ni lugha ambayo imekubaliwa kutumika katika shughuli  za kielimu na ambayo  inakubaliwa  kimatumizi na wasemaji wengi zaidi.
Ø  Lugha za kibantu
Ni baadhi ya lugha za kiafrika ambazo zasemekana  zilitokana na lugha  mama moja. Lugha hizi zilipewa jina la lugha za kibantu  na W. BLEEK, mwanaisimu mmoja wa Kijerumani aliyefanya utafiti wa muda mrefu  kusini mwa jangwa la Sahara. Alizipa lugha hizo jina hilobaada ya kugundua kwamba zote zilikuwa zinatumia  neno Bantu (au pengine wantu, vantu, Batu, antu,watu, anhu, Banhu n.k.) kwa maana ya watu. Lugha za kibantu hujibainisha  kwa kuwa na utaratibu wa kuziweka  nomino zake katika ngeli mbalimbali na kila ngeli kuwa na viambishi vyake.
Ø  Prediketa
Katika sarufi ya kimapokeo hii ni sehemu mojawapo  kati ya sehemu kuu mbili zinazojenga sentensi.Kwa mujibu wa mtazamo huu sentensi ina kiima, kwa upande mmoja na prediketa kwa upande mwingine.Kiima huhusu mtendaji wa tendo  na maneno mengine yanayoambatana nacho, na prediketa huhusu tendo  na maneno mengine yanayoandamana nalo.
Ø  Sentensi
Kipashio kikubwa kabisa cha kimuundo  chenye kuleta maana kamili. Ni tungo yenye muundo wa kiima na kiarifu inayotoa taarifa kamili. Aina zake ni sentensi sahili, sentensi changamano, sentensi ambatano, sentensi shurutia.
Ø  Tungo
Ni kipashio cha kimiundo ambacho ni matokeo ya uwekaji pamoja vipashio sahili ili kujenga kipashio kikubwa zaidi. Aina zake ni: tungo neno, tungo kirai, tungo kishazi, tungo sentensi,
Ø  Yambwa ­
Ni nomino inayodokeza mtendwa upande wa kiarifu.
Ø  Yambiwa
   Ni nomino inayodokeza mtendewa katika sentensi upande wa kiarifu.
Ø  Upatanisho wa kisarufi
Ni kuwiana kwa viambajengo vinavyounda sentensi kama kitenzi, kivumishi, kielezi na maneno yanayohusiana nayo katika sentensi au tungo.
Ø  Othografia
Ni mfumo wa maandishi  unaotumiwa  katika lugha fulani; unaweza kuwa wa alama  au michoro.
Ø  Radidi
-enye kurudiwa rudiwa
Ø  Lafudhi
Sifa ya msikiko wa sauti ya msemaji  ambayo humpa utambulisho fulani katika jamii au eneo la kijiografia analotoka.
Ø  Alasauti
Sehemu ya viungo katika kinywa cha binadamu vitumikavyo katika utoaji  wa sauti za lugha. Mfano: ulimi, kaakaa gumu, kaakaa laini, meno, fizi, midomo (n.k.)
Ø  Alofoni
Umbo lingine la fonimu ileile moja/ maumbo tofauti ya fonimu moja. Mf. Shahani badala ya Sahani, suri badala ya zuri, fiatu badala ya viatu.
Ø  Fonimu
Vitamkwa vinavyoweza  kujenga maneno yenye maana  tofauti  au vinavyoweza  kubadili maana za maneno. Mfano wa fonimu ni:  /m/, /z/, /u/, /ng/ /u/ katika neno mzungu.