MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI - MFANO WA MBAZI

JIFUNZE KISWAHILI

Full Version: MFANO WA MBAZI
You're currently viewing a stripped down version of our content. View the full version with proper formatting.
Siku moja Panya akiwa darini alichungulia chini na kumuona mkulima na mkewe wakiaanda mtego utakaotumika kumnasa, Kwa majonzi alisikitika na kujiona anasiku chache za kuishi duniani.
Siku hiyo panya alizunguka huku na kule kuomba msaada wa mawazo kwa wanyama wenzake ili aweze kunusurika na mtego alioandaliwa, lakini wanyama wenzake hawakuweza kumsaidia huku wakisema matatizo yako hayatuhusu.
Awali panya alitoka ndani na kwenda kuonana na mbuzi, akamwambia mbuzi, mkulima na mkewe wananiwinda, wameandaa mtego wa kuniangamiza, tafadhali naomba nisaidie, naomba nisaidie mwenzako niepukane na kifo nilichoandaliwa, Mbuzi akamjibu ” Samahani Mimi sihusiki na mambo ya huko ndani na hayo matatizo yako hayanihusu, tafadhali acha kunisumbua, mimi siwezi kukusaidia nakuomba uondoke hapa haraka sana, mkulima akikuona hapa utanisababishia matatizo. Panya akaondoka kwa huzuni wakati huo akapata wazo la kuonana na ng’ombe akiamini ng’ombe si mbuzi japo wote ni wanyama kama yeye.
Basi Panya alienda kuonana na Ng’ombe, alianza kwa kusema ” Samahani ng’ombe, najua wewe ni mnyama kama wanyama wengine, tunachotofautiana Mimi na wewe ni ukubwa wa umbo ila ukiangalia mambo mengine hakika tunaendana, wewe una mkia na Mimi pia nina mkia, unakula mahindi na mimi pia ninakula mahindi. Tafadhali bwana naomba nisaidie mwenzako ninawindwa na mwenye nyumba kwani jana usiku nimemuona akitoa mtego unaoweza ukaniangamiza ndani ya dakika chache, najua wewe unaweza kuukanyaga ule mtego na kuuvunja vunja kabisa, nitakachofanya mimi ni kukujulisha mara tu atakapotoka, ukiuvunja nitakuwa huru kula nitakavyo, ng’ombe naye alitoa majibu kama ya mbuzi basi panya akawa amekosa kwa kukimbilia, zaidi zaidi alijiwazia mwenyewe kuwa itabidi awe makini kwa kila hatua atakayo iendea.
Usiku ule panya akiwa amelala alisikia mtego umefyatuka, mke wa mkulima na mumewe wakafurahi wakiamini kuwa ni panya amenaswa, haraka sana waliufuata mtego ulipo na kukuta mtego umenasa nyoka badala ya panya. mke wa mkulima alipojaribu kumtoa ghafla aling’atwa na hali yake ikaanza kuwa mbaya, ikabidi yule mkulima amkimbize mkewe hospitalini, hali ya mke wa mkulima aliendelea kuwa mbaya kutokana na sumu ya nyoka, watu wakawa wanakuja kutoa pole kwa mke wa mkulima, chakula kikapungua, mkulima aliamua kumchinja mbuzi, Panya aliyaona haya alisikitika huku akiwa anayakumbuka majibu ya mbuzi na kujiuliza mwenyewe kuwa mbuzi angesaidia kuuharibu ule mtego wala asingechinjwa, baadaye mke wa mkulima alifariki, watu wengi walikuja kwenye msiba, yule mkulima aliamua kumchinja ng’ombe wake ili watu wapate kitoweo siku ya msiba.
Ndivyo ilivyo katika maisha tunayoishi. Watu wengi wanakuwa na uwezo wa kutatua shida za watu wasio na uwezo, lakini kwa sababu haziwahusu hata wakiombwa msaada wanaishia kutoa maneno ya dharau na matusi huku wakisema shida zako hazinihusu wasijue msaada wanaoweza kuutoa unaweza ukawasaidia au kuwaepusha na jambo baya lililopo mbele yao.
Mbuzi na ng’ombe wangeamua kumsaidia panya kuuharibu ule mtego hata wasingeangamia, lakini kwa jeuri zao na kuona matatizo ya panya siyo yao wala hayawahusu mwishowe walijikuta wao ndio wanaangamia.