MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MBINU/NJIA ZA UFUNDISHAJI KISWAHILI KWA WAGENI/LUGHA YA PILI

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
MBINU/NJIA ZA UFUNDISHAJI KISWAHILI KWA WAGENI/LUGHA YA PILI
#1
MBINU ZA UFUNDISHAJI LUGHA YA PILI/KIGENI
Suala la ufundishaji lilianza miaka mingi tangu muingiliano wa jamii lugha tofauti karne nyingi zilizopita. Jamii moja na nyingine walianza kukubaliana na kukubalinana na lugha ngeni ili wawasiliane nao, na kuibuia haja ya kufundisha lugha ya kigeni. Ufundishaji lugha ya kigeni kitaaluma ilianza karne ya 19 na karne ya 20 ilikomaa sana. Lakini katika kipindi hk chote ufundishaji lgh za kigeni umekuwa ukibadilika kutokana na mabdiliko ya wanafunzi na nadharia za kiisimu na nadharia katika elimu kama taaluma. Hata hivyo ufundishaji lgh za kigeni unazidi kukomaa kutokana namaendeleo ya sayansi na teknolojia, hali hii imeibua mbinu za ufundishaji wa lugha za kigeni.
Mbinu za ufundishaji ni njia za ufundishaji zilizokitwa katika kanuni na miongozo maalumu
  1. Mbinu ya sarufi- tafsiri.
  2. Mbinu ya moja kwa moja.
  3. Mbinu ya usikilizaji.(audialingualism)
  4. Mbinu ya mwitiko kamili wa kivitendo
  5. Mbinu ya utambuzi (cognitive
  6. Mbinu ya ujifunzaji kijumuiya
  7. Mbinu yaupendekezi
  8. Mbinu ya kimawasiliano.
                                                           MBINU YA SARUFI- TAFSIRI.
Hii ni mbinu ya kimapoke kwa kuwa ilianza na ilitawala ufundishaji hata lugha zilizokufa. Hadi sasa inatumika kufundishia watu wengi.
SIFA ZA MBINU HII
  1. Lgh ya utunzi ndiyo inatumika kufundishia
  2. Wanafunzi hupewa orodha za kanuni ya kisarufi ili wakariri (kupewa maneno ya kigeni).
  3. Stadi zinazopewa mkazo ni kusoma na kuandika tu. Mkazo kidogo au hakuna mkazo katika utamkaji wa sauti. Vitabu vilivyoandika kwa ajili ya kufundishia lgh kwa kutumia mbinu hii kwa kiasi kikubwa hufafanua kanuni za kisarufi na kasha kutoa mazoezi mengi ya kutafsiri .
                     MBINU YA MOJA KWA MOJA.
Huzingatiaufundishaji msingi wa uasilia wa lugha. Yaani kumudu lgh ya kigeni kama lugha mama yake. Mbinu hii iliibuka kutokana na kutambua kuwa kutambua lugha ni kuzungumza zaidikuliko kuiandika
SIFA ZA MBINU HII
  1. Lugha lengwa tu ndiyo inayotumika, inachukuliwa kuwa lugha ya kwanza ni chanzo cha makosa katika kujifunza lugha ya pili.
  2. Stadi ya mazungumzo hutawala katika mbinu hii.
  3. Stadi ya kuandika haiwekewi uzito.
MBINU YA USIKILIZAJI.(AUDIALINGUALISM)
Ilijikita katika mbinu ya usikilizaji. Waasisi wa mbinu hii ni wana utabia kama vile Bloomfield 1942, walikabidhiwa mhutasari wa ufundishaji lgh za kigene marekeni na kueleza kuwa kujifunza lugha ni kama kujifunza tabia Fulani ambao wao huona kuwa kujifunza lugha ni kurudiarudia mara kwa mara . lengo la kufundisha lugha ni kuzungumza ni kumwezesha kuzungumza na kukabiliana nayo ana kwa ana kwa kiasi Fulani
SIFA
  1. Kukariri mazungumzo na kufanya mazoezi kuepuka kasoro katika uzungumzaji.
  2. Stadi za lugha hupangiliwa kuanzia stadi ya kusikiliza, kuzungumza, kusoma na kuandika
  3. Hutumia lugha ya kigeni tu kama lugha ya kufundishia/lugha ya pili. Ufundishaji wa ruwaza wa miundo ya lugha uwe wa kurudiarudia.
  4. Hakuna uelezwaji wa sarufi
  5. Msamiati hujifunzwa kutokana namuktadha
  6. Kuna matumizi ya vinasa sauti kama vile cd,video
  7. Msisitizo upo katika utamkaji
  8. Baada ya mwitiko sahihi hutolewa uimarisho/tuzo.
MBINU YA UTAMBUZI
Iliibuka miaka ya 1970 kama mwitiko wa uhakiki ni mbinu rekebishi ya mbinu 2 zilizotamgulia. Watetezi wa mbinu hii ni wanasaikolojia na wanaisimu tambuzi
SIFA ZA MBINU HII
  1. Inatilia mkazo kumpa mwanafunzi uwezo wa kuelewa mfumo wa lugha ya kigeni, kasha kumpa uhuru wa kuweza kujifunza peke yake kwa kutumia msingi aliopewa mbinu hii hupinga kujifunza lugha, baada ya mwanafunzi kupewa mbinu za ujifunzaji mazoezi na msingi mwanafunzi huachiwa huru na kumuachia ajifunze mwenyewe kwa kutumia mbinu zake. Noam Chomsky anaunga mkono mbinu hii. Vitabu vilivyoandikwa kufundishia lugha ya kigeni humsaidia mwanafunzi kutambua misingi ya kisarufi na ufaham na utungajiwa kubuni na kujieleza.
