01-09-2022, 10:18 PM
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'AMIRI'
Neno amiri katika lugha ya Kiswahili lina maana zifuatazo:
1. Nomino: [Ngeli: a-/wa-, wingi: maamiri ] mtoto wa mfalme; mwana mfalme.
2. Nomino: [Ngeli: a-/wa-] kiongozi mwenye mamlaka ya kutoa amri.
Mfano: kiongozi mkuu, amiri jeshi mkuu: mtu mwenye cheo kikubwa kijeshi anayetoa mwongozo kwa wanajeshi wengine walio chini yake.
2. Kitenzi si elekezi: amir.i anza kufanya jambo; anzisha ( Minyumbuliko : amiria, amirika, amirisha, amiriwa.)
Katika lugha ya Kiarabu, neno hili amiri(soma: amiirun/amiiran/amiirin امير) ni nomino inayotokana na kitenzi cha Kiarabu amura أمر ameamrisha , lenye maana: mwenye kutoa amri.
Maana zingine za neno (amiri) katika Kiarabu ni:
1. Mfalme
2. Mtoto wa mfalme.
3. Mtawala.
4. Mshauri.
5. Jirani.
6. Lakabu ya kiongozi wa Waislamu, amiru al-Muuminiina (soma: Amirul Muuminiina Kiongozi Mkuu wa Waislamu امير المؤمنين ).
Kinachodhihiri ni kuwa neno amiiri (soma: amiirun/amiiran/amiirin امير ) lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno amiri lilichukua baadhi ya maana zake kutoka Kiarabu na kuziacha maana zingine.
Shukran sana.
Khamis S.M. Mataka.
Neno amiri katika lugha ya Kiswahili lina maana zifuatazo:
1. Nomino: [Ngeli: a-/wa-, wingi: maamiri ] mtoto wa mfalme; mwana mfalme.
2. Nomino: [Ngeli: a-/wa-] kiongozi mwenye mamlaka ya kutoa amri.
Mfano: kiongozi mkuu, amiri jeshi mkuu: mtu mwenye cheo kikubwa kijeshi anayetoa mwongozo kwa wanajeshi wengine walio chini yake.
2. Kitenzi si elekezi: amir.i anza kufanya jambo; anzisha ( Minyumbuliko : amiria, amirika, amirisha, amiriwa.)
Katika lugha ya Kiarabu, neno hili amiri(soma: amiirun/amiiran/amiirin امير) ni nomino inayotokana na kitenzi cha Kiarabu amura أمر ameamrisha , lenye maana: mwenye kutoa amri.
Maana zingine za neno (amiri) katika Kiarabu ni:
1. Mfalme
2. Mtoto wa mfalme.
3. Mtawala.
4. Mshauri.
5. Jirani.
6. Lakabu ya kiongozi wa Waislamu, amiru al-Muuminiina (soma: Amirul Muuminiina Kiongozi Mkuu wa Waislamu امير المؤمنين ).
Kinachodhihiri ni kuwa neno amiiri (soma: amiirun/amiiran/amiirin امير ) lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno amiri lilichukua baadhi ya maana zake kutoka Kiarabu na kuziacha maana zingine.
Shukran sana.
Khamis S.M. Mataka.
Mwl Maeda