01-09-2022, 06:28 PM
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'HALMASHAURI'
Neno *halmashauri* katika lugha ya Kiswahili lina maana zifuatazo:
1. *Nomino: [Ngeli: i-/zi-]* kikundi cha watu waliochaguliwa au kuteuliwa kufanya kazi ya kuwa watawala, watunga sheria, washauri au kuelekeza jambo fulani.
2. *Nomino: [Ngeli: i-/zi-]* chombo cha kiutawala katika wilaya au mji.
2. *Nomino: [Ngeli: i-/zi-]* kundi la watu waliochaguliwa au kuteuliwa kuelekeza utendaji wa shughuli fulani.
Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *halmashauri* ni naneno mawili ya Kiarabu yaliyowekwa pamoja; neno *ahlu* (soma: *ahlu/ahla/ahli اهل)* lenye maana ya *watu, -enye,* na neno *mashauri* (soma:*mashuuratun /mashuuratan/mashuuratin* *مشورة* ) pia *mash-wara* (soma: *mash-waratun/mash-waratan/mash-waratin مشورة)* lenye maana zifuatazo:
1. Kinachotolewa nasaha kwa rai au namna nyingine.
2. Ushauri.
3. Nasaha, muongozo.
Kinachodhihiri ni kuwa maneno haya mawili *ahlu mashuurat/mash-warat* yaliipoingia katika Kiswahili na kutoholewa, neno jipya la Kiswahili *halmashauri* lilipatikana.
Katika lugha ya Kiarabu neno *shuuraa شورى* linatumika kwa kisawe cha maneno *mashuurat مشورة* na *mash-warat مشورة* na hupatikana misamiati *ahlu al-shuuraa* (soma: *ahlush shuraa اهل الشورى washauri)* na *majlis al-shuuraa* (soma: *majlisush shuraa مجلس الشورى baraza la ushauri; bunge).*
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*
Neno *halmashauri* katika lugha ya Kiswahili lina maana zifuatazo:
1. *Nomino: [Ngeli: i-/zi-]* kikundi cha watu waliochaguliwa au kuteuliwa kufanya kazi ya kuwa watawala, watunga sheria, washauri au kuelekeza jambo fulani.
2. *Nomino: [Ngeli: i-/zi-]* chombo cha kiutawala katika wilaya au mji.
2. *Nomino: [Ngeli: i-/zi-]* kundi la watu waliochaguliwa au kuteuliwa kuelekeza utendaji wa shughuli fulani.
Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *halmashauri* ni naneno mawili ya Kiarabu yaliyowekwa pamoja; neno *ahlu* (soma: *ahlu/ahla/ahli اهل)* lenye maana ya *watu, -enye,* na neno *mashauri* (soma:*mashuuratun /mashuuratan/mashuuratin* *مشورة* ) pia *mash-wara* (soma: *mash-waratun/mash-waratan/mash-waratin مشورة)* lenye maana zifuatazo:
1. Kinachotolewa nasaha kwa rai au namna nyingine.
2. Ushauri.
3. Nasaha, muongozo.
Kinachodhihiri ni kuwa maneno haya mawili *ahlu mashuurat/mash-warat* yaliipoingia katika Kiswahili na kutoholewa, neno jipya la Kiswahili *halmashauri* lilipatikana.
Katika lugha ya Kiarabu neno *shuuraa شورى* linatumika kwa kisawe cha maneno *mashuurat مشورة* na *mash-warat مشورة* na hupatikana misamiati *ahlu al-shuuraa* (soma: *ahlush shuraa اهل الشورى washauri)* na *majlis al-shuuraa* (soma: *majlisush shuraa مجلس الشورى baraza la ushauri; bunge).*
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*
Mwl Maeda