MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI - NYIMBO ZA KIZALENDO

JIFUNZE KISWAHILI

Full Version: NYIMBO ZA KIZALENDO
You're currently viewing a stripped down version of our content. View the full version with proper formatting.
TANZANIA TANZANIA NAKUPENDA
Tanzania Tanzania, nakupenda kwa moyo wote
Nchi yangu Tanzania, jina lako ni tamu sana
Nilalapo nakuota wewe, niamkapo ni heri mama wee
Tanzania Tanzania nakupenda kwa moyo wote.

Tanzania Tanzania , ninapokwenda safarini
Kutazama maajabu, biashara nayo makazi
Sitaweza kusahau mimi mambo mema ya kwetu kabisa
Tanzania Tanzania nakupenda kwa moyo wote

Tanzania Tanzania karibu wasio kwao
Kwenye shida na taabu kukimbizwa na walowezi
Tanzania yawakaribisha tuungane kiume chema wee
Tanzania Tanzania nakupenda kwa moyo wote

Tanzania Tanzania watu wako ni mema sana
Nchi nyingi zakuota nuru yako hakuna tena
Na wageni wakukimbilia ngome yako imara kweli wee
Tanzania Tanzania mola awe nawe daima

 
TAZAMA RAMANI
Tazama ramani utaona nchi nzuri
Yenye mito na mabonde mengi ya nafaka,
Nasema kwa kinywa halafu kwa kufikiri,
Nchi hiyo mashuhuri huitwa Tanzaniaaaaaaaaaa….
Majira yetu haya, yangekuwaje sasa
Utumwa wa nchi, Nyerere
ameukomesha X2

Chemchem ya furaha amani nipe tumaini,
Kila mara niwe kwako nikiburudika,
Nakupenda sana hata nikakusitiri,
Nitalalamika kukuacha Tanzania.
Majira yetu haya, yangekuwaje sasa
Utumwa wa nchi, Nyerere
ameukomesha X2

Nchi yenye azimio lenye tumaini,
Ndiwe peke yako mwanga wa Watanzania,
Ninakuthamini hadharani na moyoni,
Unilinde name nikulinde hata kufa.
Majira yetu haya, yangekuwaje sasa
Utumwa wa nchi, Nyerere
ameukomesha X2

Safi sana kwa kutukumbusha