MBINU YA MWITIKO KAMILI WA KIVITENDO
Hii ni mbinu ambayo hitwa pia mkabala asilia wa kujifunza lugha. Mbinu hii iliasisiwa na wanaisimu saikolojia kama James Asher 1969, mbinu hii inalenga utumiaji wa stadi moja ili kuimarisha stadi nyingine.
SIFA
  1. Mwanafunzi humsikiliza na kumtazama mwalimu akitamka amri na kuzitekeleza moja kwa moja na baada ya hapo mwalimu hurudia kila amri na kumtaka mwanafunzi atekeleze baadae mwanafinzi hutekeleza mwenyewe.
  2. Inasisitiza kuwa katika kujifunza lugha ya pili kwa kutumia vitenzi vilivyo katika kauli ya kuamru kama ilivyo kwa watoto wadogo wanapojifunza lugha mama. Mfano mama taka uji.
MBINU YA UJIFUNZAJI LUGHA KIJUMUIYA
Hujulikana pia kama mbinu ya ujifunzaji kwa ushauri. Ni mbinu iliyobuniwa na Charles A na Curran 1976. Ni wana saikolojia bingwa wa masuala ya ushauri na uelekezi. Katika mbinu hii mwanafunzi huzingwatiwa katika mbinu mbili, kwa upande mmoja hisia zake kama binadamu, hupewa nafasi ya kujieleza na kupewa ujuzi wa lugha kwa kiwango kinachotakiwa
SIFA ZA MBINU HII
  1. Mwanafunzi ndiye egemeo la ujifunzaji lugha. Dhima ya mwalimu ni kushauri tu na kuchochea ujifunzaji uendelee, uhusiano baina ya mwalimu na mwanafunzi ni sawa na mshauri na mteja.
  2. Mwanafunzi huchagua wanachotaka kujifunza na kuambiana kwa lugha yao. Mwalimu ambaye ni mshauri huwatafsiria namna ya kukisema katika lugha ya kigeni na wanafunzi hukisema kwa lugha ya kigeni na kukirudiarudia, mchakato huu huendelea katika mada mbalimbali na mazungumzo huhifadhiwa kwa matumizi ya baadae. Katika upande wa hisia za kibianadamu : wanafunzi hupewa nafasi za kukisema kwa kutumia lugha za kigeni. Dai kubwa la mbinu hii ni kuwa lugha ni watu , lugha ni watu kwa kukabiliana pia lugha ni watu kadri ya mahitaji na miitiko yao. Hivyo wanafunzi huwa jumuiya na hujifunza kupitia jumuiya hiyo.
  3. Katika kutumia mbinu hii hakuna mhitasari wala kitabu kinachotumika kufundishia.
                                                         MBINU YA UPENDEKEZI
Mwasisi wake ni Gorge lozanov 1979. Kwa mujibu wa mbinu hii mazingira bora
                                                         SIFA ZA MBINU HII
  1. Darasa hutengenezwa na kuwa mahara pa kuvutia sana kukaa. Wanafunzi wakae kwa muduara katika vikundi vidogo vidogo na kuwe na michoro mziki, picha. Masomo huangwa katika mada kumi na ufundishwaji hupewa masaa manne kila siku kwa siku 6 katika wiki. Wanafunzi hupewa orodha ya msamiati ili kukariri. Mbinu mbalimbali hutumika ikiwa ni pamoja na uigaji, maswali na majibu, uigizaji n.k. vitabu viulivyoandikwa katika mbinu hii husheheni vielelezo mbalimbali ili kumvutia mwanafunzi katika kujifunza. Lengo la mbinu hii ni kupata umilisi wa mazungumzo yaani maneno 230 katika siku 30.

8/04/2014

                                                   MBINU YA KIMAWASILIANO
Mbinu hii iliibuka katika miaka ya 1980 na iliendelea kukubalika katika nchi nyingi duniani kama njia bora ya kufundishia lugha ya pili. Kuibuka kwake kulichochewa na hali ya kutegemeana miongoni mwa nchi za bara la ulaya hasa kiuchumi na soko la dunia kati ya nchi hizo, kama taaluma mbinu hii chimbuko lake lilitokea siku nyingi hata kabla ya 1980, wapo wanaisimu waamirifu kama vile Firth 1968, Halliday 1973 na mwanaisimu jamii Hyrmes 1972, walikuwa na mawazo kuwa lugha ni mawasiliano, wanasema “msingi wa mbinu hii ni mwanafunzi ndilo eneo la mafinzo na kwamba kujifunza lugha ni kujifunzakuwasiliana. Hawa wanatofautiana na Noam chomscky kuwa anayedai kuwa kujua lugha ni kujua umilisi wa mfumo nakanuni na hivyo kuitumia sahihi.
