MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
ETIMOLOJIA YA NENO ' JAALA', 'JALIA' 'JALI.A/JAALI.A' na 'MAJALIWA'

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
ETIMOLOJIA YA NENO ' JAALA', 'JALIA' 'JALI.A/JAALI.A' na 'MAJALIWA'
#1
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO ' JAALA', 'JALIA' 'JALI.A/JAALI.A' na 'MAJALIWA'

Neno *jaala*[ *Ngeli: i-/i-]* katika lugha ya Kiswahili ni nomino yenye maana ya' mambo yafanyikayo kwa mapenzi/uwezo wa Mwenyezi Mungu'.

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *jaala* (soma: *ja-a-la جعل)* ni kitenzi cha Kiarabu chenye maana zifuatazo:

1. Amefanya kitu fulani kiwepo.

2. Ametoa kitu kumpa mtu mwengine.

3. Ameanza jambo fulani.

4. (Kwa Mwenyeezi Mungu tu) Ameumba.

5. Ametengeneza.

Neno *jalia*[ *Ngeli: a-]* katika lugha ya Kiswahili ni kisawe cha neno *jalali* [ *Ngeli: a-]*  lenye maana ya 'jina la kumtaja Mwenyeezi  Mungu kwa sifa yake ya kuwa utukufu mwingi'.

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *jalali* (soma: *jalaalun/jalaalan/jalaalin جلال)* ni nomino ya Kiarabu yenye maana zifuatazo:

1. Utukufu. Mwenyeezi Mungu hutajwa kuwa *Dhul Jalaali*  *ذو* *الجلال* mwenye utukufu.

2. -enye cheo/hadhi kubwa.

3. Kilicho kikubwa zaidi.

Maneno *jali.a/jaali.a*[ *Vitenzi Elekezi* ] katika lugha ya Kiswahili vina maana ya 'fanya uwezekano, saidia, wezesha: Mwenyeezi Mungu *akitujalia/akitujaalia* uhai tutaonana.

Neno hili linaponyambuliwa tunapata vitenzi: *jaalika, jaalisha na jaaliwa.*

Neno *majaliwa*[ *Ngeli: ya-/ya-]* katika lugha ya Kiswahili ni nomino yenye maana ya' mambo yafanyikayo kwa uwezo/mapenzi ya Mwenyezi Mungu'.

Maneno ' *jaala* ' na ' *majaliwa* ' ni visawe.

Neno ' *majaliwa* ' halina mfano wake kimatamshi katika lugha ya Kiarabu bali yumkini limebuniwa kutokana na nomino ' *jaala* ' au kitenzi ' *jaalia/jaaliwa*'.

Kitenzi ' *jali.a/jaali.a'* kinamhusu Mwenyeezi  Mungu tu kwa maana ya kumpa mtu uwezo wa kupata au kuweza kufanya jambo fulani.

Kinachodhihiri ni kuwa neno *jaala* ( *soma: ja-a-la  جعل*) ambalo ni kitenzi katika lugha ya Kiarabu lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *jaala* limekuwa nomino kwa maana ya 'mambo yafanyikayo kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu'.
Kiujumla, maneno yote haya hayakuepukana na maana zake katika lugha ya asili - Kiarabu.

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)