MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
ETIMOLOJIA YA NENO 'AMIRI'

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
ETIMOLOJIA YA NENO 'AMIRI'
#1
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'AMIRI'

Neno amiri katika lugha ya Kiswahili lina maana zifuatazo:

1. Nomino: [Ngeli: a-/wa-, wingi: maamiri ] mtoto wa mfalme; mwana mfalme.

2. Nomino: [Ngeli: a-/wa-] kiongozi mwenye mamlaka ya kutoa amri.

Mfano: kiongozi mkuu, amiri jeshi mkuu: mtu mwenye cheo kikubwa kijeshi anayetoa mwongozo kwa wanajeshi wengine walio chini yake.

2. Kitenzi si elekezi:  amir.i anza kufanya jambo; anzisha ( Minyumbuliko : amiria, amirika, amirisha, amiriwa.)

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili amiri(soma: amiirun/amiiran/amiirin امير) ni nomino inayotokana na kitenzi cha Kiarabu amura أمر ameamrisha , lenye maana: mwenye kutoa amri.

Maana zingine za neno (amiri) katika Kiarabu ni:

1. Mfalme

2. Mtoto wa mfalme.

3. Mtawala.

4. Mshauri.

5. Jirani.

6. Lakabu ya kiongozi wa Waislamu, amiru al-Muuminiina (soma: Amirul Muuminiina Kiongozi Mkuu wa Waislamu امير المؤمنين ).

Kinachodhihiri ni kuwa neno amiiri (soma: amiirun/amiiran/amiirin امير ) lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno amiri  lilichukua baadhi ya maana zake kutoka Kiarabu na kuziacha maana zingine.

Shukran sana.

Khamis S.M. Mataka.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)