Hivyo tangu siku ya kwanza jitihada za mawasiliano lazima zifanyike katika ujifunzaji na ufundishaji, madhumuni ya mbinu hii n kukuza stadi zote za lgh ambazo hutumika katika mawasiliano.

Maana ya mbinu ya kimawasiliano:-
Ni mbinu iliyokitwa kwa mwanafunzi, hutoa mwanya kwa mwanafunzi si katika umilisi wa sarufi bali pia katika stadi za jamii yaani nini cha kusema, namna ya kusema, lini aseme na wapi aseme ili kuridhika na kile anachohitaji kila siku.
Lengo kuu la mbinu hii ni kumfanya mwanafi=nzi apate umilisi wa mawasiliano na mwalimu kazi yake ni kumwezesha mwanafunzi kupata umilisi wa mawasiliano, na umilisi ni pamoja na
  1. Umilisi wa kisarufi
  2. Umilisi wa uneni
  3. Umilisi wa kiufundi, kv alama za kiuakfishi like koma, nukta nk
  4. Umilisi wa kiisimu jamii. Kv namna ya kusema, wapi nk.
                               MISINGI YA MBINU YA UFUNDISHAJI LUGHA KIMAWASILIANO
  1. Namna ya kutumia lugha
  2. Uamiliaji asilia wa lugha kuwa mwanafunzi ajifunze lugha katika muktadha halisi na wenye uasilia
  3. Ufundishaji uhusishwe na hali halisi ya maisha, ili mwanafunzi aelewe uasilia wa maisha
  4. Lugha ifindishwe kama stadi, lugha isifundishwe kama somo, katika mbinu hii mwal awafanye wanafunzi wake wazungumze ili kujua hali halisi. Hivyoikubalike kuwa lugha ni stadi
  5. Ukuzaji uwezo wa kuwasiliana, katika mawasiliano kuna stadi ndogo 4 ambazo zinapaswa kukuzwa kwa mwanafunzi ili aweze kuwasiliana ambazo ni
(a)    Kuzungumza
(b)   Kusikiliza
©    Kusoma
(d)   Kuandika

SIFA ZA MBINU YA KIMAWASILIANO
  1. Sifa kuu ni mawasiliano, inasisitiza mawasiliano lugha inatumika kwa mawasiliano, hivyo mbinu hii husisitiza mawasiliano katika kufundisha lugha. Husisitiza hali halisi ya maisha na mawasiliano katika muktadha hivyo ujumbe unaoelezwa katika mawasiliano huwa katika muundo wa kidhima.
  2. Inamlenga mwanafunzi kwa sababu kazi ya mwalimu ni mwezeshaji tu, anawezesha kisha anaruhusu mwanafunzi kujifunza mwenyewe.
  3. Muktadha wa kijamii, mbinuhii husisistiza mawasiliano ya kijamii na miktadha halisi, hivyo mwanafunzi hujifunza lugha kwa sababu muktadha wa kijamii hutengenezwa.
  4. Uwezo wa kuzungumza, mbinu hii huwasaidia wanafunzi uwezo wa kuzungumza kitu ambacho ni muhimu katika maisha.
  5. Lugha lengwa hujifunzwa kama lugha ya kwanza katika mbinu hii.
  6. Mbinu hii hukuza stadi za lugha kv, kusikiliza na kuzungumza, kusoma kuandika

                                                           MAHITIMISHO
  1. Mbinu hii haihitajiki kupuuzwa kwa sababu hihitaji mawasiliano ya kila siku.
  2. Utumizi wa lugha wa kila siku ndio msingi wa lugha ya pili na siyo lugha ilivyo katika maandishi, kitendo cha kujifunza lgh kwa kimazingira huitwa
  3. Kama ilivyo ujifunzaji wa mfumo zalishi ni muhimu pia kujifunza raghibaya wanafunzi na kuwapa kiwango Fulani cha kujiamini, mwl awape fursa ya kutumia kile walichojifunza katika mazingira halisi.
  4. Kama uzuri wa mzungumzaji mzawa “ni uzuri huo huo anatakiwa aupate mzungumzaji wa lugha ya pili/asiye mzawa. Vitu vya kuandaa: matini ziwe bora ili mjifunzaji kumudu lugha anayojifunza.
  5. Ni muhimu kwa matini kuwa rahisi ili wanafunzi wasitumia muda mrefu kupata dhana ya matini hiyo, katika hali halisi wanapokutana na matini za namna hii wanachanganya hivyo wapewe muda wa kutosha na mazoezi ya kutosha pia.
