MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI - SHAIRI: MABONDENI WAHAME

JIFUNZE KISWAHILI

Full Version: SHAIRI: MABONDENI WAHAME
You're currently viewing a stripped down version of our content. View the full version with proper formatting.
TANGAZO GAZETINI
ULAMAA HEMED
Shikeni hili gazeti, kuna tangazo msome,
Kurasa za katikati, wa mabondeni wahame.
MFAUME HAMISI
Sababu hasa ni nini, tuache makazi yetu,
Tueleze tubaini, au eneo la mtu?
ULAMAA HEMED
Imesema serikali, watu wahamie juu,
Mvua itakuwa kali, masika ya mwaka huu.
MFAUME HAMISI
Kauli hiyo si kweli, serikali imezusha,
Wataka eneo hili, lengo ni kutuondosha.
ULAMAA HEMED
Hebu acheni ubishi, fateni mnoambiwa,
Mkiona ni uzushi, kwa nguvu mtatolewa.
MFAUME HAMISI
Mvua tangu azali, mbona huwa inanyesha?,
Na tena zilizo kali, wala sio rasharasha.
ULAMAA HEMED
Wataalamu wasema, kumechafuka angani,
Hivyo hameni mapema, kabla ya tafarani.
MFAUME HAMISI
Hiyo ni danganya toto, hapa haondoki mtu,
Nayatufike mazito, ila hatung’oki katu.
ULAMAA HEMED
Juwa ni hasara kwenu, mafuriko yakifika,
Zapotea mali zenu, kupata mlisumbuka.
MFAUME HAMISI
Hayo uloelimisha, yaweza kuwa huwenda,
Ili wakituondosha, ni wapi tutapokwenda?
ULAMAA HEMED
Hilo wala usijali, kujuwa wapi muende,
Kumbuka wale awali, walikwenda Mabwepande.
MFAUME HAMISI
Najua sio mjini, watatupeleka shamba,
Ila twataka baini, watatujengea nyumba?
ULAMAA HEMED
Kujengewa sitaraji, ila viwanja mwapewa,
Pia huduma za maji, na umeme mwawekewa.
MFAUME HAMISI
Hapo bila ya kupinga, naiona ahueni,
Pili nimepata mwanga, hakufai mabondeni.
ULAMAA HEMED
Kwa kuwa umeelewa, athari utaepuka,
Nishamaliza kahawa, kwa herini naondoka.
MFAUME HAMISI
Asante ndugu yangu, sina cha kusubiria,
Naacha ubishi wangu, bondeni napakimbia.
Watunzi:
1: Mfaume Hamisi
(Mshairi Machinga)
0716541703
2: Ulamaa Hemed
(Fundi wa tungo)
0717 501557