  6. Matini hizi zipo si kwa ajili ya kusoma tu bali pia katika kuibua lugha itakavyotumiaka darasani na kuongeza marifa zaidi
  7. Urefu matini sharti ziwe fupi.

UGUMU KATIKA MBINU YA MAWASILIANO
Husababishwa na muktadha ambao lugha hiyo inafundishwa unatakiwa kujua kuwa
  1. Unafundisha akina nani?
  2. Wanajifunzia wapi kwa wazawa au ugenini?
  3. Kwanini wanajifunza?
Hivyo muktadha wa ufundishaji uzingatie mambo makuu manne
  1. Umri mfano watoto, vijana au watu wazima
  2. Viwango, unafundisha katika kiwango gani
  3. Ueledi wao, ueledi wao/kazi zao
  4. Muktadha wa kijamii,
UMRI
(a)    Ufundishaji wa watoto
Inaaminika kuwa watoto hujifunza lugha kirahisi kuliko watu wazima, hujifunza bila kujua jitihada wnazofanya katika kujifunza lugha. Utafiti unaonyesha kuwa waqtu wazima wanaweza kuwa wazuri katika baadhi ya maeneo, wanaweza kurunza misamiati mingi kuliko watoto. Wanaweza kutumia michakato mifupi katika kujifunza michakato ya kisarufi na kiisimu wakati watu wazima wakiwa darasani wana uwezo wa juu wa kujifunza haraka. Hivyo wakati watoto huzungumza katika mzingira halisi bila shida watu wazima wanapata shida. Watoto darasani wanaweza kupata ugumu katika kujifunza lugha ya pili kwa sababu ya tofauti binafsi, kijamii, kiutamaduni na kisiasa ambazi zio katika ufundishaji wa lugha ya pili. Ili kuwa na ufundishajiwa wenye mafanikio unatakiwa kuwa na stadi maalumu tofauti na zile za watu wazima.

MAMBO MATANO YA KUZINGATIA KUFUNDISHA WATOTO.
  1. Kukuza uwezo wa kufikiri, watoto hujifunza kwa kujikita katika viti au mambo aambayo ni ya papo kwa papo katika matumizi ya lugha. Mambo ya kufanya unapokuwa darasani ili kukuza uwezo wa kufikiri wa watoto:
(a)    Usifafanue sarufi kama ilivyo,
(b)   Dhana za sarufi zifundishwe kwa kutumia ruwaza, mf: nilijifunza kisw, ulijifunza kisw, alijifunza kisw. Tulijifunza kisw-, mlijifunza kisw-
Baadhi ya dhana ngumu zirudiwerudiwe.

  1. Muda wa utayari, hii ni tofauti ya watoto na watu wazima wao huwa na mda mfupi, kazi ya mwl ni kuweka mvuto wa lugha na lifurahishe ili kuonyesha uhalisia. Ni muhimu kuelewa nini maana ya utayari, zingatia yafuatayo:
(a)    Andaa mazoezi ya kuvutia
(b)   Wape aina mabalumbali za mazoezi kuwaandaa
©    Mwl ahuishe , ahaishe na aasilishe kuhusu somo lenyewe, zingatia kuwa mwl ni lazima awe mtendaji kutengeneza utayari wa watoto.
(d)   Ucheshi huwafanya watoto wajifunze.
(e)   Hakikisha unapata udadisi, uchunguzi wa watoto ili kujua mwelekeo wao.
  1. Milango ya fahamu, watoto wanapaswa kutumia milango yote ya fahamu inayochangamushwa, kazi ya mwl ni kujitahidi kuchangamsha hii milango ya fahamu hadi zaidi ya macho na maskio. Mambo ya kufanya
(a)    Fanya michezo hii hupanua milango yao ya fahamu
(b)   Kazi mradi ndogondogo ili kuwafanya wajifunze
©    Misaada ya ufahamu , mf: maua yana harufu gani?
(d)   Tumia lugha ya ishara, n I muhimu kwa sababu watoto wataangalia kwa makini na kutambua lugha.
  1. Athari, haya ni mabo ambayo ni vizuizi katika ujifunzaji lugha. Watoto wana udhaifu kuliko watu wazima, namna ya kuondoa athari za lugha
(a)    Thibiti darasa kutomcheka mtu darasani,
(b)   Uwe mkweli katika kuwajenga,
©    Hakikisha wanashiriki mazungumzo kadri inavyowezekana, wape nafasi kujaribu kufanya kitu kwa kila mmoja.

  1. Uasilia, umaana wa lugha, watoto huingalia lugha mpya kama inaweza kutumika papo kwa papo. Hawajisikii ikiwa lugha haina manufaa kwao mfano lugha isoyo ya asili na isiyo na maana. Kipi cha kufanya:
(a)    usitumie lugha rasmi sana,
(b)   lugha ihusianishwe na mazingira kama vile mazingira, matukio, uhusika mf: motto ahusike kamapolisi, daktari nk.
©    Mbinu ya kuanza na kitu kizima itumike usianze na vipande vipande, weka mkazo katika stadi mablimbali kama kusoma, kusikiliza, kusoma na kuandika
b. ufundishaji watu wazima
watu wazima wanaweza kufundishika kwa urahisi, kiwango chao cha aibu kinaweza kuwa kikubwa hata zaidi ya watoto lakini wao hujiamini. Kuna mambo matano ya kuzingatia katika kufundisha watu wazima.
  1. Kukuza uwezo wa kufikiri, watu wazima wana uwezo wa kutumia data mbalimbali na kanuni, kuwa mwangalifu kufundisha udhahania katika matumizi ya lugha.
  1. Muda wa utayari, watu wazima wana uwezo wa kuwa na utayari kwa muda mrefu hata kama somo haliwavutii,. Lakini kanuni ya kuwapa mazoezi kanuni ni ile ile.
  1. Milango ya fahamu, itumike pia japokuwa watu wazima huongozwa na hisia zaidi.
  1. Athari, jitahidi kuondoa athari zinazotokea katika ujifunzaji na ufundishaji lugha.
  1. Uasilia na umaana wa lugha. Watu wazima wana uwezo wa kufikiri dhana dhahania za lugha na dhana zisizo asilia zinaweza kutumika katika ujifunzaji.
USIMAMIZI WA DARASA LA WATU WAZIMA
  1. MWl uoneshe heshima na nidhamu ili wasijenge dhana ya kuchukia somo au kuwa na mwelekeo hasi wa somo hilo,
  2. Mwl asiwachukulie watu wazima kama watoto
  3. Mwl awape uhuru wa kufanya wanapokuwa katika mazingira yao wanapokuwa nje ya darasa
  4. Mwl asiwafundishe watu wazima nidhamu kama vile watoto
  5. Wachukulie kuwa ni watu wazima hivyo wanaweza kufanya mambo kiutu uzima.

VIWANGO VYA WANAFUNZI
Ufundishaji wa lugha za kigeni huwa katika viwango vitati
(a)    Kiwango cha awali
(b)   Kiwango cha kati
©    Kiwango cha juu


Ufundishajiwa kiwango cha awali
Wanafunzi hawana maarifa kuhusu hiyo lugha hivyo mwl ni mwezeshaji wao katika malengo yao, mwl anapaswakutoa zawadi ili kuwafanya wanafunzi kuweka umakini,
Mambo kumi ya kuzingatia
  1. Mchakato wa ukuzaji akili kwa wanafunzi, wanafunzi washiriki kurudiarudia maneno aktika siku zile za mwanzo. Mwl asichanganyikiwe na wanafunzi kutopata mabadiliko katika kipindi kifupi maana ni lugha ngeni kwao, siku za mwanzo wapatie mazoenzi madogomadogo mf: waweze kutaja majina yao na wanakokaa. Mazoezi yalenge kuwakuza uelewa.
  2. Kazi ya mwl. Mwanafunzi hutegemea mwl katika kila kitu kuhusiana na lugha, kazi za vikundi zitumike katika kujijengea uelewa. Mf picha.
  3. Unenaji wa mwl, mwl aongee kwa sauti ya kutosha, mwl atumie misamiati rahisi kabisa na sarufi rahisi kabisa.
Mwl atumie lugha ya kwanza mara chache sana, si vizuri uwaruhusu wanafunzi kutumia lugha zao za kwanza mara kwa mara. Mwl atumie lugha ya kwanza kwa manufaa ya : kuelezea hoja za sarufi 2. Kuonyesha maneno yaloyowachanganyaau kwenye maneno ya kiutamaduni
  1. Hakikisha lugha inayotumika ni lugha inayotua inafuata kanuni za kimawasiliano hivyo ionyeshe uasilia waa lugha isiwe lugha rasmi sana kwa wako katika hatua za awali mf: salamu na utambulisho, mwl hakikisha kuwa ufundishaji   ni rahisi na mfupi. Mwl usiwakatishe tama wanafunzi wako bali wape muda kujifunza.
  2. Ufasaha na usahihi, ufasaha ni muhimu katika hatua hii hakikisha unakuwa katika semi fupifupi mana ni muhimu kuhimizauzungumzaji , usahihi utiliwe mkazo katika sarufi za lugha. Ni muhimu kuangal;ia mahitaji ya wanafunzi katika kuzungumza bila kukosolewa katika kuzungumza. Wape mazoezi ya kisarufi na kifonolojia.
  3. Ubunifu wa wanafunzi, lengo la kujifunza lugha ni kujenga uelewa na kuzalisha kitu kipya ili kuweka ubunifu na utoaji. Katika kiwango cha awali wanafunzi wanaweza kuwa wabunifu kwa kiwango Fulani usitegemee ubunifu mkubwa sana katika lugha.
  4. Mbinu, mbinu rahisi zitumike, anzisha maswali unayoyamiliki yakifuatiwa na maswali ya wanafunzi, pia mbinu ya makundi ni mbinu nzuri sana.
  5. Malengo ya mzungumzaji na msikilizaji, kazi yake ni uasilia wa mawasiliano hakikisha usikilizaji na uzuungumzaji una maana ya mawasiliano.
  6. Malengo ya usomaji na uandishi, katika kiwango cha awali mada ya kusoma na kuandika inatakiwa iwe fupi inayokidhi matakwa ya wahusika kama vile matangazo, kazi ya kuandika inapaswa kuwa ya kuorodhesha.
  7. Sarufi, inatahusisha vitenzi rahisi, viwakilishi vya nafsi .toa lugha lugha ianyieleweka. mbinu ya kuambukiza sarufi inafaa katika kufundisha sarufi na kuambukiza ruwazA
KIWANGO CHA KATI
Ni mambo yale yale ya kiwango cha awali
  1. Mchakato wa ukuzaji akili kwa wanafunzi, wanafunzi washiriki kurudiarudia maneno aktika siku zile za mwanzo. Mwl asichanganyikiwe na wanafunzi kutopata mabadiliko katika kipindi kifupi maana ni lugha ngeni kwao, siku za mwanzo wapatie mazoenzi madogomadogo mf: waweze kutaja majina yao na wanakokaa. Mazoezi yalenge kuwakuza uelewa.
  2. Kazi ya mwl. Mwanafunzi hutegemea mwl katika kila kitu kuhusiana na lugha, kazi za vikundi zitumike katika kujijengea uelewa. Mf picha.
  3. Unenaji wa mwl, mwl aongee kwa sauti ya kutosha, mwl atumie misamiati rahisi kabisa na sarufi rahisi kabisa.
Mwl atumie lugha ya kwanza mara chache sana, si vizuri uwaruhusu wanafunzi kutumia lugha zao za kwanza mara kwa mara. Mwl atumie lugha ya kwanza kwa manufaa ya : kuelezea hoja za sarufi 2. Kuonyesha maneno yaloyowachanganyaau kwenye maneno ya kiutamaduni
  1. Hakikisha lugha inayotumika ni lugha inayotua inafuata kanuni za kimawasiliano hivyo ionyeshe uasilia waa lugha isiwe lugha rasmi sana kwa wako katika hatua za awali mf: salamu na utambulisho, mwl hakikisha kuwa ufundishaji   ni rahisi na mfupi. Mwl usiwakatishe tama wanafunzi wako bali wape muda kujifunza.
  2. Ufasaha na usahihi, ufasaha ni muhimu katika hatua hii hakikisha unakuwa katika semi fupifupi mana ni muhimu kuhimizauzungumzaji , usahihi utiliwe mkazo katika sarufi za lugha. Ni muhimu kuangal;ia mahitaji ya wanafunzi katika kuzungumza bila kukosolewa katika kuzungumza. Wape mazoezi ya kisarufi na kifonolojia.
  3. Ubunifu wa wanafunzi, lengo la kujifunza lugha ni kujenga uelewa na kuzalisha kitu kipya ili kuweka ubunifu na utoaji. Katika kiwango cha awali wanafunzi wanaweza kuwa wabunifu kwa kiwango Fulani usitegemee ubunifu mkubwa sana katika lugha.
  4. Mbinu, mbinu rahisi zitumike, anzisha maswali unayoyamiliki yakifuatiwa na maswali ya wanafunzi, pia mbinu ya makundi ni mbinu nzuri sana.
  5. Malengo ya mzungumzaji na msikilizaji, kazi yake ni uasilia wa mawasiliano hakikisha usikilizaji na uzuungumzaji una maana ya mawasiliano.
  6. Malengo ya usomaji na uandishi, katika kiwango cha awali mada ya kusoma na kuandika inatakiwa iwe fupi inayokidhi matakwa ya wahusika kama vile matangazo, kazi ya kuandika inapaswa kuwa ya kuorodhesha.
  7. Sarufi, inatahusisha vitenzi rahisi, viwakilishi vya nafsi .toa lugha lugha ianyieleweka. mbinu ya kuambukiza sarufi inafaa katika kufundisha sarufi na kuambukiza ruwaza.
KIWANGO CHA JUU
  1. Mchakato wa ukuzaji akili kwa wanafunzi, wanafunzi washiriki kurudiarudia maneno aktika siku zile za mwanzo. Mwl asichanganyikiwe na wanafunzi kutopata mabadiliko katika kipindi kifupi maana ni lugha ngeni kwao, siku za mwanzo wapatie mazoenzi madogomadogo mf: waweze kutaja majina yao na wanakokaa. Mazoezi yalenge kuwakuza uelewa.
  2. Kazi ya mwl. Mwanafunzi hutegemea mwl katika kila kitu kuhusiana na lugha, kazi za vikundi zitumike katika kujijengea uelewa. Mf picha.
  3. Unenaji wa mwl, mwl aongee kwa sauti ya kutosha, mwl atumie misamiati rahisi kabisa na sarufi rahisi kabisa.
Mwl atumie lugha ya kwanza mara chache sana, si vizuri uwaruhusu wanafunzi kutumia lugha zao za kwanza mara kwa mara. Mwl atumie lugha ya kwanza kwa manufaa ya : kuelezea hoja za sarufi 2. Kuonyesha maneno yaloyowachanganyaau kwenye maneno ya kiutamaduni
  1. Hakikisha lugha inayotumika ni lugha inayotua inafuata kanuni za kimawasiliano hivyo ionyeshe uasilia waa lugha isiwe lugha rasmi sana kwa wako katika hatua za awali mf: salamu na utambulisho, mwl hakikisha kuwa ufundishaji   ni rahisi na mfupi. Mwl usiwakatishe tama wanafunzi wako bali wape muda kujifunza.
  2. Ufasaha na usahihi, ufasaha ni muhimu katika hatua hii hakikisha unakuwa katika semi fupifupi mana ni muhimu kuhimizauzungumzaji , usahihi utiliwe mkazo katika sarufi za lugha. Ni muhimu kuangal;ia mahitaji ya wanafunzi katika kuzungumza bila kukosolewa katika kuzungumza. Wape mazoezi ya kisarufi na kifonolojia.
  3. Ubunifu wa wanafunzi, lengo la kujifunza lugha ni kujenga uelewa na kuzalisha kitu kipya ili kuweka ubunifu na utoaji. Katika kiwango cha awali wanafunzi wanaweza kuwa wabunifu kwa kiwango Fulani usitegemee ubunifu mkubwa sana katika lugha.
  4. Mbinu, mbinu rahisi zitumike, anzisha maswali unayoyamiliki yakifuatiwa na maswali ya wanafunzi, pia mbinu ya makundi ni mbinu nzuri sana.
  5. Malengo ya mzungumzaji na msikilizaji, kazi yake ni uasilia wa mawasiliano hakikisha usikilizaji na uzuungumzaji una maana ya mawasiliano.
  6. Malengo ya usomaji na uandishi, katika kiwango cha awali mada ya kusoma na kuandika inatakiwa iwe fupi inayokidhi matakwa ya wahusika kama vile matangazo, kazi ya kuandika inapaswa kuwa ya kuorodhesha.
  7. Sarufi, inatahusisha vitenzi rahisi, viwakilishi vya nafsi .toa lugha lugha ianyieleweka. mbinu ya kuambukiza sarufi inafaa katika kufundisha sarufi na kuambukiza ruwaza.
MUKTADHA WA KIJAMII
Upo katika namna 2
  1. Kijamii na kisiasa na
  2. Kitaasisi
MUKTADHA WA KIJAMII NA KISIASA
Baadhi ya mambo ya kijamii na kisiasa ni pamoja na usahihi na kufaa
Rejesta na mitindo
Semi zinazokubalika katika jamii
Usanifu wa lugha katika kabila na kitaifa
Sera ya lugha katika taifa
Lahaja ya lugha
Katika kipengele hiki tunaangalia muktadha wa kisw kama lugha ya 2 na katika lugha ya kigeni. Unapofikiria muktadha wa lugha ya 2 na lugha ya kigeni fikiri pia nn kinatokea nje ya darasa wanafunzi wanapotoka darasani.
MUKTADHA WA UJIFUNZAJI WA LUGHA YA PILI
Lugha lengwa ya darasani hupatika nje ya darasa. Wanafunzi huweza kuwasiliana kwa lugha yao nje ya darasa. Mfano: Kiswahili Tanzania , kiingereza marekani
–          Lugha ya kigeni muktadha wa ujifunzaji wake (lugha lengwa inayofundishwa|) haipatikani nje ya darasa, wanafunzi huwa na msamiati wa darasani tu. Mfano: kiingereza Tanzania , japan, ujeruman . pia Kiswahili ni lugha ya kigen nchini marekeni, china nk. Njia za ufundishaji katika muktadha wa lugha ya pili ni tofauti na ule
MUKTADHA WA KISWAHILI KAMA LUGHA YA PILI
Mwalimu unapofundisha lugha ya Kiswahili kama lugha ya pili fanya yafuatayo:
  1. Wape kazi nyingi za nyumbani zenye uzungumzaji mahususi ili wayaone yanayotokea mtaani na walinganishe.
  2. Wahimize wanafunze kufanya mazoezi na wazawa
  3. Kusanya makala na magazeti
  4. Wahimize kupata mrejesho sahihi kutoka kwa wazawa.
  5. Wasisistize wanafunzi kutunza kumbukumbu sahihi walizojifunza darasani.
  6. Weka mpango wa kutembelea nyanjani (field trips)
  7. Kuwepo kwa ushirikiano wa wazawa wa lugha. Karibisha hata wazawa darasani
UFUNDISHAJI WA KISWAHILI KAMA LUGHA YA KIGENI
Kunakuwepo na shida katika ufundishaji wa kisw kama lugha ya kigeni kwa kuwa nje ya darasa kunakuwepo na lugha isiyopatikana nje ya darasa.
Muda wa kujifunza ni mdogo katika lugha.
MAMBO YA KUFANYA (MWALIMU)
  1. Mwalimu atumie uasilia wa lugha na mbinu shirikishi.
  2. Hakikisha unatoa motisha mara kwa mara kila utoapo zoezi ili kuwahamasisha wanafunzi.
  3. Wasaidie sana wanafunzi wako ili waone umhimu wa lugha hiyo.
  4. Wape majaribio ya kufanya kazi na usisitize kuyafanya.
  5. Toa fursa za ziada darasani kama radio, tv, magazeti, vitabu, makala nk.
  6. Fanya michezo ya uigizaji na usumuliaji
  7. Leta wazawa waje kuzungumza nao
  8. Weka mbinu za nje kuzitumia nje ya darasa
  9. Unda klabu za lugha.
  1. Ueledi wao
Hapa tunaangalia je ni wanadiplomasia, wanataaluma, wamisionari nk.

MADA YA 4: UTAYARISHAJI WA MUHTASARI (SYLABUS) NA VIFAA VYA KUFUNDISHIA
  1. Utayarishaji wa syalabus katika ufundishaji wa Kiswahili
Syllabus ni muhatasari wa mada zinazokwenda kufundishwa katika kiwango Fulani cha elimu
Mambo ya kuzingatia katika kuandaa syabus
(a)    Malengo ya kozi
(b)   Mada zizingatie uelewa wa wanafunzi kwa kila kiwango: mf, kiwango cha juu, chini au kati
©    Mada zizingatie muktadha wa wanafunzi
(d)   Izingatie uelewa wa wanafunzi, izingatie uelewa wa awali wa wanafunzi.
(e)   Izingatie matakwa na mahitaji ya wanafunzi na jamii kwa ujumla.
(f)     Izingatie muda katika ufundishaji wa kila kiwango.
VIPENGELE
  1. Malengo ya jumla ya kufundisha Kiswahili kwa wageni.
  2. Matokeo ya ujifunzaji
  3. Mada zitakazofundishwa kwa kiwango Fulani
  4. Mbinu za kufundishia mada
  5. Vifaa/zana zitakazotumika katika ufundishaji na ujifunzaji wa lugha.
  1. UTAYARISHAJI WA VITABU VYA KUFUNDISHIA KISWAHILI KWA WAGENI.
(a)    Ni muhimu kuzingatia mtiririko mzuri wa mada / masomo kuanzia somo moja hadi jingine kuanzia rahisi kwenda ngumu. Kuna vipengele vine vya kuazingatia katika uandaaji wa kitabu cha kitabu cha Kiswahili kwa wageni
(i)                  Kurasa za utangulizi, yatolewe maelezo ya utangulizi juu ya historia fupi ya lugha ile ili kusaidia mwanafunzi kujua hali na hadhi ya Kiswahili nchini Tanzania ,
pia sauti za lugha na matamshi lazima zionyeshwe katika utangulizi. Maneno ya lugha mama ya mwnafunzi yatumike kutafsiri maneno ya kigeni kumfanya mwanafunzi kutambua sauti ambazo haziko katika lugha yake.
(ii)                Kurasa zenyewe, Masomo yenyewe yaonyeshe mtiririko wa mada zenyewe
(iii)               Kurasa za mwisho,
(a)    Orodha ya misiamia na semi zilizotumika katika kitabu hicho zionyeshwe na zipangwe kialfabeti kurahisisha uapatikanaji wa msamiati. Ni vizuri orodha hiyo iwe na tafsiri katika lugha ya wanafunzi. Pia kunafaa kuwe na orodha mbili za maneno, maneno ya kigeni na maneno ya lugha mama, lengo la orodha hizo mbili ni kuipa nafasi lugha ya wanafunzi kujifunza lugha ya kigeni. Pia kurasa za mwisho zioneshe majedwali kuonesha sarufi ya lugha inayofundishwa kusaidia upatikanaji wa maneno yaliyo sahihi
  1. UTAYARISHAJI WA SOMO LENYEWE
Mambo ya kufanya
  1. Somo liwe na lengo mahususi kumsaidia mwanafunzi kuwasiliana, mada idokeze nn mwanafunzi atajifunza aweze kuwasiliana na wazawa wa lugha.
  2. Somo liwe na msamiati na sarufi ambavyo vinavyokidhi mahitaji wa mwanafunzi.
Msamiati udhihirike kutokana na mada yenyewe, sarufi imhamasishe mwanafunzi kutaka kuzungumza na si kujua kanuni tu.
  1. Somo lionyeshe lugha inavyozungumzwa na wazungumzaji.
  2. Somo liwe na vielelezo vya mazingira halisi na taarifa muhimu za kiutamaduni wa lugha ambayo mwanafunzi anajifunza. Pia aelezwe kuwa salamu yaweza kuwa fupi au ndefu. Mf: shikamoo: hutolewa na mdogo kwa mkubwa. Kifamilia si mme mke na watoto tu bali hata ndugu wa karibu wa lugha hiyo.
  3. Somo liambatane na vielezo kama vitu halisi kama picha, vielelezo,nyimbo, matangazo magazeti, ramani hasa katika hatua ya kwanza. Nk. Lengo la vielelezo ni kumuingiza mwanafunzi ndani ya lugha, utamaduni wa lugha ili aweze kujieleza.
  4. Kila somo liwe na mazoezi halisi wa stadi za lugha mazoezi hayo yatokane na matini au vielelezo vilivyoandamana na masomo hayo. Mazoezi yamwezeshe mwanafunzi kupata umahiri wa uamilifu wa lugha na kukuza mawasiliano. Baada ya kila somo lielezwe mwanafunzi akafanye nn baada ya somo.
UWASILISHAJI WA DARASANI 22/04/2014 KIPINDI CHA JIONI
Swali: Jadili mbinu ya mawasiliano inavyoweza kutumiwa na mwalimu katika kufundisha Kiswahili kwa wageni.
Richard 1996
Mbinu hii ilikuwa katika bara la ulaya na kupelekea kuongezeka kwa wahamiaji na hivyo kukawa na mahitaji makubwa ya wanafunzi wa lugha za kigeni.
Misingi ya ufundishaji
  1. Kujikita katika uwezo wa kuwasiliana katika lugha wanayofundishwa wanafunzi na usijikite katika sarufi ya lugha.
  2. Wanafunzi wapewe nafasi ya kuzungumza kile wanachokijua kuhusu lugha kwa kutumia uwezo wao.
  3. Mwalimu awe mvumilivu pale wanafunzi wanapokuwa wamekosea kwa sababu hawana misingi ya lugha hiyo.
  4. Ufundishaji lugha uzingatie misingi halisi ya maisha
  5. Umilisi wa mawasiliano kwa kutofautisha wapi pakutumia lugha rasmi na wapi pasipo pa kutumia lugha rasmi. Chanzo>>>>>
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)